Mwanachuo wa mwaka wa kwanza SAUT Mwanza amejinyonga leo asubuhi

Mwanachuo wa mwaka wa kwanza SAUT Mwanza amejinyonga leo asubuhi

fidelity

Member
Joined
Apr 22, 2012
Posts
91
Reaction score
11
Inasikitisha sana kwa msomi kuchukua maamuzi magumu kama haya.Tunasubiri polisi wafike eneo la tukio ili tupate taarifa za kina.

====== Updates =========

Ni kweli hii taarifa na shuhuda wamedai ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza,kitivo cha elimu.Taarifa za awali zinatanabaisha kwamba kijana huyo alibaki chumbani peke yake na aliagana vizuri na mwenziwe (wa kiume) aliyekuwa ameelekea lecture.Rafiki yake aliporudi ndipo alipokuta mwenzie amejitundika eneo alilokuwa anakaa ni jirani ya eneo wanapopaki pikipiki juu ya hostel ya Lema (ghorofa linaloendelea kujengwa).

Kwa maelezo mengine ni kama mita 150 magharibi-kaskazini mwa hostel ya Masha.

Polisi kwa kushirikiana na uongozi wa chuo wameutwaa mwili wa marehemu na kuupeleka chumba cha kuhifadhia maiti huku uchunguzi juu ya chanzo kujitoa uhai ukiendelea.

Taarifa kamili itakatolewa na wahusika italetwa hapa jamvini
 
Mwanachuo wa mwaka wa kwanza saut malimbe kampas ajinyonga leo asubuhi
 
Inasikitisha sana, naomba yasiwe maswala ya mapenzi maana inauma sana mtu kujitoa uhai wake wakati wazazi wamemuangaikia toka mchanga alafu anakutana na mtu mtu baki tu eti hawezi kuishi bila yeye.
 
Chanzo bado hakijafamika ila tutaleta taarifa muda si mrefu tunasubia polisi kufika eneo la tukio ili tupate habari za uhakika zaidi
 
Ni mshikaji tu amekutwa na roomate wake ananing'inia ndipo nasi tukaenda kushuhudia
inasikitisha sana
 
tatizo ni nini maskini oneeni wazazi huruma wanavyohangaika kuwasomesha...
 
huyo itakua amevamia mji vibaya kala mzigo ulioathirika ndo kaamua kujimaliza RIP KIJANA
 
Mwanachuo wa mwaka wa kwanza saut malimbe kampas ajinyonga leo asubuhi
Too shallow information to us...Weka vitu kamili hapa au ulikuwa unakimbizana na muda wa hewani - internetAndika habari kamili kwenye Ms word; ukimaliza i-paste hapa kwenye jamii kama hii ndo shida ilikufanya uandike hivi...
 
Mwanaume akijiua na asipoacha ujumbe ujue madeni au hali ngumu ya maisha
 
Ni mshikaji tu amekutwa na roomate wake ananing'inia ndipo nasi tukaenda kushuhudia
inasikitisha sana
mwaka wa ngapi....faculty........anakaaa hosteli gani...........mwaka jana nao si kuna mmoja alijinyonga
 
WANAFUNZI WANA CHANGAMOTO NYINGI SANA, HASA WA AWAMU HII YA NNE!!! LAKINI,Nini kimemsibu?..RIP MWANAFUNZI
 
Back
Top Bottom