Mwana FA autetea wimbo Mwanza wa Rayvanny na Diamond Platnumz

University_Promo

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2018
Posts
749
Reaction score
661
Harakti bado zinaendelea kama kawaida kuhusiana wimbo wa mwanamziki Rayvanny na Diamond Platnumz a.k.a Baba Tiffa wa Mwanza Nyegezi.
Na mambo yapo kama hivi.

Rapper Mwana FA ametinga BASATA kama mjumbe wa Bodi la Baraza hilo,Kuomba adhabu iliyotolewa kwa Rayvanny na Diamond Platnumz kufungia wimbo wa wao wa Mwanza Nyegezi aidha ifutwe au ipunguzwe.
Akiongea na Waandishi wa Habari mapema Leo Novemba 14,2018 Mwana FA amesema wimbo wa Mwanza ni mzuri kusikiliza kwa kijana aliyevuka miaka 18, hivyo BASATA wangeangalia na namna ya kufuta adhabu hiyo.
"Alisema MWANA FA"
==============================
Vipi kuhusiana na wewe mdau?
Toa maoni yako.
 
Mwangwi wa sauti ya kusikiliza haichagui umri. Kwakua hata wao wasinii wenyewe wanakili ni nyimbo ya ki utu uzima, maana yake nyimbo ina kasoro. Mimi naungana na basata, hatuungi mkono kufungiwa wasanii nyimbo zao bali kuwatia adabu kidogo. Na kwakua wasafi ndo magwiji wa music kwa sasa kuwaadhibu wao ndo Mahala pake. Ukitka kumdhibiti nyoka mkamate kichwani.
 
utakufa siku si zako kwa roho mbaya nyegezi wewe
 
Hivi ni kipi kwa mfano kinachokufanya uamini ule wimbo haufai?! Unaweza kunitajia mistari michafu kwenye ule wimbo?!
 
Tutaanza kuhoji shahada za mwana Fa sasa. . maana sio kwa kutoa boko huku ... kwani nchi hii ina station radio na tv ambazo huwa zinarusha mawimbi yao ya habari kwa watu wazima tu pekee !!....?
 
Nimekaa hapa nasikiliza wimbo flani, sikumbuki umeimbwa na nani....sehemu ya Mashairi yake yanasema...

"Muhogo wa jang'ombee, sijauramba Mwiko, usitukane Wakungaaa, na Uzazi ungalipoo"
 
swali lako waulize wcb ambao wanasema ule wimbo ni kwaajili ya watu wazima tu. Tena wakaenda mbele zaidi kwa kusema hata wasafi festival utapigwa usiku mnene tu.
Nimekuuliza wewe! Kama huna jibu, sema huna jibu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…