Mwamnyeto kuzikosa mechi muhimu sana za Al-Merreikh ni fundisho kwake na wazawa

Mwamnyeto kuzikosa mechi muhimu sana za Al-Merreikh ni fundisho kwake na wazawa

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Sisi mashabiki hatujui ukubwa wa tatizo lilisababisha Kapteni wa Yanga, Mwamnyeto kushindwa kwenda Rwanda kwenye mechi muhimu saaaaana kwa timu ya Yanga dhidi ya Al-Merreikh. Kama mchezaji kiongozi wa timu mechi hii haikuwa ya kukosa kwasababu hafifu hafifu tu na dhaifu.

Vitu pekee ambavyo vingeweza kusababisha kapteni wa timu kuikosa mechi ya muhimu kama ile ingekuwa labda kuumwa sana kwa mchezaji, mazishi ya mzazi, mke, au mtoto wako aliyefariki wakati wa maandalizi ya mechi na mpango wa kocha kwenye mechi husika, zaidi ya hapo mchezaji professional hatakiwi kukosa mechi muhimu kama ile kwasababu ndogondogo na fupifupi (trivial). Ni heri asicheze uwanjani lakini awepo kwenye benchi kwaajili ya kuwatia hamasa wachezaji wenzake.

Kukosekana kwa Kapteni wa timu kwenye mechi kunaongeza morali kwa timu pinzani na kupunguza morali kwa wachezaji wa timu yake, benchi la ufundi, uongozi na hata mashabiki wa timu, sio jambo ambalo kocha makini atalifurahia hata kidogo. Anaweza kukuchukia milele kwakuwa huaminiki (not reliable and dependable).

Hii inawezekana ni sababu kwa kocha Gamondi kutomjumuisha kwenye kikosi cha kilichocheza marudiano na Al-Merreikh pale chamazi. Wachezaji wazawa lazima muwe real professionals.
 
Mchezaji wa mpira siyo mashine kama roboti au trekta au tinganga.
Ana hisia, anachoka, anaumwa, ana sumbuliwa na sababu za kijamii n.k.

Kama hauna taarifa sahihi nini kimemsibu bora kukaa kimya. Msiwe mabingwa wa kulaumu.
 
Hivi unajua sababu ya yeye kutokwenda Rwanda? Mbona Klabu walitoa taarifa rasmi kuwa anauguliwa na baba yake?
Wewe unaweza kumuacha baba yako mahututi ukaenda kuitumikia klabu?
Huo ndio uswahili wenyewe kwa wachezaji wazawa. Baba akiwa mgonjwa sehemu yake sahihi ni hospitali na wajibu wa mchezaji kama Mwamnyeto ni kumkatia bima ya matibabu wazazi wake. Kwahiyo yeye alikwenda kufanya nini kwa baba yake? Je, kama mwamnyeto angekuwa anacheza mpira timu za Ulaya angerudi Tanga kumjulia hali baba yake mgonjwa kama alivyofanya? Akumbuke kuwa kocha wa Yanga sio Charles Mkwasa ambae anazifahamu mila na desturi zetu.
 
Huo ndio uswahili wenyewe kwa wachezaji wazawa. Baba akiwa mgonjwa sehemu yake sahihi ni hospitali na wajibu wa mchezaji kama Mwamnyeto ni kumkatia bima ya matibabu wazazi wake. Kwahiyo yeye alikwenda kufanya nini kwa baba yake? Je, kama mwamnyeto angekuwa anacheza mpira timu za Ulaya angerudi Tanga kumjulia hali baba yake mgonjwa kama alivyofanya? Akumbuke kuwa kocha wa Yanga sio Charles Mkwasa ambae anazifahamu mila na desturi zetu.
Badilisha jina jiite kavulana,
Ukikua utaelewa
 
Alikuwa anamuuguza Baba yake Mzazi. Taarifa ilitolewa kabla ya safari ya kwenda Kigali Rwanda
yeye ni daktari? alisaidia nini baba yake kupona? Kocha ni mzungu, na ana mipango yake. Klabu haiwezi kukosa kwenda makundi baada ya miaka 25 ya kusubiri kwasababu eti wewe baba yako ni mgonjwa tu hajafa.
 
Sisi mashabiki hatujui ukubwa wa tatizo lilisababisha Kapteni wa Yanga, Mwamnyeto kushindwa kwenda Rwanda kwenye mechi muhimu saaaaana kwa timu ya Yanga dhidi ya Al-Merreikh. Kama mchezaji kiongozi wa timu mechi hii haikuwa ya kukosa kwasababu hafifu hafifu tu na dhaifu. Vitu pekee ambavyo vingeweza kusababisha kapteni wa timu kuikosa mechi ya muhimu kama ile ingekuwa labda kuumwa sana kwa mchezaji, mazishi ya mzazi, mke, au mtoto wako aliyefariki wakati wa maandalizi ya mechi na mpango wa kocha kwenye mechi husika, zaidi ya hapo mchezaji professional hatakiwi kukosa mechi muhimu kama ile kwasababu ndogondogo na fupifupi (trivial). Ni heri asicheze uwanjani lakini awepo kwenye benchi kwaajili ya kuwatia hamasa wachezaji wenzake.

Kukosekana kwa Kapteni wa timu kwenye mechi kunaongeza morali kwa timu pinzani na kupunguza morali kwa wachezaji wa timu yake, benchi la ufundi, uongozi na hata mashabiki wa timu, sio jambo ambalo kocha makini atalifurahia hata kidogo. Anaweza kukuchukia milele kwakuwa huaminiki (not reliable and dependable).

Hii inawezekana ni sababu kwa kocha Gamondi kutomjumuisha kwenye kikosi cha kilichocheza marudiano na Al-Merreikh pale chamazi. Wachezaji wazawa lazima muwe real professionals.
Kama haujui kilichomtokea, kwanini una conclude?
 
yeye ni daktari? alisaidia nini baba yake kupona? Kocha ni mzungu, na ana mipango yake. Klabu haiwezi kukosa kwenda makundi baada ya miaka 25 ya kusubiri kwasababu eti wewe baba yako ni mgonjwa tu hajafa.
Aisee !uto kama uto,! We unajua Standing Orders za Watumishi ya Yañga.? Mbona mnapenda kujitoa stress bila sababu! Uto wenyewe wametoa taaridmfa wewe unalalama! Khaaa!
 
Huo ndio uswahili wenyewe kwa wachezaji wazawa. Baba akiwa mgonjwa sehemu yake sahihi ni hospitali na wajibu wa mchezaji kama Mwamnyeto ni kumkatia bima ya matibabu wazazi wake. Kwahiyo yeye alikwenda kufanya nini kwa baba yake? Je, kama mwamnyeto angekuwa anacheza mpira timu za Ulaya angerudi Tanga kumjulia hali baba yake mgonjwa kama alivyofanya? Akumbuke kuwa kocha wa Yanga sio Charles Mkwasa ambae anazifahamu mila na desturi zetu.
Unaujua ukubwa wa familia yake? Unajua anasumbuliwa na maradhi gani? Bima ya afya inakupeleka na kukupangia foleni kwa dakitari?
Hapa naona unazungumza kama mlivyoishi huko ulaya ambako baba yako akifariki unakwenda kumzika tu kwa muda uliopangiwa na weilazi(walizi wa kukodiwa) na ukimaliza unarudi ofisini.
 
Umeonyesha Wazi kichwani ulivyo mtupu.
Kaka uswahili ndio kisiki kikubwa cha wachezaji wazawa kubakia hapo walipo. ni bahati nzuri Yanga ina kikozi kipana, uzembe huu wa mwamnyeto umetoa nafasi kwa mchezaji mwingine kuaminiwa na kocha. Wewe unadhani Mohamed Husein Zimbwe jr. wa Simba yeye hauguliwi, hafiwi, haumii? Bro, malengo ya mwajili yanakaa mbele ya malengo ya mwajiliwa. Kama baba anaumwa na yuko hospitali tayari nitakwenda kumjulia hali nikirudi Rwanda kwenye maokoto kwanza. Kama baba yange angekuwa amefariki ingekuwa jambo lingine kabisa, no one angeweza kusikitika wala ku-mind. Gamondi aliendelea kumuweka nje ili amalizane na uswahili wake kwanza. Nimemsikia Gamondi akisema angetaka asajili wachezaji wengine kwaajili ya makundi na hatua nyingine, huenda kitendo cha mwamnyeto kilimshtua kwelikweli,
 
Unaujua ukubwa wa familia yake? Unajua anasumbuliwa na maradhi gani? Bima ya afya inakupeleka na kukupangia foleni kwa dakitari?
Hapa naona unazungumza kama mlivyoishi huko ulaya ambako baba yako akifariki unakwenda kumzika tu kwa muda uliopangiwa na weilazi(walizi wa kukodiwa) na ukimaliza unarudi ofisini.
Yaani uko kwenye first eleven ya kocha mzungu kwenye mechi ambayo inashikilia hatima ya timu kufuzu na hatima yake kusalia kuwa kocha wa timu halafu wewe unadai unakwenda kupanga foleni ya baba hospitalini anaumwa tezi dume (cold case).
 
Alikuwa anamuuguza Baba yake Mzazi. Taarifa ilitolewa kabla ya safari ya kwenda Kigali Rwanda
yeye ni daktari? alisaidia nini baba yake kupona? Kocha ni mzungu, na ana mipango yake. Klabu haiwezi kukosa kwenda makundi baada ya miaka 25 ya kusubiri kwasababu eti wewe baba yako ni mgonjwa tu hajafa.

UKo kwenye mipango ya kocha na first 11 ya kocha kwenye mechi ambayo inashikilia hatima ya kocha kubaki kwenye timu na hatima ya timu kutinga makundi baada ya miaka 25 halafu mchezaji muhimu (kapteni) anasema hawezi kwenda kucheza kwakuwa baba yake hana mtu wa kumkalia foleni ya kwenda kumuona dk wake wa tezi dume. Atakuchukia milele.
 
yeye ni daktari? alisaidia nini baba yake kupona? Kocha ni mzungu, na ana mipango yake. Klabu haiwezi kukosa kwenda makundi baada ya miaka 25 ya kusubiri kwasababu eti wewe baba yako ni mgonjwa tu hajafa.

UKo kwenye mipango ya kocha na first 11 ya kocha kwenye mechi ambayo inashikilia hatima ya kocha kubaki kwenye timu na hatima ya timu kutinga makundi baada ya miaka 25 halafu mchezaji muhimu (kapteni) anasema hawezi kwenda kucheza kwakuwa baba yake hana mtu wa kumkalia foleni ya kwenda kumuona dk wake wa tezi dume. Atakuchukia milele.
Family over everything, hata hao wazungu linapo kuja swala la familia wapo tayari kuacha kazi kama family yake haipo stable
 
Family over everything, hata hao wazungu linapo kuja swala la familia wapo tayari kuacha kazi kama family yake haipo stable
Familia inayomsumbua mzungu ni ile ya mke/mume na mtoto wake, baba na mama kuna watu wengi kama mkewe, kaka, dada, wajukuu, shangazi wanaweza kwendaga huko wakati mimi ninakamilisha taratibu nyingine. Sanasana naweza kuwatumia fedha ya ambulance na matumizi/matibabu wakati mimi nikimalizia shughuli muhimu, yaani nitaungana na nyinyi baadae. hata wanafunzi vyuoni na mashuleni wakati wa mitihani huwa wanafichwa kuambiwa matukio mabaya yanayotokea nyumbani kama ugonjwa au kifo cha mwanafamilia hadi atakapomaliza mitihini yake yote, sembuse mechi ya kufuzu makundi na wewe ndiye kapteni wa timu. Uswahili tu bhana.
 
Yaani uko kwenye first eleven ya kocha mzungu kwenye mechi ambayo inashikilia hatima ya timu kufuzu na hatima yake kusalia kuwa kocha wa timu halafu wewe unadai unakwenda kupanga foleni ya baba hospitalini anaumwa tezi dume (cold case).

Yaani uko kwenye first eleven ya kocha mzungu kwenye mechi ambayo inashikilia hatima ya timu kufuzu na hatima yake kusalia kuwa kocha wa timu halafu wewe unadai unakwenda kupanga foleni ya baba hospitalini anaumwa tezi dume (cold case).
"Hapa naona unazungumza kama mlivyoishi huko ulaya ambako baba yako akifariki unakwenda kumzika tu kwa muda uliopangiwa na weilazi(walizi wa kukodiwa)" huko kwao ukilazwa ndugu zako wanakuletea maua na kadi, mambo mengine yote hata utakachopenda kula ni juu ya hospitali, sisi hapa labda waliokuja kumtazama jirani yako kitanda cha pili wakuonee huruma wakakununulie chips kachumbali na pilipili kwa mbali! Wanaofanya kazi kwenye ofisi za wazungu ukifiwa unapewa ruhusa ukashinde nyumbani japo hauwezi kumfufua, wao kwao unakuwa kazini mpaka wakati wa kuzika kulingana na wazikaji walivyokufahamisha muda.
 
Back
Top Bottom