Mwalimu wa Madrasa apandishwa Kizimbani kwa tuhuma za kuwachapa fimbo (Ukatili) wanafunzi wa madrasa

Mwalimu wa Madrasa apandishwa Kizimbani kwa tuhuma za kuwachapa fimbo (Ukatili) wanafunzi wa madrasa

Mwafrika mbele ya imani za kigeni amekuwa mtu wa hovyo sana. Imani gani inaambatana na ukatili wa namna hii kwa watoto wadogo. Huyo usitazi anatakiwa kufugwa ili iwe fundisho kwa wengine ambao hata saikolojia ya kukaa na watoto hawaijuwi zaidi kutumia Jazba. Wazazi pia wanaopeleka watoto maeneo hayo waongeze umakani matukio ya aina hii ili yadhibitiwe.
Mnafiki! Unapinga adhabu ya viboko muda huo huo unataka kijana akafungwe unachimba chimo hili ili ufukie shimo lile
 
Kama watu ni rahisi kufundishika adhabu za kunyonga na viboko kwenye sheria zetu zimetungiwa nani?
Binadamu anafundishika,ingawa sio wote, na sheria zimetungwa kwa wale ambao wanavunja sheria
Mimi sijawahi kuwa na kosa lolote la kupelekwa mahakamani au hata polisi
Lakini hainifanyi kuwa siwezi kutenda kosa
Fimbo kuchapwa kila siku je huyo mtoto anabadilika? na je kama habadiliki utaendelea kupiga?
Nafikiri kuna wengine hawajali mafundisho bila fimbo

Ukipata mda angalia dog whisperer au dog behaving very bad
Utaona hao watu wanavyowabadili tabia za mbwa wakati wenye mbwa wameshindwa baada ya miaka
Ni mfano tu huo
Ila kwa watoto watukutu pia anaitwa Annie The Nanny akiwasaidia wazazi
Lakini pia kila mmoja anaona yuko sawa kwa anachofanya

Mtoto anadokoa nyama unamchoma mikono je una akili hapo?
 
Binadamu anafundishika,ingawa sio wote, na sheria zimetungwa kwa wale ambao wanavunja sheria
Mimi sijawahi kuwa na kosa lolote la kupelekwa mahakamani au hata polisi
Lakini hainifanyi kuwa siwezi kutenda kosa
Fimbo kuchapwa kila siku je huyo mtoto anabadilika? na je kama habadiliki utaendelea kupiga?
Nafikiri kuna wengine hawajali mafundisho bila fimbo

Ukipata mda angalia dog whisperer au dog behaving very bad
Utaona hao watu wanavyowabadili tabia za mbwa wakati wenye mbwa wameshindwa baada ya miaka
Ni mfano tu huo
Ila kwa watoto watukutu pia anaitwa Annie The Nanny akiwasaidia wazazi
Lakini pia kila mmoja anaona yuko sawa kwa anachofanya

Mtoto anadokoa nyama unamchoma mikono je una akili hapo?
Embu taja adhabu mbadala ambazo unaweza ukatoa kwa mtoto mtukutu
 
Embu taja adhabu mbadala ambazo unaweza ukatoa kwa mtoto mtukutu
Mkuu nimeona watoto watukutu wakipigwa sana lakini hawabadiliki, badala yake wanakuwa Nunda
Mimi sio muumini wa kufundisha kwa kupiga.
Sasa unaponiuliza hilo swali nimeishalijibu kwenye hoja iliyopita
Kuwa kila mmoja anamfundisha kwa njia anazoona yeye.
Hata wewe kama unaona ni sawa kupiga siwezi kukupangia
Mkuu kuna binadamu wabaya sana wanapopiga watoto wao au hujaona?

Kuna siku nimekaa sehemu, akapita mama mmoja akiwa na mtoto mdogo wa miaka miwili hivi
Mtoto kaamua kukaa chini kwa sababu ametoka kijijini na mama kachoka kumbeba
Akawa anampiga ili atembee.(Ni kosa)na sio suluhu hilo
Mama kachoka kumbeba mtoto, nikamuuliza umetoka nae wapi na unanda wapi
Akasema kijijini nampeleka hospital na nimechoka
Nikamuita na kuwapa maji na kuwakodishia pikipiki waende hospital

Nikamwambia najua umechoka kumbeba na yeye kachoka kutembea lakini mngepumzika kwanza
 
Akiwa Mwislamu ndiyo inakuwaje?

Ninyi mambo yenu ya kukataa hicho mnachokiita elimu dunia yanawafanya mwonekane nanii
Katika uislam hakuna elimu dunia wala elimu kuzimu, pili kwa hii tz kuna maprofesa wangapi ni waislam na wanaijua dini vizuri? Kuna shule ngapi za kiislam? Mnakaa mnazusha vitu kisha chuki tu.
 
Katili mwingine huyu hapa. Kwanza unaelewa neno mtoto? Yaani watoto ndiyo mmeona ni wa kuchapwa tu? Nyinyi ndiyo huwafanyia watoto ukatili.

Mtoto kama kafanya makosa, ongea naye, fimbo haijawahi kuwa suluhisho, ndiyo maana tuna watoto watukutu, watoto wa mitaani waliokimbia vipigo majumbani na mateso. Hata hivyo mtoto wangu kafanya mafundisho, hakuwahi nilalamikia kuchwapwa.
Binafsi nimesoma madrsa na nimechapwa na sijawahi lalamika nyumbani kwa mzazi wangu, adhabu zitoke lakini kwa kiasi zinasaidia kuchangamsha mtoto, kwenye hiyo video ustaadh kazidisha adhabu.
 
Mimi sitaki kushutumu ni watoto wa dini Gani hawana maadili Kwakuwa sijafanya utafiti wa Hilo na kujua sababu ni zipi ?

Ila Kwa mtazamo wangu kuhusu hiyo clip sijaona kosa la ustadhi kutoa adhabu inategemea na kosa walilofanya BTW sidhani kama wazazi walikuwa hawajui Hilo au watakuwa wao ndo wamewashitaki

Cha mwisho Mimi ni mkristo tena KKKT usijefikiri kutakuwa na ligi ya kidini
Mimi ni muislam na nimeona hiyo video, ustaadh katoa adhabu kubwa kulinganisha na umri wa watoto, hao wa kike ilibidi fimbo moja tu.
 
Back
Top Bottom