Mwalimu wa Kike apigwa na Mwalimu Mkuu

Mwalimu wa Kike apigwa na Mwalimu Mkuu

Hapo mwalimu Hasira utakuta hasira zimeongeza baada ya kutuma na yakutolea halafu akakukumbuka pia alikatwa na tozo daaaahhhh inauma sana kwa kweli.
Kaamua kuondoka na jino la bidada
 
Kakataa kutoa kwa mwalimu mkuu a test mitambo kuona kama chanjo ya korona imefanya kazi au la!
 
Hadi muda huu, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Vijijini na Mkuu wa Wilaya hawana taarifa.



Mwalimu Witness Makoti ameomba asaidiwe katika kulipazia sauti jambo hili aweze kupata msaada kusudi haki iweze kutendeka lakini pia ili kuokoa maisha yake.

Mtoa mada unaelewa fika kwamba wahusika hawana taarifa juu ya tukio. Aliyefikwa na mkasa anaomba asaidiwe. Wewe unaelekeza taarifa yako kwa Askofu ambaye wala hayuko kwenye wilaya au mkoa wa tukio. Si hivyo tu, hata huo ujumbe unaouelekeza kwa Askofu unauandika kwa barua ya wazi hapa kwenye jamvi la JF. Sijui kama una uhakika kama mlengwa wa ujumbe huu ni mwanachama wa JF. Hata kama ni mwanachama, huenda zikapita siku kabla hajatua hapa jamvini. Hivyo atakuwa ameukosa ujumbe huo.

Hoja yangu ni kwamba malalamiko yanasambazwa kwenye vyombo vya habari badala ya kuwafikishia wahusika. Mtu analalamika kwamba ajali imetokea saa nzima iliyopita lakini mpaka sasa polisi wa usalama barabarani hawajafika. Au tukio la ujambazi limefanyika mahali fulani na vyombo vya usalama havijafika kwenye tukio.

Lawama kama hizi si sahihi. Tusikimbilie kulalamika kwenye vyombo vya habari kabla ya kutoa taarifa kwenye vyombo vinavyohusika. Hapo ndipo utakuwa sahihi kulalamika kwamba taarifa imefikishwa kwa wahusika saa kadhaa zilizopita lakini bado hawajaja.
 
Waende tume ya utumishi wa walimu,mamlaka yao ya utatuzi wa nigogoro wanaijua,kwenda kwa askofu ilipaswa kuwa baada ya ofisi za serikali kumaliza mgogoro,pia kumleta huku JF sio sawa
Mkuu Sheikh23; Hilo halijaharibu kitu. Amefanya vyema ili na ss huku maporini tuweze kuwa tumelijua na kama yupo mwengine (Mwl) anayefikiri au amezoea kufanya ujinga kama huyo Hasira awe amepata Fundisho ajihadhari na kujiepusha na ukorofi kama huo.😠👿
 
Huyu madam beautiful,kuna kitu hapa
Waache wapigwe tu mkuu, mzee Pinda alisema wapigwe tu, na mimi nakazia WAPIGWE TU, maana hawa ndio wanaolindaga kura za ccm na kuiba za upinzani
 
MWALIMU WA KIKE APIGWA NA MWALIMU MKUU NA KUVUNJWA JINO MOROGORO VIJIJINI. WENZAKE WAMUOMBA ASKOFU MWAMAKULA ASAIDIE KUPAZA SAUTI ILI MAWAZIRI WENYE DHAMANA WASIKIE NA KUINGILIA KATI

Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Tunapenda kukujulisha tukio la kusikitisha lililomkuta mwalimu mwenzetu aitwaye Witness Makoti wa Shule ya Msingi Mkuyuni iliyopo Tarafa ya Mkuyuni katika Wilaya ya Morogoro Vijijini Mkoani Morogoro.

Siku ya Ijumaa, tarehe 15 Oktoba 2021 muda wa Saa 6 mchana, Mwalimu Witness Makoti ambaye ni mwanamke alikuwa akiongea na wanafunzi watatu darasani. Wakati akiongea na watoto wake, ghafla alishambuliwa na kuanza kupigwa na Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo ambaye ni mwanaume aitwaye Mussa Hasira. Alipigwa sana lakini aliokolewa na mwalimu mmoja.

Baada ya kushambuliwa na kupigwa, Witness alikwenda kuripoti katika Kituo cha Polisi cha Mkuyuni na kupewa PF3 ya kwenda Zahanati ya Mkuyuni na kupata matibabu ya awali. Baada ya hali kuendelea kuwa mbaya, leo Jumapili alikwenda Hospitali ya Nunge kwa matibabu zaidi ambapo imegundulika kuwa Witness ana vidonda mdomoni na pia amevunjwa jino.

Hali yake ya kiafya mpaka sasa siyo nzuri sana na inazidi sana na ameleza pia kuwa pressure imempanda. Hadi muda huu, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Vijijini na Mkuu wa Wilaya hawana taarifa.

Mwalimu Witness Makoti anahofia usalama wa maisha yake kwani ameelezwa kuwa Mwalimu Mkuu alimfuata mwalimu aliyemgombelezea Witness akaanza kumlaumu na kusema kuwa angelimuacha bila kumgombelezea ili amuue kabisa.

Mwalimu Witness Makoti ameomba asaidiwe katika kulipazia sauti jambo hili aweze kupata msaada kusudi haki iweze kutendeka lakini pia ili kuokoa maisha yake.

Tunaambatanisha picha ya Mwalimu Witness Makoti hapa chini.

Tunakushuru sana Baba Askofu Mwamakula kwa kutupokea na tunaamini kuwa kupitia sauti yako, Witness atapata msaada anaouhitaji.


Kwani mheshimiwa mbunge Tale Tale wa pande za huko anasema je 😁😁?
 
ni pisi kali....
IMG-20211018-WA0000.jpg
 
uonevu wa kijinsia mimi mara nyingi nashangaa kwanini mwanaume rijali umpige mwanamke na unajua hawezi kujitetea, piganeni na wanaume wenzenu au naukuta tabia chafu sana hii na ya kukemea ni unyanyasaji wa jinsia,sheria ifate mkondo wake awajibishwe.
 
hawezi kupigwa pasipo sababu, huyo mwalimu siyo kichaaa nadhan ingekuwa busara wangeweka na sababu au mambo ya mahusiano, usikte alikua analiwa darasani
 
uonevu wa kijinsia mimi mara nyingi nashangaa kwanini mwanaume rijali umpige mwanamke na unajua hawezi kujitetea, piganeni na wanaume wenzenu au naukuta tabia chafu sana hii na ya kukemea ni unyanyasaji wa jinsia,sheria ifate mkondo wake awajibishwe.
mwanamke gani hawz kujitetea?? hawa tunaolewa nao kila siku?? wnye midomo kama chuchunge??
 
Hili halihitaji kusikiliza, hakuna sheria inayotoa uhalali wa kipigo kwa mtu mwingine.

Hili halihitaji kusikiliza, hakuna sheria inayotoa uhalali wa kipigo kwa mtu mwingine.
Nimemwelewa rasjeff kapita kwamba wahusika wa pande zote mbili i.e. Mlalamikaji (Mwl. Witness aliyepigwa/jeruhiwa) na Mlalamikiwa (mwl. Mkuu aliyejeruhi) katika shauri hili wapate fursa ya kusikilizwa = wajieleze mbele ya sheria. Ni kweli Hakuna Sheria inayotoa Uhalali wa kipigo kwa mtu mwingine Lakini mkuu Renegade ujue kwamba inawezekana mtu akapigwa kihalali kutokana na matendo au kauli zake mwenyewe. Mathalani mtu anakutukana, anakufanyia mizengwe na unamuonya x 2 au 3 lakini hakusikii na anafikia hatua ya kukugusa/ kukushika/kukuundia genge la mizengwe ; Je, hutapandwa na hasira ya ghafla hususan unapomkuta Red hand? Ndo maana huyo rasjeff kasema wasikilizwe ili ibainike ni nini hasa kilichojiri/kisababishi.
 
Pole kwa mwalimu Witness

Kumpiga mwenzio haikubaliki hata awe mke wa ndoa, vyovyote vile itakavyokuwa.

Lakini tuelezeni ikiwa mwalimu mkuu sio kichaa kwanini aliamua kumpiga Witness na sio kumpiga mwalimu mwingine?
Hahahaa mwalimu mwingine ndiyo Huyo Witness mkuu.
 
Back
Top Bottom