Mwana FA amkana Baba yake mzazi

Mwana FA amkana Baba yake mzazi

Mtu mwenyewe anaomba msaada,hiyo jeuri ya kufufuana kuendesha bendi atakuwa nayo?nani siku hizi atataka kusikiliza Moro Jazz ,kwa kizazi kipi,wengine hizi ndio huita ndoto za alinacha .Ushauri mzee sasa atafute tu shamba aanze kulima matikiti maji,lakini hizo ndoto za kukufufua bendi ni kichekesho,
Labda ndio anaomba huo msaada wa kufufua bendi
 
Watangazaji wa siku hizi bana yani wanashindwa kuweka habari kwenye mtiririko mzuri...full repetition of words,that is the problem ya kutostick kwenye point
Utangazaji umerahisishwa sana Siku hizi, yaani Kila MTU ni mtangazaji
 
Ila wanaume wanachumisha watoto dhambi. Yaani mwana Fa anakosea ilakwa kosa la kutengenezewa mazingira
 
Watangazaji wa siku hizi bana yani wanashindwa kuweka habari kwenye mtiririko mzuri...full repetition of words,that is the problem ya kutostick kwenye point
Huyu jamaa anayetangaza ni mseng* badala ya kutangazwa habari za mwanafa anatangaza habari za diamond
 
Hichi kizazi nacho kimezidi kuwakana baba zao...

Super hero daddy
Tatizo wazazi wengi wanapenda kuvuna kutoka kwa watoto wao bila ku-invest kwa watoto wakiwa wadogo. Hakuna faida bila kuwekeza. Wengi wameamua kuwa sperm donors, tatizo wanadai faida kubwa baadae.
Nina experience ya kijana hakuwahi kumjua wala kupata huduma ya mzazi wa kiume. Baba alikataa kuanzia mimba hadi mtoto. Mtoto kalelewa na mama, alipomaliza chuo na kuwa anajitegema na maisha yake, akambana mama yake na kumtafuta baba yake. Baba alipomuona tu, kitu cha kwanza ni kuomba kununuliwa gari pickup. Baba hajui mtoto alikula nini, alisomaje, lakini now anataka kuvuna matunda ya jasho la wengine kumlelea mwanae. Alichoamua kijana ni kuwawezesha kimaisha wadogo zake kwa huyo baba (yeye kwa mama yupo peke yake), lakini kagoma kumpa baba yake direct financial assistance. Mtoto kasema huyu baba hawezi kuvuna kitu ambacho hakupanda.
 
Ila tukumbuke mzazi ni mzazi tu...mimi kwangu haijalishi nn kilitokea huko nyuma lkn wazazi wangu niliwapa upendo sawa. Ingawa kuna miaka dingi alikuwa na mchepuko akamzingua sana maza lkn mwisho wa siku walielewana na maisha yakaendelea mpk alipofariki na muda wote wa matatizo sikuwahi kuchagua upande
Baba/ mama kuwa na mchepuko si tatizo lako. Ila kukukana na kukataa kukuhudumia ni kesi tofauti ya wewe pia kumkana baadae
 
Hili jambo tukilitazama kwa undani zaidi ni jambo kubwa sana na lina mzizi mrefu.

Tukumbuke mwanamke naye anachangia kutokea kwa hili jambo.

Kwa upande mwingine wanawake wanajirahisisha kwa wanaume mwishowe wanaachwa na watoto kutwlekezwa maana mwanaume hakuwa na nia na mwanamke isipokuwa ni kwa haja ya muda mfupi tu.
Sasa kama ni haja ya muda mfupi si ujichukulie huna mtoto.Kwa ninin unamsumbua mtoto akuhudumie ukiona kafanikiwa?
 
Back
Top Bottom