HABARI: Mwalimu wa madrassa Abuubakar Mussa Hamisi (19) na mwendesha bodaboda Muhaji Mohamed Rajab 25 wote wakazi wa Dule B lililopo eneo la Bumbuli, wilayani Lushoto, wamepandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wilayani Lushoto kwa tuhuma za kuwalawiti wanafunzi wawili wa kiume na mmoja wa kike.
Imedaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka, Wakili wa Serikali Sylivia Bitanto kuwa, mnamo mwezi Oktoba mwaka huu, Hamisi katika eneo la Dule B, alimwingilia kinyume cha maumbile mwanafunzi wake wa kiume mwenye umri wa miaka 9.
Aidha, mwendesha mashtaka huyo Sylivia Bitanto ameendelea kudai kuwa, katika eneo hilo hilo la Dule B Bumbuli, dereva wa bodaboda Muhaji Mohmed Rajab anatuhumiwa kumbaka mwanafunzi wa kike mwenye umri wa mika 11 katika eneo hilo la Dule B lililopo Halmashauri ya Bumbuli.
Hata hivyo, Mwendesha Mashtaka huyo amezidi kueleza kuwa, mbali na shauri hilo, pia mtuhumiwa Muhaji Mohmed Rajab alimlawiti mwanafunzi wa kiume mwenye umri wa miaka 7 katika tukio lililotokea mwanzoni mwa mwezi huu katika eneo la Dule B lililopo wilayani Lushoto.
Watuhumiwa hao waliofikishwa katika mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Wilaya ya Lushoto Kavumo Mndimi aliahirisha shauri hilo hadi Disemba 5, mwaka huu litakapotajwa tena huku watuhumiwa wakiendelea kusota rumande ndani ya Ngome Kuu iliyopo wilayani Lushoto.
Source: ITV Digital
Imedaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka, Wakili wa Serikali Sylivia Bitanto kuwa, mnamo mwezi Oktoba mwaka huu, Hamisi katika eneo la Dule B, alimwingilia kinyume cha maumbile mwanafunzi wake wa kiume mwenye umri wa miaka 9.
Aidha, mwendesha mashtaka huyo Sylivia Bitanto ameendelea kudai kuwa, katika eneo hilo hilo la Dule B Bumbuli, dereva wa bodaboda Muhaji Mohmed Rajab anatuhumiwa kumbaka mwanafunzi wa kike mwenye umri wa mika 11 katika eneo hilo la Dule B lililopo Halmashauri ya Bumbuli.
Hata hivyo, Mwendesha Mashtaka huyo amezidi kueleza kuwa, mbali na shauri hilo, pia mtuhumiwa Muhaji Mohmed Rajab alimlawiti mwanafunzi wa kiume mwenye umri wa miaka 7 katika tukio lililotokea mwanzoni mwa mwezi huu katika eneo la Dule B lililopo wilayani Lushoto.
Watuhumiwa hao waliofikishwa katika mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Wilaya ya Lushoto Kavumo Mndimi aliahirisha shauri hilo hadi Disemba 5, mwaka huu litakapotajwa tena huku watuhumiwa wakiendelea kusota rumande ndani ya Ngome Kuu iliyopo wilayani Lushoto.
Source: ITV Digital