Mwalimu wa Kike apigwa na Mwalimu Mkuu

Mwalimu wa Kike apigwa na Mwalimu Mkuu

Kwa nini MD hana taarifa? Fateni ngazi. Kuna ofisi ya malalamiko pia , kila halmashauri ipo ofisi hyo.
 
Bila shaka huyo ticha atahamishwa sababu kisaikolojia ameshaathirika, hawezi fanya kazi hapo tena. Na kwa huyo hasira, apigwe miaka yake saba.
 
Hawa walimu nao wanashangaza kweli,sasa Mwamakula hapo msaada wake ni upi kwa jambo la kijinai? Huyo mwalimu akaripoti polisi halafu aende kwa Mkurugenzi ambaye ndo mwajiri wao. Walimu kwa kweli hamjielewi ndo maana huwa mnanyanyasika.
 
Aisee mimi ndo maana niliachaga ualimu, maana mtu anakudhalilisha kizembe kabisa as if huna haki za msingi.
Zamani nikiwa mwalimu nikiwa mwalimu headmaster alikuwa akinionea sana kila siku ananisingizia kuvaa nguo fupi yaan alitaka mimi niwe navaa vitenge vinavyoburuza chini.

Kha mimi abavyo sipendi manguo marefu nilikuwa najitahidi kuvaa nguo za kati chini ya magoti, siku nyingine ndefu kabisa lakini siku nikiivaa ya hiyo chini ya magoti naandikiwa barua.
Aliendelea kunichukia niajisikia vibaya nikaanza kuchukia ualimu.

Siku moja ndo naingia darasani kufundisha, nae akaingia darasani eti anataka kuona ufundishaji wangu, kha kwa nini anifanyie surprise bila kunipa taarifa?

Moyoni nikajisemea huyu fala nini?. Kaingia kakaa dawati za nyuma. Nikaongea na wanafunzi kidogo nikawapa kazi ya kufanya wasome kitabu fulani chp fulani tutakuja kudiscuss next time. Nikawaambia leo sijisikii vizuri nikatoka nikamuacha darasani. Alijisikia vibaya sana. Alivimba balaa.

Nikaona huu upuuzi nikaomba chuo kusoma fan nyingine nikaacha kazi, am happy nafanya ninachojisikia.
Hongera kwa kujikomboa kutoka utumwani. Headmaster anayo mamlaka ya kumsimamia ufundishaji wa mwalimu wake darasani?
 
Hao Ni wapenwapenz
Aisee mimi ndo maana niliachaga ualimu, maana mtu anakudhalilisha kizembe kabisa as if huna haki za msingi.
Zamani nikiwa mwalimu nikiwa mwalimu headmaster alikuwa akinionea sana kila siku ananisingizia kuvaa nguo fupi yaan alitaka mimi niwe navaa vitenge vinavyoburuza chini.

Kha mimi abavyo sipendi manguo marefu nilikuwa najitahidi kuvaa nguo za kati chini ya magoti, siku nyingine ndefu kabisa lakini siku nikiivaa ya hiyo chini ya magoti naandikiwa barua.
Aliendelea kunichukia niajisikia vibaya nikaanza kuchukia ualimu.

Siku moja ndo naingia darasani kufundisha, nae akaingia darasani eti anataka kuona ufundishaji wangu, kha kwa nini anifanyie surprise bila kunipa taarifa?

Moyoni nikajisemea huyu fala nini?. Kaingia kakaa dawati za nyuma. Nikaongea na wanafunzi kidogo nikawapa kazi ya kufanya wasome kitabu fulani chp fulani tutakuja kudiscuss next time. Nikawaambia leo sijisikii vizuri nikatoka nikamuacha darasani. Alijisikia vibaya sana. Alivimba balaa.

Nikaona huu upuuzi nikaomba chuo kusoma fan nyingine nikaacha kazi, am happy nafanya ninachojisikia.
Mkuu wa Shule Ni mkaguzi namba MOJA was Shule.

Taarifa ya Nini akupe?
Ili uandae Nini Cha ziada ambacho Kama asingekuja usingekiandaa?

Wewe ndo hujui ualimu ,

Nguo ndefu Ni SHERIA Siyo hiyari yako,

Halafu uvae nguo FUPI ili hao wanafunzi waone Tako LAKO au? Bora ulivyoandika ualimu.
 
Hao Ni wapenwapenzi,

Wala Siyo Mambo ya kazi,

Ama mwalimu wa kike alikuwa akimchunguza huyo mwalimu mkuu Kwenye KESI za mapenzi na hao watoto ,

Au mwalimu wa kike alimtusi mkuu wake akampandisha hasira akapigwa .

UCHUNGUZI ufanyike vzr
 
Sio effects za mahaba kweli hizi[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1732][emoji1732][emoji1732][emoji1732] mseleleko
 
MWALIMU WA KIKE APIGWA NA MWALIMU MKUU NA KUVUNJWA JINO MOROGORO VIJIJINI. WENZAKE WAMUOMBA ASKOFU MWAMAKULA ASAIDIE KUPAZA SAUTI ILI MAWAZIRI WENYE DHAMANA WASIKIE NA KUINGILIA KATI

Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Tunapenda kukujulisha tukio la kusikitisha lililomkuta mwalimu mwenzetu aitwaye Witness Makoti wa Shule ya Msingi Mkuyuni iliyopo Tarafa ya Mkuyuni katika Wilaya ya Morogoro Vijijini Mkoani Morogoro.

Siku ya Ijumaa, tarehe 15 Oktoba 2021 muda wa Saa 6 mchana, Mwalimu Witness Makoti ambaye ni mwanamke alikuwa akiongea na wanafunzi watatu darasani. Wakati akiongea na watoto wake, ghafla alishambuliwa na kuanza kupigwa na Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo ambaye ni mwanaume aitwaye Mussa Hasira. Alipigwa sana lakini aliokolewa na mwalimu mmoja.

Baada ya kushambuliwa na kupigwa, Witness alikwenda kuripoti katika Kituo cha Polisi cha Mkuyuni na kupewa PF3 ya kwenda Zahanati ya Mkuyuni na kupata matibabu ya awali. Baada ya hali kuendelea kuwa mbaya, leo Jumapili alikwenda Hospitali ya Nunge kwa matibabu zaidi ambapo imegundulika kuwa Witness ana vidonda mdomoni na pia amevunjwa jino.

Hali yake ya kiafya mpaka sasa siyo nzuri sana na inazidi sana na ameleza pia kuwa pressure imempanda. Hadi muda huu, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Vijijini na Mkuu wa Wilaya hawana taarifa.

Mwalimu Witness Makoti anahofia usalama wa maisha yake kwani ameelezwa kuwa Mwalimu Mkuu alimfuata mwalimu aliyemgombelezea Witness akaanza kumlaumu na kusema kuwa angelimuacha bila kumgombelezea ili amuue kabisa.

Mwalimu Witness Makoti ameomba asaidiwe katika kulipazia sauti jambo hili aweze kupata msaada kusudi haki iweze kutendeka lakini pia ili kuokoa maisha yake.

Tunaambatanisha picha ya Mwalimu Witness Makoti hapa chini.

Tunakushuru sana Baba Askofu Mwamakula kwa kutupokea na tunaamini kuwa kupitia sauti yako, Witness atapata msaada anaouhitaji.

Mbona hapo Hospitali ya Bunge Ni karibu kabisa na ofisi za CWT kwanini asiende yspo? Pia ungeweka picha ya Mwalimu aliyempiga
 
Ila walimu wameonesha hadhira kuwa weledi wao ni mdogo.Hawakupaswa kuripoti jambo hilo kwa Askofu Mwamakula bali walitakiwa waripoti ktk taasisi za umma kama Ofisi ya Mkurugenzi wa hiyo Halmashauri, Chama cha walimu Tanzania nk.
 
Natamani nikasomee uhakimu na kuhitimu muda huu huu halafu nifanye mpango ili nipangiwe kesi ya huyu mbabe Mwalimu Mkuu
 
Mussa Hasira akapimwe akili

Habari hii nayo ya upande mmoja sijui waandishi wa aina gani hawa!?

Au kampeni meneja wa mwamakula🤣🤣🤣
 
Sio effects za mahaba kweli hizi[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1732][emoji1732][emoji1732][emoji1732] mseleleko
Mambo ya wivu wa mapenzi yamemsababishia mwalimu Hasira kupata hasira.
 
Yaani hapo mwakee hasira bini jaziba [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Hapo mwalimu Hasira utakuta hasira zimeongeza baada ya kutuma na yakutolea halafu akakukumbuka pia alikatwa na tozo daaaahhhh inauma sana kwa kweli.
 
Wameshariport polisi mkuu,, nadhani polisi na huyo mwalimu mkuu wana lao moja.
Mm ninavyojua ni kwamba Polisi wanazo taratibu za kushughulika na Tatizo kama hilo na sio kukurupuka kwani mpaka hapo tayari anayo makosa matatu:- 1. Kujeruhi 2. Kudhalilisha 3. Uvunjifu wa Amani mahali pa kazi - mengine yatajitokeza huko mbele ya safari.(Mkurugenzi (DED), anatakiwa awe ameshamsimamisha Kazi)
Inasikitisha pia mtoa uzi hajatuambia Mwl. Mkuu kwa sasa yuko wapi. Je, yupo kashikiliwa/kazuiliwa kituo cha Polisi au imekaaje ? Kwa ujumla mwl. HASIRA alichokifanya ni uovu na Amejichukulia Sheria mkononi mwake. Hii sio sawa. Kwa hali hiyo inatakiwa Sheria ichukue mkondo wake dhidi ya mwl. Hasira na Haki ionekane kutendeka i.e. Anastahili apumzishwe pale Mahabusu (Polisi) wakati taratibu za kumfikisha mahakamani zinaendelea.
 
Back
Top Bottom