Mwana FA: Kuendesha timu Kabla ya kukamilisha taratibu za kisheria za uwekezaji chanzo cha Mgogoro Simba

Mwana FA: Kuendesha timu Kabla ya kukamilisha taratibu za kisheria za uwekezaji chanzo cha Mgogoro Simba

Bila bila

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2016
Posts
22,168
Reaction score
39,118
Akiongea Jana kwenye hafla ya uzinduzi wa kitabu cha historia ya klabu ya Yanga, Mwana FA ambaye ni Naibu Waziri wa michezo, alisema kitendo cha viongozi na wanachama wa Simba kukubali kuendesha timu Kwa miaka 6 bila kukamilisha mchakato wa mabadiliko ya katiba na sheria za uendeshaji wa timu hiyo kuwa kampuni ndiyo chanzo kikubwa cha Mgogoro unaoendelea Sasa.

Aliongeza kusema Kwa Sasa serikali imewaachia wanachama na viongozi waumalize wenyewe lakini itakapoona unaanza kuathiri ukuaji wa soka nchini serikali itaingilia Kati.

Binafsi naungana na Naibu Waziri kwenye hoja yake. Naamini sababu ya Mgogoro huu kuwa mkubwa na kutokuwepo Kwa taratibu zilizo Wazi za uendeshaji wa timu.

Mpaka Sasa Hakuna sheria inayoeleweka iliyoweka mamlaka ya Mwekezaji na mamlaka ya wanachama hasa baada ya mchakato wa awali wa katiba ya Simba sports club company kusitishwa na Baraza la michezo likiwataka Simba aabadilishe kipengele cha 49% ya hisa za upande wa Mwekezaji kumilikiwa na watu 3 badala ya kuhodhiwa na Mtu mmoja kama ilivyo Sasa.

Kwa maana nyingine Mwana FA anasema Simba inaendeshwa kinyemela bila katiba. Na Kwa vile Miaka minne nyuma Mambo yalikuwa yanakwenda vizuri, timu iliachwa iende bila kujua huko mbele lazima watakwama.

Hapa nailauamu serikali na mamlaka zinazosimamia michezo Kwa kitendo cha kuona timu inaendeshwa kinyume cha taratibu lakini Kwa vile inashinda Hakuna anayeshauri au kuchukua hatua. Kipindi kizuri cha kufanya mabadiliko salama ilikuwa ni kipindi timu inapata mafanikio. Kusubiri Mambo yaharibike tuseme "tulijua hawatafika mbali" siyo sahihi.

Kama wizara inajua kuna timu nyingine ina mazingira kama haya na haichukui hatua eti Kwa vile inafanya vizuri basi viongozi wa wizara na wote wanaosimamia michezo wajitafakari maana wanafunika Moto chini ya miguu yao.

Tunaona timu inaendeshwa bila kujua katiba inayotumika ni ya kampuni ambayo ilikataliwa na Baraza na ndiyo aliyotumia Abdalla Mhene "kumteua" Mo kuwa Mwenyekiti baada ya yeye kujiuzulu au ni ya zamani ya mpito kuelekea kampuni ambayo ndo Mangungu aliitumia kusema àlipojiuzulu Try Again Bodi itakaa ichague Mwenyekiti mpya?

Ushauri wangu Kwa wanasimba ni kutokubali kutafuta suluhisho la funika Kombe mwanaharamu apite ili timu itulie Kwa Muda. Wahakikishe Kila kitu kinawekwa Sawa Sasa hata kama watachelewa kupata mafanikio lakini watengeneze timu iliyojengwa kwenye misingi imara ambapo Kila upande ndani ya Simba utakuwa na HAKI na WAJIBU bila kuingilia upande mwingine.
 
Muda si mrefu utashangaa wanaanza kumtuhumu na huyo mwenzao Mwana FA, kisa tu kaongea ukweli wasio upenda! Wanachotaka wao ni furaha tu!!

Hata timu ikiwa haina katiba, au mfumo mzuri wa uendeshaji; kwao siyo tatizo. Wakiitwa mbumbumbu, wanakasirika!
 
Akiongea Jana kwenye hafla ya uzinduzi wa kitabu cha historia ya klabu ya Yanga, Mwana FA ambaye ni Naibu Waziri wa michezo, alisema kitendo cha viongozi na wanachama wa Simba kukubali kuendesha timu Kwa miaka 6 bila kukamilisha mchakato wa mabadiliko ya katiba na sheria za uendeshaji wa timu hiyo kuwa kampuni ndiyo chanzo kikubwa cha Mgogoro unaoendelea Sasa. Aliongeza kusema Kwa Sasa serikali imewaachia wanachama na viongozi waumalize wenyewe lakini itakapoona unaanza kuathiri ukuaji wa soka nchini serikali itaingilia Kati.
Binafsi naungana na Naibu Waziri kwenye hoja yake. Naamini sababu ya Mgogoro huu kuwa mkubwa na kutokuwepo Kwa taratibu zilizo Wazi za uendeshaji wa timu. Mpaka Sasa Hakuna sheria inayoeleweka iliyoweka mamlaka ya Mwekezaji na mamlaka ya wanachama hasa baada ya mchakato wa awali wa katiba ya Simba sports club company kusitishwa na Baraza la michezo likiwataka Simba aabadilishe kipengele cha 49% ya hisa za upande wa Mwekezaji kumilikiwa na watu 3 badala ya kuhodhiwa na Mtu mmoja kama ilivyo Sasa.
Kwa maana nyingine Mwana FA anasema Simba inaendeshwa kinyemela bila katiba. Na Kwa vile Miaka minne nyuma Mambo yalikuwa yanakwenda vizuri, timu iliachwa iende bila kujua huko mbele lazima watakwama. Hapa nailauamu serikali na mamlaka zinazosimamia michezo Kwa kitendo cha kuona timu inaendeshwa kinyume cha taratibu lakini Kwa vile inashinda Hakuna anayeshauri au kuchukua hatua. Kipindi kizuri cha kufanya mabadiliko salama ilikuwa ni kipindi timu inapata mafanikio. Kusubiri Mambo yaharibike tuseme "tulijua hawatafika mbali" siyo sahihi.
Kama wizara inajua kuna timu nyingine ina mazingira kama haya na haichukui hatua eti Kwa vile inafanya vizuri basi viongozi wa wizara na wote wanaosimamia michezo wajitafakari maana wanafunika Moto chini ya miguu yao. Tunaona timu inaendeshwa bila kujua katiba inayotumika ni ya kampuni ambayo ilikataliwa na Baraza na ndiyo aliyotumia Abdalla Mhene "kumteua" Mo kuwa Mwenyekiti baada ya yeye kujiuzulu au ni ya zamani ya mpito kuelekea kampuni ambayo ndo Mangungu aliitumia kusema àlipojiuzulu Try Again Bodi itakaa ichague Mwenyekiti mpya?
Ushauri wangu Kwa wanasimba ni kutokubali kutafuta suluhisho la funika Kombe mwanaharamu apite ili timu itulie Kwa Muda. Wahakikishe Kila kitu kinawekwa Sawa Sasa hata kama watachelewa kupata mafanikio lakini watengeneze timu iliyojengwa kwenye misingi imara ambapo Kila upande ndani ya Simba utakuwa na HAKI na WAJIBU bila kuingilia upande mwingine.
Kwa maneno rahisi ngoja wapate akili baada ya kupata changamoto, ni kawaida Kwa binadamu akipata changamoto huamsha ubongo wake hivyo huweza kutatua changamoto zake, tuwaache fuvu lifanye kazi kwa maana mashibiki wa Simba ni mbumbumbu, ulimwengu wa Sasa unahitaji, (reflective practice), yaani mawazo mbadala yenye fikra chanya,
 
Muda si mrefu utashangaa wanaanza kumtuhumu na huyo mwenzao Mwana FA, kisa tu kaongea ukweli wasio upenda! Wanachotaka wao ni furaha tu!!

Hata timu ikiwa haina katiba, au mfumo mzuri wa uendeshaji; kwao siyo tatizo. Wakiitwa mbumbumbu, wanakasirika!
Furaha Bila ukweli huwezi kuipata Manala hupenda kusema Simba wanapenda kuendesha mambo Kwa ,(chupri chupri),yaani kiujanja ujanja
 
Swala la kuendesha timu bila kukamilika kwa mchakato wa mabadiliko halipo kwa Simba pekee, hata Yanga yenyewe inaendeshwa bila kukamilika kwa mchakato wa mabadiliko. Katiba iliyopitishwa Yanga sio inayotumika kwasasa. Kwa Yanga labda imekuwa na lugha tofauti kwamba wao bado hawajampa timu mwekezaji ila Simba wamempa mwekezaji tayari ambaye anaendesha timu kinyume na maagizo ya serikali.
 
Swala la kuendesha timu bila kukamilika kwa mchakato wa mabadiliko halipo kwa Simba pekee, hata Yanga yenyewe inaendeshwa bila kukamilika kwa mchakato wa mabadiliko. Katiba iliyopitishwa Yanga sio inayotumika kwasasa. Kwa Yanga labda imekuwa na lugha tofauti kwamba wao bado hawajampa timu mwekezaji ila Simba wamempa mwekezaji tayari ambaye anaendesha timu kinyume na maagizo ya serikali.
Samahi kidogo mkuu, hebu nifungue boliti za ubongo, kwani timu zetu hizi zinaendeshwa kwa mujibu wa maagizo ya Serkali?
 
Samahi kidogo mkuu, hebu nifungue boliti za ubongo, kwani timu zetu hizi zinaendeshwa kwa mujibu wa maagizo ya Serkali?
Nanukuu "mchakato wa awali wa katiba ya Simba sports club company kusitishwa na Baraza la michezo likiwataka Simba aabadilishe kipengele cha 49% ya hisa za upande wa Mwekezaji kumilikiwa na watu 3 badala ya kuhodhiwa na Mtu mmoja kama ilivyo Sasa."

Mwisho wa kunukuu
 
Mwana FA anamjua anayekwamisha huo mchakato kukamilika?

Kuna wale viumbe wanaitwa UCC kama sijakosea hao ndio chanzo cha yote, wamekuwa wakiweka vikwazo kila mara Mo anapotaka kukamilisha mchakato.

Kwa hili Mo asilaumiwe.
 
Akiongea Jana kwenye hafla ya uzinduzi wa kitabu cha historia ya klabu ya Yanga, Mwana FA ambaye ni Naibu Waziri wa michezo, alisema kitendo cha viongozi na wanachama wa Simba kukubali kuendesha timu Kwa miaka 6 bila kukamilisha mchakato wa mabadiliko ya katiba na sheria za uendeshaji wa timu hiyo kuwa kampuni ndiyo chanzo kikubwa cha Mgogoro unaoendelea Sasa.

Aliongeza kusema Kwa Sasa serikali imewaachia wanachama na viongozi waumalize wenyewe lakini itakapoona unaanza kuathiri ukuaji wa soka nchini serikali itaingilia Kati.

Binafsi naungana na Naibu Waziri kwenye hoja yake. Naamini sababu ya Mgogoro huu kuwa mkubwa na kutokuwepo Kwa taratibu zilizo Wazi za uendeshaji wa timu.

Mpaka Sasa Hakuna sheria inayoeleweka iliyoweka mamlaka ya Mwekezaji na mamlaka ya wanachama hasa baada ya mchakato wa awali wa katiba ya Simba sports club company kusitishwa na Baraza la michezo likiwataka Simba aabadilishe kipengele cha 49% ya hisa za upande wa Mwekezaji kumilikiwa na watu 3 badala ya kuhodhiwa na Mtu mmoja kama ilivyo Sasa.

Kwa maana nyingine Mwana FA anasema Simba inaendeshwa kinyemela bila katiba. Na Kwa vile Miaka minne nyuma Mambo yalikuwa yanakwenda vizuri, timu iliachwa iende bila kujua huko mbele lazima watakwama.

Hapa nailauamu serikali na mamlaka zinazosimamia michezo Kwa kitendo cha kuona timu inaendeshwa kinyume cha taratibu lakini Kwa vile inashinda Hakuna anayeshauri au kuchukua hatua. Kipindi kizuri cha kufanya mabadiliko salama ilikuwa ni kipindi timu inapata mafanikio. Kusubiri Mambo yaharibike tuseme "tulijua hawatafika mbali" siyo sahihi.

Kama wizara inajua kuna timu nyingine ina mazingira kama haya na haichukui hatua eti Kwa vile inafanya vizuri basi viongozi wa wizara na wote wanaosimamia michezo wajitafakari maana wanafunika Moto chini ya miguu yao.

Tunaona timu inaendeshwa bila kujua katiba inayotumika ni ya kampuni ambayo ilikataliwa na Baraza na ndiyo aliyotumia Abdalla Mhene "kumteua" Mo kuwa Mwenyekiti baada ya yeye kujiuzulu au ni ya zamani ya mpito kuelekea kampuni ambayo ndo Mangungu aliitumia kusema àlipojiuzulu Try Again Bodi itakaa ichague Mwenyekiti mpya?

Ushauri wangu Kwa wanasimba ni kutokubali kutafuta suluhisho la funika Kombe mwanaharamu apite ili timu itulie Kwa Muda. Wahakikishe Kila kitu kinawekwa Sawa Sasa hata kama watachelewa kupata mafanikio lakini watengeneze timu iliyojengwa kwenye misingi imara ambapo Kila upande ndani ya Simba utakuwa na HAKI na WAJIBU bila kuingilia upande mwingine.
Wasichokifahamu wanachama wa Simba ni siku MO akifilisika au akiona timu haina manufaa kwake kitakuwa kisanga kikubwa! Ndiyo maana Kaduguda na Rage wanawaita mbumbumbu🤣🤣
 
Means fa kama mwanachama wa Simba kweli anaacha tatizo limalizwe na wanachama wenyewe
Hili tatizo wamelitengeza viongozi na wanachama,(mashabiki), kinadharia akili zilezile zilizo tengeneza tatizo haziwezi kutatua tatizo, lakini binadamu akipata changamoto huamsha ubongo wake na kutatua changamoto zake tusome, what causes uncertainty and how to overcome uncertainty
 
Mwana FA anamjua anayekwamisha huo mchakato kukamilika?

Kuna wale viumbe wanaitwa UCC kama sijakosea hao ndio chanzo cha yote, wamekuwa wakiweka vikwazo kila mara Mo anapotaka kukamilisha mchakato.

Kwa hili Mo asilaumiwe.
UCC wamefanyaje? Elezea
 
Kuna mambo yanashangaza sana! Serikali kupitia vyombo vyake kama FCC na BMT tayari wameshaweka muongozo kwamba uwekezaji unaotakiwa ni wanachama wamiliki hisa 51% na mwekezaji awe na hisa 49% tena mwekezaji asiwe mmoja lakini kinatokea kikundi cha watu wachache kwa sababu ya maslahi yao binafsi wanapindisha pindisha halafu tena serikali hiyo hiyo inasema eti inawaachia wenyewe kwanza wamalizane wakishindwa ndipo serikali iingilie kati sasa sijui inasubiri timu ivurugike kiasi cha kukosekana amani ndipo watajua wameshindwa! Wakati ndiyo huu serikali iingilie kati kuinusuru Simba kwa maslahi ya walio wengi.
Kweli tunataka timu ifanye vizuri sisi mashabiki ndiyo raha yetu lakini siyo kwa mtu mmoja kuipora timu kwa sababu ya fedha zake.
 
Kwani timu zipi mbali na zile zinazomilikiwa na watu binafsi zimekamilisha hizo taratibu za uwekezaji na hazina hiyo migogoro?
 
Back
Top Bottom