Mwana J.F..Unakula Tsh.ngapi kwa siku?

Mkuu samahani,Chakula tu kwanza....
 
Asubuhi Chapati Moja,bakuli la maharage, chai na yai la kienyeji moja kazi inaanza (2000), mchana Ugali wa dona na maharagwe 2500(my favoured dish) + maji ya 500=3000 jioni aina tofauti ya msosi usiozidi 5000 Jumla kwa siku chakula na maji wastani wa kama 10000 hivi anasa za chakula kwangu mara nyingi wikiendi
 
Kwa kweli weekend hasa jumamosi nimeamua niiache kwasababu huwa inatumika bajeti kubwa kuliko ya wiki nzima! Sometimes unarudi home huamini umetumia kiasi fulani kirahisi tu.
Mwenyewe nimeamua kukausha, weekend zilitaka kuniletea uchizi!

Yaani mi ikifika ijumaa jioni mda wa kutoka job akili inaniruka, nafikiria kujaza gari wese na kutafuta sehemu za kula bata, hiyo ni kuanzia ijumaa, j'mosi naj' pili!

Namshukuru mungu nina mwezi sasa sishoboki na weekend na savings naiona!
 
Hicho kifurushi si ni cha 24hrs?

We mbona unasema siku nne?
 
Kuna mahali nimehamia miezi minne sasa yaani najutia dunia!
15,000TZS na kuendela pa day
Detail:
Asubuhi: 3,500-4,000TZS. Maziwa au chai kikombe kidogo...500, andazi/chapati..500, supu...3000
Mchana: 5,000-6,000TZS.
Ugali....2500, wali.....3500-4000
Jioni: 5,000-6,000TZS.
Ugali....2500, wali.....3500-4000, pilau....4000. Ukila ugali kuku ni 3500
Nahapo sinywi bia. Soda sio lazima sana maji kama kawaida......tushauliane aiee. naona kwa mwezi inakula kwangu maana kipato chenyewe sio kikubwa kwa kuhimili hii gharama
 
Mchana na kula kama 2000 tu jioni najipikilisha nikijaza gesi 17000 inakaa hadi miezi 3 unga k 3 =2400 unatoboa wiki nzima
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…