Mwakalabela afungiwa miaka mitano kutojihusisha na soka

Mwakalabela afungiwa miaka mitano kutojihusisha na soka

Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, Fredrick Mwakalebela hatotakiwa kujishughulisha na mpira wa miguu ndani na nje ya nchi kwa kosa la kutoa maneno ya uchochezi kwa nia ya kuwachochea mashabiki wa Yanga dhidi ya vyombo vinavyosimamia mpira wa miguu nchini

Maamuzi hayo yamefikiwa na Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) baada ya kupokea malalamiko yaliyotolewa Februari 19 alipokuwa akizungumza na wanahabari ambapo alisema TFF na TPLB vinaihujumu Yanga

Mwakalebela amemtozwa faini ya Tsh. Milioni 5 kwa kosa la maadili. Pia ametozwa Tsh milioni 2 kwa kosa la kuta taarifa za uongo juu ya mkataba kati ya mchezaji Bernad Morrison na klabu ya Simba
1617353096810.png
 
Nakumbuka tulimwambia ajiandae kula mvua kutoka mamlaka husika

Alitaka kuwafurahisha mashabiki bila kujali kanuni na sheria za kandanda
hapo amewahi kiongozi TFF inakuwaje hajui kanuni. Jamaa wanaongoza timu kihunihuni
 
Huu Ulikuwa Mzigo Pale Jangwani...Sasa Umebaki mzigo mmoja.Nao bora Wangeuondoa. Haiwezekani Timu Iwe inaongoza Ligi Lakini Mashabiki hawana Raha Wala Hawajiamini.
 
Tunamuomba mama Samia aangalie hii TFF na maamuzi yao. Wanafanya maamuzi ya kipuuzi kuua soka letu
 
Daah huyu jamaa nae alikuwa anaropoka sana, alikuwa hata hajui anafanya nini?
Badala ya kuiongoza yanga ifike pazuri lakini yeye ndio alikuwa tatizo pale yanga, kelele, figisu na majungu yeye ndo mpikaji pale jangwani.
 
Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, Fredrick Mwakalebela hatotakiwa kujishughulisha na mpira wa miguu ndani na nje ya nchi kwa kosa la kutoa maneno ya uchochezi kwa nia ya kuwachochea mashabiki wa Yanga dhidi ya vyombo vinavyosimamia mpira wa miguu nchini

Maamuzi hayo yamefikiwa na Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) baada ya kupokea malalamiko yaliyotolewa Februari 19 alipokuwa akizungumza na wanahabari ambapo alisema TFF na TPLB vinaihujumu Yanga

Mwakalebela amemtozwa faini ya Tsh. Milioni 5 kwa kosa la maadili. Pia ametozwa Tsh milioni 2 kwa kosa la kuta taarifa za uongo juu ya mkataba kati ya mchezaji Bernad Morrison na klabu ya Simba
View attachment 1741073
YOUNG AFRICAN Semeni chochote hapa
 
Hv ktk hili katazo la miaka mi5 ndani na Nje ya Nchi... Je? Anaruhusiwa kushiriki Football BETTING?

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
Haruhusiwi... Ni marufuku nje na ndani... Afanye shughuli zingine lakini sio mpira, hata mkimuona bar ana cheki mpira wa Liverpool toeni taarifa tff tafadhari...
 
[emoji3][emoji3][emoji3]hili halimo kwenye katazo
Kujihusisha na mpira ni eneo kubwa tena nje na ndani... Kama ni betting za farasi au magari sawa...

Yani huyu hata kuangalia mpira hatakiwi, na itakuwa ngumu kumuona majukwaani taifa ktk kipindi chote cha adhabu... Hata kutangaza au kuchambua...
 
Tunamuomba mama Samia aangalie hii TFF na maamuzi yao. Wanafanya maamuzi ya kipuuzi kuua soka letu
Mama ana kazi nyingi za kufanya, kwani boss wenu kilo 800 wakati anaenda kulopoka alijua Tff itampigia makofii eeh
 
Tunamuomba mama Samia aangalie hii TFF na maamuzi yao. Wanafanya maamuzi ya kipuuzi kuua soka letu
Ulitaka aachwe na uzushi wake? Kufuata Sheria Ni kuua soka?


Alikuwa analalamikia TFF mwishowe Utopolo wote wakajua kuwa Hawana timu ya kutwaa ubingwa.

Safi Sana [emoji1376][emoji1376][emoji1376]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom