Mwalimu Nyerere na Mkapa wamepumzika kwa amani, kwanini Magufuli haachwi apumzike kwa amani?

Mwalimu Nyerere na Mkapa wamepumzika kwa amani, kwanini Magufuli haachwi apumzike kwa amani?

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
16,427
Reaction score
22,418
Viongozi wetu wakuu waliokwisha kutangulia kama Mwalimu Nyerere na Mkapa wanaonekana “kupumzika kwa amani”, lakini yupo mmoja wao John Magufuli anayeonekana kutoachwa “apumzike kwa amani”. Je, Kuna nini nyuma ya jambo hili la kihistoria?

Kwa mtazamo wangu Nyerere na Mkapa (kwa kiwango kikubwa) waliwaachia watu uhuru wa kusema na kutoa maoni yao kupitia vyombo vya habari na mikusanyiko mbalimbali, ila uhuru huu ulikosekana wakati wa utawala wa Magufuli.

Kinachotokea sasa ni watu kutumia uhuru wao wa kujieleza ulioporwa enzi za Magufuli na hivyo kumfanya Magufuli kutopumzika hadi watu watakapomaliza kusema.
 
Viongozi wetu wakuu waliokwisha kutangulia kama Mwalimu Nyerere na Mkapa wanaonekana “kupumzika kwa amani”, lakini yupo mmoja wao John Magufuli anayeonekana kutoachwa “apumzike kwa amani”...
Good.

Magufuli alijifanya Mungu hakupenda kukosolewa pindi akiwa hai sasa nafasi kwa Watanzania wengi kumsema wakati huu akiwa kaburini.
 
Viongozi wetu wakuu waliokwisha kutangulia kama Mwalimu Nyerere na Mkapa wanaonekana “kupumzika kwa amani”, lakini yupo mmoja wao John Magufuli anayeonekana kutoachwa “apumzike kwa amani”...
Hao uliowataja hawana kundi la kuwatetea mitandaon maan, waliyofanya hayahitaj watetezi!! NB; Kama kuna mazuri kafanya mtu je kuna haja ya kuwepo kikundi cha kumtetea ama la!
 
Viongozi wetu wakuu waliokwisha kutangulia kama Mwalimu Nyerere na Mkapa wanaonekana “kupumzika kwa amani”, lakini yupo mmoja wao John Magufuli anayeonekana kutoachwa “apumzike kwa amani”...
Nyerere na Mkapa hawajapumzika kwa amani.

Kuna vitabu vitatu vimeandikwa na Profesa Shivji na wenzake kuhusu maisha ya Nyerere.

Wamemchambua sana.

Kila siku kwenye mijadala ya Watanzania Nyerere na Mkapa wanatajwa sana.

Hiyo amani unayoisema ni ipi?

Kuna mazungumzo mengi ya Magufuki kwa sababu Magufuki alikuwa mkora, na amekuwa rais wa kwanza kufariki akiwa rais, na amefariki miaka miwili tu iliyopita.
 
Siku ambayo familia za Azory Gwanda, Ben Saanane, wale waliokufa kwenye vile viroba pale CoCo beach, Ruvu basin zitapata closure ndipo huyu katili ataachwa apumzike, familia ya mwendazake wanajua kapumzika wapi.

Je, familia ya Ben Saanane tunaifikiria? Watoto wake wanakua bila baba yao, ni muhimu tuanze kufikiri hivyo tusiwe selfish maana hii sio familia yetu, Mr.Ben mauaji ya Mwembechai Masjid ipo siku kuna mtu au watu watawajibika, time ni mwamuzi wa haki.
 
Viongozi wetu wakuu waliokwisha kutangulia kama Mwalimu Nyerere na Mkapa wanaonekana “kupumzika kwa amani”, lakini yupo mmoja wao John Magufuli anayeonekana kutoachwa “apumzike kwa amani”....
Kutotaka kupangiwa/kushauriwa.

Kutumbua watu hadharani.

Kutukana watu hadharani.

Kuamini yeye ndo alikuwa na akili kubwa kuliko yeyote hapa Tanzania
 
Kila rais ataongelewa kwa mema na mabaya lakini Magufuli ametia fora kuongelewa kwa mabaya, sio bure kuna sababu.
Nimekupa sababu hapo juu, labda unataka zako ulizokuja nazo mfukoni mwako.

1. Ni rais w akwanza kufa madarakani, hili halijawahi kutokea.

2. Amekufa ndiyo kwanza miaka miwili imepita, kumbukumbu bado ziko fresh.

3. Alikuwa rais katili, mshenzi, mkora na mwenye siasa za ulaghai sana, kwa namna ambayo haijawahi kuonekana wazi hivi Tanzania.

Unataka sababu gani zaidi ya hizi?
 
Nimekupa sababu hapo juu, labda unataka zako ulizokuja nazo mfukoni mwako.

1. Ni rais w akwanza kufa madarakani, hili halijawahi kutokea.

2. Amekufa ndiyo kwanza miaka miwili imepita, kumbukumbu bado ziko fresh.

3. Alikuwa rais katili, mshenzi, mkora na mwenye siasa za ulaghai sana, kwa namna ambayo haijawahi kuonekana wazi hivi Tanzania.

Unataka sababu gani zaidi ya hizi?
Sasa andiko langu na point zako hasa point number 3 kuna ukinzani gani yakhe.
 
Sasa andiko langu na point zako hasa point number 3 kuna ukinzani gani yakhe.
Wewe umekuw bingwa wa kuandika kwa mafumbo na vitendawili kama kawaida ya Watanzania wengi.

Ndiyo maana Watanzania wengi wanaweza kuwa wanaongea kitu kimoja, lakini hawaelewani.

Kwa sababu wengi mnapenda kutumia mafumbo na vitendawili kama "si bure kuna jambo".

Jambo gani?

Ukisema "si bure kuna jambo" hujulikani umesimamia wapi. Unatuachia mtihani, kitendawili na fumbo hapo hapo.

Unasema si bure kuna jambo kivipi? Kwa kumaanisha Magufuli anaonewa? Kwa kusema kuna sababu ya msingi anasemwa?

Kauli yako inakuwa haiko hapa wala pale, hueleweki.

Mimi nimeweka wazi sababu, halafu wewe unaendelea kuleta mafumbo na vitendawili vya "si bure kuna jambo".

Lazima tusielewane hata kama tunazungumz akitu kimoja.
 
Wewe umekuw bingwa wa kuandika kwa mafumbo na vitendawili kama kawaida ya Watanzania wengi.

Ndiyo maana Watanzania wengi wanaweza kuwa wanaongea kitu kimoja, lakini hawaelewani.

Kwa sababu wengi mnapenda kutumia mafumbo na vitendawili kama "si bure kuna jambo".

Mimi nimeweka wazi sababu, halafu wewe unaendelea kuleta mafumbo na vitendawili vya "si bure kuna jambo".

Lazima tusielewane hata kama tunazungumz akitu kimoja.
Si bure kuna jambo, inakuwa fumbo kwako?
 
Viongozi wetu wakuu waliokwisha kutangulia kama Mwalimu Nyerere na Mkapa wanaonekana “kupumzika kwa amani”, lakini yupo mmoja wao John Magufuli anayeonekana kutoachwa “apumzike kwa amani”. Je, Kuna nini nyuma ya jambo hili la kihistoria?

Kwa mtazamo wangu Nyerere na Mkapa (kwa kiwango kikubwa) waliwaachia watu uhuru wa kusema na kutoa maoni yao kupitia vyombo vya habari na mikusanyiko mbalimbali, ila uhuru huu ulikosekana wakati wa utawala wa Magufuli.

Kinachotokea sasa ni watu kutumia uhuru wao wa kujieleza ulioporwa enzi za Magufuli na hivyo kumfanya Magufuli kutopumzika hadi watu watakapomaliza kusema.
Ushetani wake ndiyo unamfanya alaaniwe hata huko kuzimu aliko sasa
 
Back
Top Bottom