Mwalimu Maganga, Katibu Mkuu CWT aliyekataa uteuzi wa Ukuu wa Wilaya arudishwa kwenye Ualimu

Mwalimu Maganga, Katibu Mkuu CWT aliyekataa uteuzi wa Ukuu wa Wilaya arudishwa kwenye Ualimu

Hizi ndizo akili za watanzania maana 99.9% ni machawa hawana msimamo na wala hawafuati wanachotaka.
Yeye hakutaka uteuzi akakataa, ila watu wanamnanga kama vile kuna kosa alilofanaya
Ni akili za kimasikini na kifukara sana.

Kuna watu hawataki kazi fulani tu, bila kujali zina heshima gani, zina fursa gani, hawazitaki tu.

Tuheshimu maamuzi yao.

Zaidi, serikali inapokuteua na kutangaza uteuzi bila hata kukuambia wewe kabla ya kutangaza uteuzi, ni kama imekudharau fulani hivi kwamba ni lazima ukubali uteuzi.

Kuna watu wana commitments za kifamilia, kijamii etc, hawawezi kuacha maisha yao sehemu fulani mara moja waende sehemu nyingine kisa uteuzi wa rais.

Mimi nilifurahi kusikia kuna watu wamekataa teuzi, serikali iwape hawa watu hata professional courtesy ya kuwaarifu kabla ya kutangaza, na kuwapa nafasi ya kukubali au kukataa uteuzi, rais asije kuaibika kukataliwa uteuzi na mteule wake.
 
Bwana Maganga ana akili sana tena kuzidi wewe mtoa mada alijua fika kuwa cheo cha ukuu wa wilaya ni cheo cha kwenda kudhalilishwa na alikuwa ametegwa ali atenguliwe na kupigwa bench kwa mgongo wa kupangiwa kazi nyingine …kwa hiyo alikuwa mbele ya muda na alifikiri zaidi yako….

Hivi kwa akili yako kabisa alikataa tuu bila kujua kitakachotokea? Alijua fika…
Bora afundishe kwa uhuru kabisa kuliko kwenda kudhalilishwa kwenye ukuu wa wilaya…
Yuko wapi jerry muro? Leo tuu mkuu wa wilaya ya Mtwara katenguliwa…

Alifanya jambo sahihi kabisa
Unahisi angeeenda afu akatenguliwa asingeweza kurudi kwenye kazi yake ya awali ya ualimu...?
Hapana angerudi tu na kuendelea kuwa mwalimu wa daraja A, Kwa ufupi alipisha na gari la mshahara....
 
Mnavyo toa maoni utadhani jamaa amefungwa jela maisha🤔🤔, amesha pata pesa ya kutosha kwenye ukatibu sasa anarudi kwenye kazi yake aliyo izoea huku akiendelea kula pesheni yake taratiiiibu,
 
Sasa unajua pesa aliyokuwa anapata kama Katibu Mkuu CWT ni kubwa na Ingeweza kulingana na Pesa ya Mkuu wa wilaya.

Ila kwa sasa anapelekwa kurudi kama Mwalimu mwandamizi Daraja A unajua anapata kiasi gani na atafundisha Shule ya msingi unajua udhalilishaji na majuto atakayopata maana hata diwani atakuwa boss wake sasa....KIPI NI BORA?
Kwani lazima arudi huko?? Akiamua kujiajiri inakuwaje?? Hizi tabia za kibongo za kuviziana na kukomoana ndizo zinatuharibia maendeleo kama nchi! Hovyo kabisa!!
 
Mantiki ya taarifa za mwajiriwa kuwekwa hadharani ni zipi?

Alipaswa apewe barua yake kisha aripoti kazini. Kubandikwa kwenye mbao za matangazo ni upuuzi usio na maana.

Mbona kabla ya hapo, vibali vyake havikuwa wazi?

Pathetic!.
Kwenye hii dunia ukijifanya mjinga basi watu wanakujibu kulingana na ujinga wako ili uelewe kirahisi. Hiyo ndo lugha anayoweza kuelewa kirahisi huyo Mwalimu
 
Sasa unajua pesa aliyokuwa anapata kama Katibu Mkuu CWT ni kubwa na Ingeweza kulingana na Pesa ya Mkuu wa wilaya.

Ila kwa sasa anapelekwa kurudi kama Mwalimu mwandamizi Daraja A unajua anapata kiasi gani na atafundisha Shule ya msingi unajua udhalilishaji na majuto atakayopata maana hata diwani atakuwa boss wake sasa....KIPI NI BORA?
Kwa taarifa yako hata angekubali uteuzi ule hadi sasa asingelikuwa mkuu wa wilaya…lengo lilikuwa ni kuwakomesha ukuu wa wilaya ilikuwa njia ya kuwachomoa na kuwahadhiri walijua fika
 
Mantiki ya taarifa za mwajiriwa kuwekwa hadharani ni zipi?

Alipaswa apewe barua yake kisha aripoti kazini. Kubandikwa kwenye mbao za matangazo ni upuuzi usio na maana.

Mbona kabla ya hapo, vibali vyake havikuwa wazi?

Pathetic!.
Hata mimi nashangaa sana.

Lakini ndo hivyo tena imeshafanyika. Na bila shaka haya ndiyo "maagizo toka juu" maana nakumbuka boss wao mkuu Rais Samia just recently alipokuwa anafungua kile kikao cha TCD alisema hili kuwa na watu wanaopewa kazi na serikali halafu wanakataa, hao hawastahili

Kwa hiyo obviously, hilo ni agizo la kumdhalilisha mwalimu huyu.

Hivi ndivyo serikali ya CCM inavyoji behave, kishetani shetani tu.
 
Cha ajabu mkurugenzi sio aliyepost ila afisa habari wa Tamisemi ndo kapost najiuliza imekuwaje wizara itume report ya Mamlaka ya manispaa
Ili kumdhalilisha tuu…najiuliza utaratibu huu umeanza lini?
 
Hii inanikumbusha kauli moja iliwahi kusemwa na wahenga kuwa ukibebwa bebeka na ukilishwa kamwe using'ate kidole kikulishacho!

Hatimaye rasmi sasa bwana huyo kukiona cha moto kwa kurudishwa kituo chake cha kazi kama Mwalimu Mwandamizi Daraja A katika Manispaa ya Temeke.

Ikumbukwe kwamba Ndg. Japhet Maganga na Viongozi wenzake wa CWT walikataa uteuzi huo January mwaka huu na wakasahau kwamba wanafanya kazi katika serikali hiyo hiyo yenye mamlaka ya kuwasubiri (hii imedhihirisha usemi wa aliye juu mgonje chini)

Leo nilishtuka baada ya kuona barua hii Kutoka Tamisemi ikiwa imeandikwa na manispaa ya Temeke. Maelezo yote yapo kwenye barua hii;

USAHIHI ni kuwa "AMEKATALIWA KUPEWA KIBALI NA KURUDISHWA KUFUNDISHA DARASANI" na sio "KURUDISHWA KWENYE UALIMU" kwa sababu siku zote yeye amekuwa ni mwalimu na hata kama akistaafu au akifa bado atakufa au kustaafu na UALIMU wake
 
Mantiki ya taarifa za mwajiriwa kuwekwa hadharani ni zipi?

Alipaswa apewe barua yake kisha aripoti kazini. Kubandikwa kwenye mbao za matangazo ni upuuzi usio na maana.

Mbona kabla ya hapo, vibali vyake havikuwa wazi?

Pathetic!.
Kiukweli nimeshangaaa sana Kumbe ni Mwalimu. Maana ya Ualimu naona haijui. Ni muhimu apangiwe majukumu Mengine kwenye ualimu hatoshi
 
Kulazimisha uchawa au ukada kwenye vyama vya wafanyakazi si sawa kabisa. Teuzi hizo hazikuwa za nia njema, waliozikataa wanastahili hongera na naamini watanzania watawapa nafasi kwa mlango mwingine Kiongozi.
 
Mwalimu Japhet maganga aliyekuwa katibu mkuu wa chama cha walimu Tanzania na aliyegomea teuzi ya ukuu wa wilaya kutoka Kwa bi Mkubwa namba moja anahitajika kuripoti kituo chake cha kazi Baada ya ombi lake kukataliwa na katibu mkuu utumishi
20230923_205104.jpg
 
Bwana Maganga ana akili sana tena kuzidi wewe mtoa mada alijua fika kuwa cheo cha ukuu wa wilaya ni cheo cha kwenda kudhalilishwa na alikuwa ametegwa ali atenguliwe na kupigwa bench kwa mgongo wa kupangiwa kazi nyingine …kwa hiyo alikuwa mbele ya muda na alifikiri zaidi yako….

Hivi kwa akili yako kabisa alikataa tuu bila kujua kitakachotokea? Alijua fika…
Bora afundishe kwa uhuru kabisa kuliko kwenda kudhalilishwa kwenye ukuu wa wilaya…
Yuko wapi jerry muro? Leo tuu mkuu wa wilaya ya Mtwara katenguliwa…

Alifanya jambo sahihi kabisa
Umenena vyema ndugu yangu, huyu mwalimu alikua mbele ya muda kifikra kuliko wengi wetu na Phd zao.
 
Daaah pole yake sana... tusifurahie anguko la wenzetu... hii tabia ya kukomeshana imejaa sana zerikalini.

Wangempa tu hitaji la moyo wake
 
Waalimu wanachama wa CWT - Chama cha Waalimu Tanzania waonyeshe solidarity na waandamane kupinga viongozi wao kuburuzwa na watawala.
Kuburuzwa vipi wakati ajira yake rasmi ni tamisemi.. huko kwengine alikuwa anafanya kwa ruhusa ya mwajiri wake
 
Back
Top Bottom