Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sasa kisha onyesha nia yake ni kubaki kule cWT mumuache aende, tatizo la watu kama wewe mnadhani roho mbaya ni sifa. Yeye hataki kurejea Temeke anataka kubaki CWT, kwanini msimwache afanye anachotaka? kwanini kulazimishana? mwajiri mkuu, mwajiri mkuu kwani serikali ni Mungu? Tumieni busara na hekima mumuache akafanye apendacho, mkimlazimisha mnapata nini?Tumeambiwa aliomba kibali Utumishi,sasa mm na ww tujiulize Hv kibali huwa hakiishi ,mm naamini kibali kinaisha kulingana na muda uliopewa.JANETH hakuajiriwa CWT,waliomuajiri ndio walimpa kibali pale alipoomba kutumikia CWT,Kumbuka mwajiri mkuu ni serikali ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na CWT sio mwajiri na kuigomea serikali iliyokupa kibali kwenda huko uliko ni kosa lingine,kama kibali kimeisha muda wake basi turudi tulipotokea ndio busara kuliko kuwa na kiburi kisicho na maana.Angeenda kutumikia CWT bila kibali kutoka Ofisi ya Utumishi kwa muda wote ambao amekuwa huko,ningewashangaa sana Utumishi kumtaka arudi kule alikokuwa ilhali hawakumuandikia kibali.Ni vema tukazingatia taratibu za Utumishi na tusi sikilize bush loyals ambao mwisho wa siku hawana cha kutusaidia.
Arudi Temeke tu kwa sababu hakusomea ukatibu mkuu alisomea ualimu.Sasa kisha onyesha nia yake ni kubaki kule cWT mumuache aende, tatizo la watu kama wewe mnadhani roho mbaya ni sifa. Yeye hataki kurejea Temeke anataka kubaki CWT, kwanini msimwache afanye anachotaka? kwanini kulazimishana? mwajiri mkuu, mwajiri mkuu kwani serikali ni Mungu? Tumieni busara na hekima mumuache akafanye apendacho, mkimlazimisha mnapata nini?
Hata hela za serikalini zinaliwa hovyo hilo pia ujueLet's assume kwamba huyo Maganga amezuia serikali isichote pesa huko Cwt kwa maelezo yako.Je hizo hela za walimu zimekuwa safe kiasi gani na lini ? Mbona bado kuna malalamiko kibao kwamba huko Cwt hela za walimu zinatafunwa ovyo ni kama hazina mwenyewe na ripoti ya CAG ya mwaka 2017/2018 ilithibitisha hivyo na mwaka huo huyo Maganga alikuwa kiongozi huko Cwt .Niombe mama Samia akiona inafaa atume tena CAG aone ni kwa namna gani hela za walimu wetu zinakuwa monitored tangu ukaguzi wa mwisho enzi za Magu
Heri wanaokula hela za serikali kuliko kikundi cha watu kilichojimobilise kwa jina la Cwt na kutafuna hela za walimu wetu maskini bila soniHata hela za serikalini zinaliwa hovyo hilo pia ujue
Mzee hii picha mbona inafikirisha hivo, walikuwa wanampa bahasha , jamaa akagoma
Jamiiforum ni hela yako tu ukitaka kumchafua mtu mwaga hela kwa viongozi wa JF utamchafua mpaka uchoke na ukitaka usichafuliwe fanya ivoivoNimeona hata Jamii Forum wameandika habari hii kishabiki ,Jamii Forum ni chombo cha kutetea wananchi ,nilitegemea viongozi wa jamii Forum chini ya mtu bingwa @maxmello wangekua mstari wa mbele kuwa katika jukwaa la utetezi wa viongozi wa vyama vya Wafanyakazi kwa kusoma sheria ya kazi na mahusiano kazini ,pamoja na kusoma mkataba namba 87 wa ILO na Mkataba namba 98
Lakini wameandika taarifa kama gazeti la Nipashe ambalo limenunuliwa na kundi lililokua na mirija CWT sasa imekatwa,sitaki kusema kuwa JF nayo itakua imewekwa mfukoni baadhi ya watendaji wake .ndio maana hawataki kuchimba ukweli
Mbona Dr Mhina aliekua Mkurugenzi serikali za Mitaa pale TAMISEMI aliteuliwa kuwa DC ,akwenda na haikuandikwa kuwa ni mgomo kwa Rais ..
Sheria ya ajira na mahusiano kazini namba 7 ya mwaka 2004 inapiga marufuku kukata mshahara wa mtumishi pasipo ridhaa ya mwajiriwa anayoitoa kwa mwajiri wake kwa kujaza fomu iitwayo Tuf 15 na kutuma maombi ya kujiunga kwenye chama cha wafanyakazi. Ila kwa bahati mbaya siwitiii wakishirikiana na maafisa utumishi kwa makusudi wameamua kwa makusudi kuikanyaga sheria halali kwakuingiza makato kwenye check number za walimu pasipo indorsement za wenye mishahara hasa kwa walimu walioanza kazi kuanzia mwaka 2015 kurudi nyuma .Hivi hao Cwt kiburi cha kudharau sheria hiyo halali ya nchi mpaka sasa watendaji wake wamediriki mpaka kukataa teuzi toka kwa mh Rais wanakipata wapi?
Hata ile kupewa ukuu wa wilaya ilikuwa ni mipango ya kuelewa wamnase vipi. Akastuka. Ana team kiubwa sana nyuma yake.Kwanini aandamwe kipindi hiki baada ya kuukataa uCHAWA? Kwani kuwa chawa lazima?
Hiyo kitu nimesikia ila nilikuwa sijui huyu uliyemtajaNdg, tpaul na wasomaji wengine.
Mie naujua mgogoro huu wa CWT nje ndani. Kufupisha ni kwamba huu mgogoro hauwezi kuisha kamwe hadi siku Mh. Jenista Mhagama, atakapopoteza uwaziri wake.
Huyu ndiye injinia wa kuanzia uteuzi wa hawa kina maganga kwenda kuwa wakuu wa wilaya.
Katika hili hata mh. Rais Samia nakiri ni majina tu aliletewa na wala hakuwajua.
Mhagama na aliyekuwa Rais wa CWT aliyefungwa kwa matumizi mabaya ya ofisi, ambae aliwahi kuhudumu ktk chama cha walimu, na ndio kisa cha mbivu na mbichi huko CWT.
Kiufupi Mhagama na mkubwa wake flani walikuwa kwenye payroll ya CWT, hawa kina maganga waliwatoa.
Stori ni ndefu. Ipo siku nitaiandika yote.
Ogopa sana mirija ya fedha na siasa za ovyo.
Yeye amechagua kutoenda kufundisha na pia aliukataa uchawa. Wewe unatakaje?Sio lazima na hata yeye sio chawa, ila ni Mwalimu na kituo chake ni Temeke kuna maelfu na maelfu ya walimu ambao wanaweza kuongoza hiko chama kama muajiri kakataa arudi kwenye kazi aliyoiomba
Sasa mbona wanaogopa kumfuta kazi? Unadhani yeye hawasomi? Kama kweli wana ubavu wamfute kazi awawashie moto wa makaa ya mawe.Hata ile kupewa ukuu wa wilaya ilikuwa ni mipango ya kuelewa wamnase vipi. Akastuka. Ana team kiubwa sana nyuma yake.
Kila mtu ashinde mechi zakeYeye amechagua kutoenda kufundisha na pia aliukataa uchawa. Wewe unatakaje
Kuitwa kazini ni suala la binafsi kati ya mtumishi na mwajiri. Kwanini mwajiri anafanya suala la mtumishi mmoja katika halmashauri yake kuwa la kitaifa? Wewe unadhani mwajiri hajavunja haki ya faragha ya mtumishi huyu?Mwajiri ana haki ya kukuita kazini. Mnamjaza tuu huyu Jamaa.
Reading between the lines....wanataka kumtumia kama case study kwa watumishi wengine kwamba wasijisahau wanapokuwa kwenye secondment kama huyo bwana...kwamba ukijisahau mwajiri wako anao uwezo wa kutia kitumbua chako mchanga kama ambavyo watatia kitumbua cha huyo mwalimu mchanga.Mbona walimu wengi tu, kwanini wanalazimisha mwalimu asiyetaka kufundisha? Haya ni matumizi mabaya ya ofisi za umma. Kiongozi unapotumia wadhifa wako kuadhibu watu badala ya kutatua matatizo ya watu. Mwalimu humlipi mshahara, analipwa na CWT. Yeye anataka kuendelea kuwa huko, nyie hamtoi sababu ya kwanini mnataka arejee, mmegeuka miungu. Hamtaki tu, bila sababu yoyote.
Nyumbu wanamjaza ujinga wa kushindana na mwajiri wake!Huyo naye akafundishe huko Temeke hakusomea kuwa katibu wa cwt.