Mwana FA amkana Baba yake mzazi

Mwana FA amkana Baba yake mzazi

Ila tukumbuke mzazi ni mzazi tu...mimi kwangu haijalishi nn kilitokea huko nyuma lkn wazazi wangu niliwapa upendo sawa. Ingawa kuna miaka dingi alikuwa na mchepuko akamzingua sana maza lkn mwisho wa siku walielewana na maisha yakaendelea mpk alipofariki na muda wote wa matatizo sikuwahi kuchagua upande

Hakuna kitu km hicho, uzae halafu wakulelee wengine, mzazi lazima uwajibike kwa mtoto uliemzaa. Kuna wazazi wengine wapuuzi sana. Mzazi usiyejua mtoto anakula nn, analala wapi, amevaa nn au akiumwa katibiwa na nani Kwa gharama zipi, mzazi wa hivyo huna tofauti na mnyama tena kuna baadhi ya wanyama wanalea watoto wao. Mtoto hawezi tu from nowhere asimjali mzazi lazima huyo mtu hakutimiza wajibu wake sawasawa akaachia wengine. Malipo ni hapa hapa duniani[emoji36]
 
Kama Mick Hacknal wa Simply Red
Nimekumbuka "Holding back the years"
Huyu jamaa alipitia mitihani sana lakini alikuja kuwa muimbaji ambaye ni mahiri sana

Ukiwa maarufu na maisha yako lazima yajulikane, hasa kama ulipitia maisha magumu

Sent from my SM-G570F using Tapatalk
 
Ni kiri tu mkuu, mimi ni miongoni mwa waliopitia hii dhahamaHadi sasa naishi kwa Anko tangu nikiwa na miaka 7, anko kanipeleka shule maana mzee alikataa na hata ndugu zangu wengine waliokuwa wanaishi na mzee walikataliwa kupelekwa shule. Maza alikomaa kivyake akawapeleka shule ndugu zangu wengine aliokuwa anaishi nao, Bro wangu alianzia MEMKWA hatimaye alifanikiwa kumaliza form 4 na Mungu akajalia akasonga mbele japo hajapitia Advance.

Mimi nilikomaa kwa Anko kibishi japo tunajua namna ya malezi kwa wasiokuwa wazazi wako yalivyo, nilisoma primary, secondary(O-level & A-level) hadi Chuo nishahitimu nipo mikononi mwa Anko huku Mzee yupo mzima wa Afya tu na hajawahi kuchangia hata kidogo kwenye malipo ya masomo yangu.

Nikifikiria mzee alivyokuwa mkatili ninaumia sana ila naishia kusema hakujua alitendalo na nishamsamehe, life linaendelea..

Wazee mara nyingi wanakuwa na viburi sana lakini pia wanawake nao wanachagia katika haya mambo ikiwemo kupandikiza chuki juu ya wazee kwa watoto.Mimi nishamsamehe, tunakula sahani moja kote kote na walionilea na yeye pia
Mara nyingi hawa wazee huwa wanaviburi ila hawafikirii mbali yatakayotokea hasa wakifika umri wa uzee.

Laiti wangejua siku moja wataachwa na watoto wao kama walivyowaacha wao wasingethubutu kufanya hivyo
Mungu akuzidishie kwa roho nyepesi!

Mungu akuongoze umsaidie anko mkuu maana kuchukua jukumu la mtu( baba ako) aliekua hai akajifanya amekufa kwa kujifanya dume la mbegu sio kazi ndogo aliyoifanya mjomba.

hii mifano tunayo mingi katika jamii zetu me nimeshuhudia mengi juu ya wababa kutelekeza watoto.

Nilitokwa na machozi siku moja nimeenda kumtembelea binamu yangu shule akiwa kidato cha pili, alikuja na rafiki yake kunipokea lakini rafiki yake alikua ana huzuni na kusononeka kuona wenzie wanakula vyakula na wazazi wao yeye hana mzazi aliekuja kumsalimia. nilipomuuliza binamu kwa lugha ya nyumbani akanambia hali ya rafiki yake ilinibidi nirudi mjini kuchukua chakula kingine ili asijione kama anadoea kwa rafiki yake.

Ambao hatuna watoto tujifunze kitu kupitia haya matukio sio kwamba vile leo wallet inazo noti za elfu kumi uwe na kibri hata kwa mtu ambae hata hajatembea kisa mama ake sio mzuri( umelala nae wa nini?) au hatuendani au ni jeuri!

kama mama ake hamuendani achana nae mapema!
 
Hayo ndiyo matokeo ya kuzalisha halafu unaingia mitini halafu unajiona mjanja kuwadharau single mothers. Mwanaume mwenzangu kama ulitelekeza mtoto na mama yake hakikisha hauhitaji msaada uzeeni. Watoto wa siku hizi siyo wale wa enzi zile sasa hivi JINO KWA JINO. UKINIKATAA BAADAE NITAKUKATAA
Nakazia............
 
mdingi alikataa katakata kwamba huyo siyo mtoto wangu sasa hivi anapiga U TURN

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna uhusiano gani kati ya kukataliwa au kutelekezwa na mzazi wa kiume na kuwa na kismati au kupendwa/kufanikiwa sana na kukubalika na jamii?

Hebu chunguza hawa watu maarufu utagundua kitu.
 
Ni kiri tu mkuu, mimi ni miongoni mwa waliopitia hii dhahamaHadi sasa naishi kwa Anko tangu nikiwa na miaka 7, anko kanipeleka shule maana mzee alikataa na hata ndugu zangu wengine waliokuwa wanaishi na mzee walikataliwa kupelekwa shule. Maza alikomaa kivyake akawapeleka shule ndugu zangu wengine aliokuwa anaishi nao, Bro wangu alianzia MEMKWA hatimaye alifanikiwa kumaliza form 4 na Mungu akajalia akasonga mbele japo hajapitia Advance.

Mimi nilikomaa kwa Anko kibishi japo tunajua namna ya malezi kwa wasiokuwa wazazi wako yalivyo, nilisoma primary, secondary(O-level & A-level) hadi Chuo nishahitimu nipo mikononi mwa Anko huku Mzee yupo mzima wa Afya tu na hajawahi kuchangia hata kidogo kwenye malipo ya masomo yangu.

Nikifikiria mzee alivyokuwa mkatili ninaumia sana ila naishia kusema hakujua alitendalo na nishamsamehe, life linaendelea..

Wazee mara nyingi wanakuwa na viburi sana lakini pia wanawake nao wanachagia katika haya mambo ikiwemo kupandikiza chuki juu ya wazee kwa watoto.Mimi nishamsamehe, tunakula sahani moja kote kote na walionilea na yeye pia
Mara nyingi hawa wazee huwa wanaviburi ila hawafikirii mbali yatakayotokea hasa wakifika umri wa uzee.

Laiti wangejua siku moja wataachwa na watoto wao kama walivyowaacha wao wasingethubutu kufanya hivyo

Upuuzi huo mie nimeukataa kwanza hatuna bond yoyote na hata tukikaa hatuna la kuongea mi na yeye mbalimbali hana mchango wowote katika Maisha yangu, ukaribu na Mimi aliuanza baada ya kusikia niko chuo kikuu, pasipo kuwa na mchango wowote katika Safari yangu ya Maisha na kielimu. Simuhitaji kwa lolote km ushauri naupata kwa aliyenilea, awepo asiwepo it doesn’t make any difference.
 
Swadaqta !!
Naomba usone kisa hiki

Kisa kama hiki kilitokea huko (jina na mji kapuni) " Jamaa baada ya kufariki dunia akaamua kwenda hadi mlangoni mwa jahanamu kuulizia maSwahiba zake...!! Akajibiwa kuwa msawahiba zako uliowaacha duniani walishatubu baada ya kifo chako, hivo hapa hawapo !! "

Jee msomaji umejifunza nini ktk issue hii !!
Kujifunza kitu kwenye vitu vya kufikirika tu visivyo na uhalisia?
 
Mungu akuzidishie kwa roho nyepesi!

Mungu akuongoze umsaidie anko mkuu maana kuchukua jukumu la mtu( baba ako) aliekua hai akajifanya amekufa kwa kujifanya dume la mbegu sio kazi ndogo aliyoifanya mjomba.

Amiin mkuu.

Na wewe akubariki sana na akufanyie wepesi katika mambo yako ya kila siku yaliyo mema kwa dua yako hii
 
Upuuzi huo mie nimeukataa kwanza hatuna bond yoyote na hata tukikaa hatuna la kuongea mi na yeye mbalimbali hana mchango wowote katika Maisha yangu, ukaribu na Mimi aliuanza baada ya kusikia niko chuo kikuu, pasipo kuwa na mchango wowote katika Safari yangu ya Maisha na kielimu. Simuhitaji kwa lolote km ushauri naupata kwa aliyenilea, awepo asiwepo it doesn’t make any difference.
Fuata nafsi yako inavyopenda na usiidhulumu hata kidogo.

Unaweza ukawa unamsaidia/kumjali lakini nafsi ikawa haijaridhia, pale utakuwa unatwanga maji kwenye kinu.

Kwa hiyo ni vizuri ubaki na msimamo wako huo huo uliouchagua.
 
Back
Top Bottom