Mwanafunzi aliyefunika hisabati darasa la saba

Mwanafunzi aliyefunika hisabati darasa la saba

Safi sana,sasa ajipange vizuri na elimu ya Sekondari,ingekuwa nchi za wenzetu huyu angekuwa anafuatiliwa na kuwezeshwa kufikia malengo muhimu ya nchi lakini hapa baada ya sifa na vijizawadi visivyo na maana mtoto huyu hutomsikia tena labda afanye tena vizuri Sekondari.

Unaweza kuta kapangiwa shule ya kata kule Kisarawe nyuma kule na kipaji chake kikafia huko. Mungu mlinde mtoto huyu, anaweza kuja kutuokoa huko tuendako.
 
Beauty with brains...kazuuuriiii kenyewe....the way she smiles ....oooooohhh...God Protect her..afikie ndoto zake
 

Attachments

  • 1415373903940.jpg
    1415373903940.jpg
    19.5 KB · Views: 483
Mimi nimeshahifadhi jina lake sehemu, 2018 nitaangalia matokeo yake ya Form 4, namuomba mungu atuweke salama mimi, yeye na wana JF tuliofurahishwa na matokeo yake, manake hizi ajali za magari zinatumaliza, kila siku humu JF hapakosekani ajali ya gari tena iliyoua, sijui ifunguliwe ya Ajali Forum!
 
Continuous assessment ...zinakuwa considered pia....ukute hao wengine walikua na average ndogo ktk test ...so huenda yy aliwazidi

Nijuavyo mimi,(ndivyo ilivyo)kwa shule za msingi huwa hawazingatii kitu hicho(continous assessment)
 
Alama za juu kivip wakati alama ya juu kabisa ndo hiyo 50,na waliopata 50/50 wapo 30? Sasa yeye kaongoza kwa kigezo gani hapo?Nawaomba waandishi wa habari hiyo watupe ufafanuzi tafadhal.
usanii tuu halafu ni multiple choice.Yaani watawala wanawadharau sana wananchi
 
Hongera binti mzuri kwz kusona kwa bidii bila kuringia uzuri wako.
 
Alama za juu kivip wakati alama ya juu kabisa ndo hiyo 50,na waliopata 50/50 wapo 30? Sasa yeye kaongoza kwa kigezo gani hapo?Nawaomba waandishi wa habari hiyo watupe ufafanuzi tafadhal.

Waii mimi sitaki hata kujua
 
RacheKiunsi-November7-2014.jpg

Mwanafunzi aliyefunika hisabati darasa la 7

Mwanafunzi bora wa somo la Hisabati katika mitihani ya taifa ya darasa la saba iliyofanyika nchini Septemba mwaka huu, Rachel Kiunsi (13).
Mwanafunzi bora wa somo la Hisabati katika mitihani ya taifa ya darasa la saba iliyofanyika nchini Septemba mwaka huu, Rachel Kiunsi (13), ameeleza siri ya mafanikio yake kuwa ni kujituma katika masomo na kuwaheshimu walimu.

Akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu jana kutoka mkoani Singida, Rachel ambaye alikuwa anasoma shule ya msingi Kimara 'B', jijini Dar es Salaam, alisema alikuwa na bidii ya kujituma katika masomo yake hasa katika la hisabati na ya Sayansi na kwamba alikuwa anashindwa kupata usingizi bila kujisomea usiku.

Akizungumzia jinsi alivyopokea taarifa za matokeo yake, Rachel alisema ni kwa furaha na alikuwa akitengemea kufaulu, lakini siyo kwa mafanikio kama hayo aliyoyapata.
“Nanamshukuru sana Mungu kwani nilikuwa namwomba atende maajabu katika matokeo yangu... nilikuwa nasali kila nikifanya mtihani na kumaliza,” alisema Rachel, ambaye alikuwa akiishi na bibi yake Kimara.

Aliwashukuru walimu wake wa masomo yote kwa juhudi za kuwafundisha vizuri wanafunzi wote katika shule hiyo kwani walikuwa wakiingia darasani kwa muda wa ziada na kutoka saa 11 jioni.

“Mimi nawashauri wanafunzi wenzangu tuliomaliza wote na kufaulu kuwa tuongeze bidii katika masomo yetu ya Sekondari kwani bila juhudi hatutaweza kufaulu kama tulivyofaulu sasa,” alisema.

Akielezea masomo anayoyapenda, Rachel, alisema kuwa ni ya Sayansi na ndoto zake zilikuwa ni kusoma katika shule ya sekondari ya vipaji maalumu ya wasichana ya Kilakala iliyopo mkoani Morogoro.

MAMA MZAZI AZUNGUMZA
Kwa upande wake, mama mzazi wa mwanafunzi huyo, Grace Kiunsi, akizungumza na NIPASHE kwa simu kutoka Singida, alisema matokeo ya mtoto wake aliyapata kwenye tovuti ya Baraza la Mitihani la Taifa (Nacte) na alifurahi, lakini hakufahamu kama ameongoza katika somo la Hisabati.

“Kusema ukweli nilipata furaha ya hali ya juu baada ya kuona matokeo ya mwanangu kuwa amefaulu kwa daraja la kwanza ‘A’, kwa masomo yote nilimpigia simu baba yake ambaye yupo masomoni katika Chuo cha Biblia Dodoma na kumweleza naye alifurahi sana,” alisema Kiunsi.

Alisema taarifa za kuwa mwanaye ameibuka kinara wa hisabati nchi nzima alizipata kupitia gazeti la NIPASHE ndipo furaha yake ilipozidi kwani hakufaulu kwa daraja la kwanza tu bali hata kitaifa.

Aliongeza kuwa mwanaye hakuna kitu anachopenda zaidi ya kusoma kwani kuna wakati mwingine alikuwa anashindwa kula au kulala kama hajamaliza kazi alizopewa na walimu wake shuleni.

“Rachel alikuwa ni mwenye heshima sana kwa walimu wake ilifika kipindi hata wazazi wake alikuwa hatutii kama anavyowatii walimu wake,” alisema Kiunsi.
Alisema hiyo ndiyo siri ya mafanikio ya mwanaye katika masomo yake, hivyo aliwaomba walimu wa shule aliyosoma Rachel kuongeza bidii kwani ndiyo zitakazoinua shule yao.

MWALIMU MKUU ASIMULIA

Naye Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Zuxine Mponda, alisema Rachel alikuwa ni mtoto wa kipekee katika shule yake kwani alikuwa ni mtiifu, msafi, mpole na msikivu kwa walimu wake.

Alisema walimu walikuwa wanategemea matokeo mazuri kwa wanafunzi wao kwani shule yake ina misingi mizuri ya kuaandaa wanafunzi kufaulu mitihani yote sio tu ya mwisho.

Alisema mwanafunzi huyo alikuwa akiongoza katika mitihani ya majaribio (moku), ya wilaya na mkoa na wastani aliokuwa akiupata ni wa 50 kwa 50 hasa katika Hisabati.

Mwalimu Mponda, alisema kuwa katika matokeo ya mtihani wa mwisho wa darasa la saba mwaka 2012 shule yake ilishika nafasi ya tatu kiwilaya na wanafunzi watatu walishinda kwenda katika shule ya Sekondari vipaji ya wanaume ya Ilboru.

Alisema wanafunzi waliomaliza darasa la saba katika shule yake mwaka huu ni 191 huku wasichana wakiwa 90 na wavulana 101.

Mpanda alisema wanafunzi waliopata alama ‘A’ katika somo la hisabati ni 37, Kingereza 13, Sayansi 12, Maarifa 16 na Kiswahili 16.

Aliongeza kuwa kutokana na ufaulu huo matokeo ya shule yake ni mazuri kwani wanafunzi waliopata daraja la kwanza ‘A’ katika masomo yote walikuwa watatu huku ‘A’ zikiwa ni 13 ‘B’ 76, ‘C’ 84, ‘D’ 18 huku hakuna mwanafunzi aliyepata alama ya F au E.

Aliongeza kuwa utamaduni wa shule hiyo kwa mwanafunzi yoyote aliyefanya vizuri ni kupewa zawadi hivyo wakapofanya kikao cha kamati ya shule watachagua zawadi ya kumpa mwanafuzi huyo.

Aliitaka Serikali kubadilisha utaratibu wa kulinganisha wastani kwa shule za Serikali na shule binafsi ili kumpata mwanafunzi bora au shule bora kwani mazingira ya ufundishaji ni tofauti .

MWALIMU WAKE AMWELEZEA
Naye mwalimu wa Hisabati shuleni hapo, Aron Mwinyi, alieleza siri ya mafanikio ya ufaulu huo kwa wanafunzi wake kwa kusema waliandaliwa vyema.

Alieleza kuwa shule hiyo ina utaratibu wa kuwaandaa wanafunzi toka awali na kuwajengea ukaribu ili wanapokuwa na tatizo masomo iwe rahisi kutatuliwa.

Alielezea sifa za Rachel na kusema kuwa alikuwa ni mwanafunzi makini tangu darasa la tano kwani alikuwa akiwasumbua walimu pale anapokuwa hajaelewa na hiyo ikamjengea uwezo wa kuongoza darasani katika kila somo.

“Katika shule yetu hapa hakuna tabia ya wanafunzi kujitenga kwa kujiona kuwa wanaakili sana, hapa wanafunzi wote ni sawa na wanafundishana na hiyo ndio sababu kuu ya ushindi huu kwa shule yetu,” alisema Mwinyi.

Mwinyi aliongeza kuwa walimu wanashirikiana katika ufundishaji kwani wakati mwanafunzi anakuwa na shida na mwalimu wake wa somo hayupo, mwanafunzi akimwona mwalimu yeyote anamsaidia.

Kwa upande wa mwalimu wa Kingereza, Privatus Mbehoma, alisema ni faraja kwa wanafunzi wao kufaulu masomo ya Kingereza na maarifa kwani ni masomo ambayo ufaulu wake ni mdogo lakini kwa shule yake wamefaulu kwa kiwango cha kuridhisha.

Juzi Katibu Mtendaji wa Necta, Dk. Charles Msonde, alitangaza matokeo ya mitihani ya darasa la saba uliofanyika Septemba mwaka huu huku wavulana wakiwa wameongoza na kanda ya ziwa ikitoa shule nane katika 10 bora.

Matokeo hayo yalionyesha kuwa watahimiwa wengi hawakufanya vizuri somo la Hisabati lenye ufaulu wa asilimia 37.56 huku somo la Kiswahili ufaulu wake ukiwa unaongoza kwa asilimia 69.70.

Katika Somo la Hisabati kati ya watahimiwa 34 waliopata 50 kwa 50 wasichana ni nane na wavulana ni 26.

UPINZANI WAKOSOA MATOKEO

Waziri kivuli wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Susan Lymo (Chadema), amesema ongezeko la ufaulu wa darasa la saba mwaka huu haufanani na halisi inayoonekana kwenye sekta ya elimu nchini.

Taarifa ya Necta) ilisema ufaulu umeongezeka kwa asilimia 6.38 ikilinganishwa na mwaka jana.

Lyimo alisema ili kutokea kiwango hicho cha ufaulu, sekta ya elimu ingeonekana kuwa na mabadiliko ya dhahiri tofauti na sasa ambapo kinachoshuhudiwa ni matamko, kama vile Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN).

Lymo ambaye kitaaluma ni mwalimu, alisema pamoja na hali hiyo, ufaulu hafifu unaoendelea kuonekana kwenye somo la Hisabati ni kiashiria
kikuu cha uwezo duni wa wahitimu.

Alisema mwanafunzi yeyote anayefaulu somo hilo anakuwa na uwezo mkubwa kitaaluma na kwamba akiamua kujifunza somo lolote anaweza kulimudu.

Alisema ufaulu ndogo kiini chake kikuu ni serikali kutowekeza katika sekta ya ajira, kwa lengo la kupata matokeo mazuri yaliyo ya kweli.

“Na ukienda mbali zaidi utabaini kuwa wengi wa wanaofaulu ni watoto wa wenye kipato cha juu na kati, wanaomudu kusomesha watoto wao kwenye shule binafsi, upo uwezekano mkubwa wa watoto wengi wa maskini kubaki bila elimu,” alieleza.

Lymo alisema hakushangazwa na kauli ya Waziri wa Elimu na Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa, iliyotaka wananchi watarajie matokeo mazuri zaidi katika matokeo ya kidato cha nne na kwamba hata hayo yatakuwa matokeo mazuri kwa wingi siyo kwa ubora.

HAKI ELIMU
Meneja wa Idara ya Utafiti na Uchambuzi wa Sera wa Taasisi ya Haki Elimu, Godfrey Boniventura, alisema katika miaka ya nyuma kiwango cha ufaulu kiliikuwa kinafika asilimia 80 hadi 85 tofauti na sasa wanafunzi wanapata matokeo yasiyoridhisha..

Alisema matokeo mabaya ya somo la Hisabati yamesababishwa na namna ya somo linavyofundishwa bila kuzingatia mbinu zinazofaa, kukosekana kwa mfumo madhubuti wa tathmini ya ufundishaji na ukaguzi huku akiitaka serikali kubadili mfumo wa ukaguzi kwenye shule.

Imeandikwa na Frank Monyo, Hussein Ndubikole, Kamili Mmbando, Dar na Edita Majura , Dodoma.

CHANZO: NIPASHE

Allahu Akbar. Mwenyezi Mingus amtangulie Hugh mtoto NA aweze kufanya vizuri zaidi katika ngazi ya sekondari. Aendelee kutia bidii katika masomo na kuzidisha heshima kwa waalimu. HONGERA SANA DOGO I HOPE YOU WILL STILL DO WELL.
 
RacheKiunsi-November7-2014.jpg

Mwanafunzi aliyefunika hisabati darasa la 7

Mwanafunzi bora wa somo la Hisabati katika mitihani ya taifa ya darasa la saba iliyofanyika nchini Septemba mwaka huu, Rachel Kiunsi (13).
Mwanafunzi bora wa somo la Hisabati katika mitihani ya taifa ya darasa la saba iliyofanyika nchini Septemba mwaka huu, Rachel Kiunsi (13), ameeleza siri ya mafanikio yake kuwa ni kujituma katika masomo na kuwaheshimu walimu.

Akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu jana kutoka mkoani Singida, Rachel ambaye alikuwa anasoma shule ya msingi Kimara 'B', jijini Dar es Salaam, alisema alikuwa na bidii ya kujituma katika masomo yake hasa katika la hisabati na ya Sayansi na kwamba alikuwa anashindwa kupata usingizi bila kujisomea usiku.

Akizungumzia jinsi alivyopokea taarifa za matokeo yake, Rachel alisema ni kwa furaha na alikuwa akitengemea kufaulu, lakini siyo kwa mafanikio kama hayo aliyoyapata.
“Nanamshukuru sana Mungu kwani nilikuwa namwomba atende maajabu katika matokeo yangu... nilikuwa nasali kila nikifanya mtihani na kumaliza,” alisema Rachel, ambaye alikuwa akiishi na bibi yake Kimara.

Aliwashukuru walimu wake wa masomo yote kwa juhudi za kuwafundisha vizuri wanafunzi wote katika shule hiyo kwani walikuwa wakiingia darasani kwa muda wa ziada na kutoka saa 11 jioni.

“Mimi nawashauri wanafunzi wenzangu tuliomaliza wote na kufaulu kuwa tuongeze bidii katika masomo yetu ya Sekondari kwani bila juhudi hatutaweza kufaulu kama tulivyofaulu sasa,” alisema.

Akielezea masomo anayoyapenda, Rachel, alisema kuwa ni ya Sayansi na ndoto zake zilikuwa ni kusoma katika shule ya sekondari ya vipaji maalumu ya wasichana ya Kilakala iliyopo mkoani Morogoro.

MAMA MZAZI AZUNGUMZA
Kwa upande wake, mama mzazi wa mwanafunzi huyo, Grace Kiunsi, akizungumza na NIPASHE kwa simu kutoka Singida, alisema matokeo ya mtoto wake aliyapata kwenye tovuti ya Baraza la Mitihani la Taifa (Nacte) na alifurahi, lakini hakufahamu kama ameongoza katika somo la Hisabati.

“Kusema ukweli nilipata furaha ya hali ya juu baada ya kuona matokeo ya mwanangu kuwa amefaulu kwa daraja la kwanza ‘A’, kwa masomo yote nilimpigia simu baba yake ambaye yupo masomoni katika Chuo cha Biblia Dodoma na kumweleza naye alifurahi sana,” alisema Kiunsi.

Alisema taarifa za kuwa mwanaye ameibuka kinara wa hisabati nchi nzima alizipata kupitia gazeti la NIPASHE ndipo furaha yake ilipozidi kwani hakufaulu kwa daraja la kwanza tu bali hata kitaifa.

Aliongeza kuwa mwanaye hakuna kitu anachopenda zaidi ya kusoma kwani kuna wakati mwingine alikuwa anashindwa kula au kulala kama hajamaliza kazi alizopewa na walimu wake shuleni.

“Rachel alikuwa ni mwenye heshima sana kwa walimu wake ilifika kipindi hata wazazi wake alikuwa hatutii kama anavyowatii walimu wake,” alisema Kiunsi.
Alisema hiyo ndiyo siri ya mafanikio ya mwanaye katika masomo yake, hivyo aliwaomba walimu wa shule aliyosoma Rachel kuongeza bidii kwani ndiyo zitakazoinua shule yao.

MWALIMU MKUU ASIMULIA

Naye Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Zuxine Mponda, alisema Rachel alikuwa ni mtoto wa kipekee katika shule yake kwani alikuwa ni mtiifu, msafi, mpole na msikivu kwa walimu wake.

Alisema walimu walikuwa wanategemea matokeo mazuri kwa wanafunzi wao kwani shule yake ina misingi mizuri ya kuaandaa wanafunzi kufaulu mitihani yote sio tu ya mwisho.

Alisema mwanafunzi huyo alikuwa akiongoza katika mitihani ya majaribio (moku), ya wilaya na mkoa na wastani aliokuwa akiupata ni wa 50 kwa 50 hasa katika Hisabati.

Mwalimu Mponda, alisema kuwa katika matokeo ya mtihani wa mwisho wa darasa la saba mwaka 2012 shule yake ilishika nafasi ya tatu kiwilaya na wanafunzi watatu walishinda kwenda katika shule ya Sekondari vipaji ya wanaume ya Ilboru.

Alisema wanafunzi waliomaliza darasa la saba katika shule yake mwaka huu ni 191 huku wasichana wakiwa 90 na wavulana 101.

Mpanda alisema wanafunzi waliopata alama ‘A’ katika somo la hisabati ni 37, Kingereza 13, Sayansi 12, Maarifa 16 na Kiswahili 16.

Aliongeza kuwa kutokana na ufaulu huo matokeo ya shule yake ni mazuri kwani wanafunzi waliopata daraja la kwanza ‘A’ katika masomo yote walikuwa watatu huku ‘A’ zikiwa ni 13 ‘B’ 76, ‘C’ 84, ‘D’ 18 huku hakuna mwanafunzi aliyepata alama ya F au E.

Aliongeza kuwa utamaduni wa shule hiyo kwa mwanafunzi yoyote aliyefanya vizuri ni kupewa zawadi hivyo wakapofanya kikao cha kamati ya shule watachagua zawadi ya kumpa mwanafuzi huyo.

Aliitaka Serikali kubadilisha utaratibu wa kulinganisha wastani kwa shule za Serikali na shule binafsi ili kumpata mwanafunzi bora au shule bora kwani mazingira ya ufundishaji ni tofauti .

MWALIMU WAKE AMWELEZEA
Naye mwalimu wa Hisabati shuleni hapo, Aron Mwinyi, alieleza siri ya mafanikio ya ufaulu huo kwa wanafunzi wake kwa kusema waliandaliwa vyema.

Alieleza kuwa shule hiyo ina utaratibu wa kuwaandaa wanafunzi toka awali na kuwajengea ukaribu ili wanapokuwa na tatizo masomo iwe rahisi kutatuliwa.

Alielezea sifa za Rachel na kusema kuwa alikuwa ni mwanafunzi makini tangu darasa la tano kwani alikuwa akiwasumbua walimu pale anapokuwa hajaelewa na hiyo ikamjengea uwezo wa kuongoza darasani katika kila somo.

“Katika shule yetu hapa hakuna tabia ya wanafunzi kujitenga kwa kujiona kuwa wanaakili sana, hapa wanafunzi wote ni sawa na wanafundishana na hiyo ndio sababu kuu ya ushindi huu kwa shule yetu,” alisema Mwinyi.

Mwinyi aliongeza kuwa walimu wanashirikiana katika ufundishaji kwani wakati mwanafunzi anakuwa na shida na mwalimu wake wa somo hayupo, mwanafunzi akimwona mwalimu yeyote anamsaidia.

Kwa upande wa mwalimu wa Kingereza, Privatus Mbehoma, alisema ni faraja kwa wanafunzi wao kufaulu masomo ya Kingereza na maarifa kwani ni masomo ambayo ufaulu wake ni mdogo lakini kwa shule yake wamefaulu kwa kiwango cha kuridhisha.

Juzi Katibu Mtendaji wa Necta, Dk. Charles Msonde, alitangaza matokeo ya mitihani ya darasa la saba uliofanyika Septemba mwaka huu huku wavulana wakiwa wameongoza na kanda ya ziwa ikitoa shule nane katika 10 bora.

Matokeo hayo yalionyesha kuwa watahimiwa wengi hawakufanya vizuri somo la Hisabati lenye ufaulu wa asilimia 37.56 huku somo la Kiswahili ufaulu wake ukiwa unaongoza kwa asilimia 69.70.

Katika Somo la Hisabati kati ya watahimiwa 34 waliopata 50 kwa 50 wasichana ni nane na wavulana ni 26.

UPINZANI WAKOSOA MATOKEO

Waziri kivuli wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Susan Lymo (Chadema), amesema ongezeko la ufaulu wa darasa la saba mwaka huu haufanani na halisi inayoonekana kwenye sekta ya elimu nchini.

Taarifa ya Necta) ilisema ufaulu umeongezeka kwa asilimia 6.38 ikilinganishwa na mwaka jana.

Lyimo alisema ili kutokea kiwango hicho cha ufaulu, sekta ya elimu ingeonekana kuwa na mabadiliko ya dhahiri tofauti na sasa ambapo kinachoshuhudiwa ni matamko, kama vile Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN).

Lymo ambaye kitaaluma ni mwalimu, alisema pamoja na hali hiyo, ufaulu hafifu unaoendelea kuonekana kwenye somo la Hisabati ni kiashiria
kikuu cha uwezo duni wa wahitimu.

Alisema mwanafunzi yeyote anayefaulu somo hilo anakuwa na uwezo mkubwa kitaaluma na kwamba akiamua kujifunza somo lolote anaweza kulimudu.

Alisema ufaulu ndogo kiini chake kikuu ni serikali kutowekeza katika sekta ya ajira, kwa lengo la kupata matokeo mazuri yaliyo ya kweli.

“Na ukienda mbali zaidi utabaini kuwa wengi wa wanaofaulu ni watoto wa wenye kipato cha juu na kati, wanaomudu kusomesha watoto wao kwenye shule binafsi, upo uwezekano mkubwa wa watoto wengi wa maskini kubaki bila elimu,” alieleza.

Lymo alisema hakushangazwa na kauli ya Waziri wa Elimu na Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa, iliyotaka wananchi watarajie matokeo mazuri zaidi katika matokeo ya kidato cha nne na kwamba hata hayo yatakuwa matokeo mazuri kwa wingi siyo kwa ubora.

HAKI ELIMU
Meneja wa Idara ya Utafiti na Uchambuzi wa Sera wa Taasisi ya Haki Elimu, Godfrey Boniventura, alisema katika miaka ya nyuma kiwango cha ufaulu kiliikuwa kinafika asilimia 80 hadi 85 tofauti na sasa wanafunzi wanapata matokeo yasiyoridhisha..

Alisema matokeo mabaya ya somo la Hisabati yamesababishwa na namna ya somo linavyofundishwa bila kuzingatia mbinu zinazofaa, kukosekana kwa mfumo madhubuti wa tathmini ya ufundishaji na ukaguzi huku akiitaka serikali kubadili mfumo wa ukaguzi kwenye shule.

Imeandikwa na Frank Monyo, Hussein Ndubikole, Kamili Mmbando, Mchungaji Mtikila Dar na Edita Majura , Dodoma.


Hongera ,MFUMO KRİSTO,Mbona waislamu sijawaona?
Hawa NECTA wanapendelea wakristo tu.
Waislamu tumekosea wapi?
İshauri wangu kwa BAKWATA:-Wapeni watoto elim dunia,hawa iran,saudi,syriA,boko haram ,al shabab,tunawashabikia lakini wao hawataki watu wasome,pia mtoto mara anakariri kiarabu,mara sjui anaiga kiswahili cha pemba eti ndo uislam?

Tutabaki ma hause boy & girls wa makafiri,tunawaoshea magari!

Ukienda maeneo ya mwnanyamala,kigogo,temeke, na kwengineko,hamna denti wa kiswahili anazidi form four!
Kwann azidi wakati kaanza kigodoro tangu lasaba?
Kila siku mara diamond mara omi dimpo,ooh wema sepetu!Kuda dadaki,Mi nabadiliaha dini nakuwa mlokole wanangu wafaulu na wawe watenda mema!
 
Back
Top Bottom