Mwalimu mwenye kujua kazi ya 2% ya makato ya Mshahara wake kwenda CWT tukutane hapa

Mwalimu mwenye kujua kazi ya 2% ya makato ya Mshahara wake kwenda CWT tukutane hapa

Wanaumaga maneno tu.

Eti kuboresha maslahi ya wafanyakazi,

Maslahi gani Kwa mfano?

Kuongezeka Kwa mishahara hadi Rais apende asipopenda basi.

Maslahi gani ya watumishi wanayoshughukia Na kuboreshwa?

Hata vyama vingine ni hivyo hivyo kina tukta.

Bongo bahati mbaya aisee!

Yaani hawamuogopi Mungu ?
 
Hakika hili SUALA linatatiza sana ,inabidi siku Serikali walitolee MAELEZO, kama ni suala la SHERIA basi zipelekwe ,Bungeni kubadilishwa.

Napendekeza
1.Kwanza iwe HIARI,
2.Pili isiwe kwa % itamkwe kwa AMOUNT/FIGURE kwamba kila mfanyakazi atachangia 1000/=Tsh kwa mwezi..kwa kuwa CHANGAMOTO/MATATIZO huwa almost sawa kwa wafanyakazi wote
 
Samahani mkuu,kuna chama ambacho hawakatwi? Maana hata huku TUGHE tunakatwa vile vile lakini naona mnawajadili walimu tu..
Kwanza nieleweke, sipingi wafanyakazi kuwa wananchama wa vyama vya wafanyakazi, na pia kulipa ada ya kuendeshea hivyo vyama (Trade Unions).

Hoja yangu iko sehemu moja tu. Vyama vya wafanyakazi vikusanye michango ya ada kwa wanachama wake kwa usawa! Yaani wanachama wote watozwe viwango sawa vya ada kila mwezi.

Kinachofanywa na CWT ndiyo kinacholalamikiwa na wadau wengi wa Elimu nchini. Yaani wanawakata wananchama wao 2% ya ada kila mwezi kwenye mishahara yao, jambo ambalo siyo sahihi hata kidogo. Maana hizo 2% hutofautiana kutoka mwanachama mmoja kwenda mwingine.

Badala yake wangetumia mfumo wa kuwakata kwa usawa kama walivyo anzisha hao wa elfu 5 kwa mwezi. Au unataka kuniambia na nyinyi TUGHE pia mnakatwa kwa mfumo huu wa 2% kwenye basic salaries zenu kila mwezi? Na kama na nyinyi pia mnafanyiwa hivyo, basi na mtakuwa mnaibiwa pia.
 
Kwanza nieleweke, sipingi wafanyakazi kuwa wananchama wa vyama vya wafanyakazi, na pia kulipa ada ya kuendeshea hivyo vyama (Trade Unions).

Hoja yangu iko sehemu moja tu. Vyama vya wafanyakazi vikusanye michango ya ada kwa wanachama wake kwa usawa! Yaani wanachama wote watozwe viwango sawa vya ada kila mwezi.

Kinachofanywa na CWT ndiyo kinacholalamikiwa na wadau wengi wa Elimu nchini. Yaani wanawakata wananchama wao 2% ya ada kila mwezi kwenye mishahara yao, jambo ambalo siyo sahihi hata kidogo. Maana hizo 2% hutofautiana kutoka mwanachama mmoja kwenda mwingine.

Badala yake wangetumia mfumo wa kuwakata kwa usawa kama walivyo anzisha hao wa elfu 5 kwa mwezi. Au unataka kuniambia na nyinyi TUGHE pia mnakatwa kwa mfumo huu wa 2% kwenye basic salaries zenu kila mwezi? Na kama na nyinyi pia mnafanyiwa hivyo, basi na mtakuwa mnaibiwa pia.
Hatukatwi flat rate mkuu,sijajua tu exactly asilimia..means kama ni TGHS C kuna amount yao inakatwa kama ni TGHS D kuna amount yao inakatwa na kuendelea.
 
Hatukatwi flat rate mkuu,sijajua tu exactly asilimia..means kama ni TGHS C kuna amount yao inakatwa kama ni TGHS D kuna amount yao inakatwa na kuendelea.
Basi na huko nako mnaibiwa. Maana kama wanachama wote wa vyama vya wafanyakazi wanatakiwa kupata haki sawa.
Sasa kwa nini kuwe na tofauti kwenye makato ya ada ya kuendeshea hivyo vyama?

Ifikie wakati wafanyakazi wote waupinge huu wizi. Ada ya uanachama wa chama chochote kile inatakiwa iwe flat rate kwa wanachama wake wote.
 
Vyama vyote vinakata ila isizidi Tsh 5,000 kwa mwezi kwa kila mwalimu.
Chukua deductions average of 4,000 each.
Then wastani wa walimu 290,000 Tanzania.
Zidisha kwa hiyo kiasi kwa miezi 12.
Jumla utakayo ipata ni bilioni kumi na tatu, milioni miatisa na ishirini (13,920,000,000/=).
Sasa swali lingeanzia hapa
 
Miaka kadhaa nyuma nakumbuka nilikua nakatwa 1/% (23,000) na chama cha NUMET kila mwezi, lakini wanachama walikua tunapata stahiki zetu mujarab kabisa.
 
Samahani mkuu,kuna chama ambacho hawakatwi? Maana hata huku TUGHE tunakatwa vile vile lakini naona mnawajadili walimu tu..
Kinachozungumzwa hapa si kukata bali kiasi Cha makato tena Kwa % km Bima ya afya. Labda nikuulize ni chama gani Cha wafanyakazi chenye makato makubwa zaidi ya CWT. Ebu lete hapa ya TUGHE. Wanacholalanikia ni makato makubwa na siyo kukatwa.
 
Kwa mtazamo wangu, Tanzania hakuna vyama vya wafanyakazi bali ni matawi tu ya vyama vya siasa. Km vipo basi havijui wajibu na malengo ya kuanzishwa kwake. Hivi vyama vinavyojinasibu eti ni vya wafanyakazi ni toothless dog na wanaoviendesha ni opportunistic seekers, nothing helpful is instilled in their hearts to help the workers.
 
Kinachozungumzwa hapa si kukata bali kiasi Cha makato tena Kwa % km Bima ya afya. Labda nikuulize ni chama gani Cha wafanyakazi chenye makato makubwa zaidi ya CWT. Ebu lete hapa ya TUGHE. Wanacholalanikia ni makato makubwa na siyo kukatwa.
Twende taratibu mkuu. Makato makubwa ni kiasi gani?
 
Njooni Chakuhawata, buku tano tu Kwa mwezi
Hicho chama naskia kinapigwa vita Kila Kona. Kuna Walimu sehemu mbalimbali wamekwaruzana na waajiri wao kwa kukikataa eti hakina ofisi sehemu walipo Walimu, (Hii ni hoja Mfu na ya kijinga kabisa, hakuna chama chochote kiwe Cha kisiasa au Cha wafanyakazi kiliwahi kuanzishwa na hapohapo kikawa na ofisi Kila mkoa, wilaya, Jimbo, kata au vitongoji). Hii sababu eti nayo wanapewa Walimu watu tunaoamini ni wasomi wabovevu na wao wamekuwa wanaikubali (either voluntarily or by force).

Inaonekana chama hiki cha CHAKUHAWATA kingekuwa msaada mkubwa kwa Walimu lakini inavyoonekana Viongozi wake either hawako makini au wamejaa uoga kukieneza na kusaidia Walimu wa zile sehemu zilizopata mkwamo hata kwa kuwapa msaada wa kisheria. Km wangefanikiwa hili nina uhakika CWT ingekufa kibudu.
 
Back
Top Bottom