Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Waziri mkuu naye yumo anatafuta mtoto , wanajiaibisha sana hawa watu !Hili taifa wakati mwingine la kipumbavu sana..
Tunapotezeana muda kwa upumbavu kabisa. Mtu kajiona kakua wala wazazi hana time nao kaenda kwa wanaume..taifa zima likuwe alerted .
The search finally has ended with fruitful results.. Mengine atayaongea mlengwa maana bado yuko haiHatimaye Ester Noah Mwanyiru mwanafunzi wa sekondari ya Pandahill aliyetoweka 18 May 2023 amepatikana.
Taarifa iliyotolewa na mama yake mzazi inaeleza amepatikana wilayani Mbalizi kwa mama fundi cherehani. Alibadili jina kuwa Erica na amekua akivaa Hijab inayofunika uso, na kuacha macho tu na hivyo kuwa ngumu kutambulika.
Chanzo cha kupatikana ni baada ya binti mmoja wa Mbalizi kusimuliwa kisa cha Ester na kudai amemuona kwa mama mmoja fundi cherehani. Leo asubuhi polisi wamevamia nyumba ya mama huyo na kumkuta Ester. Wote wawili wapo kituo cha Polisi Mbalizi kutoa maelezo.
#MyTake:
Simulizi ya kupotea kwa Ester na kupatikana kwake inaacha maswali mengi kuliko majibu.
1. Ester alitoroka shuleni baada ya kukutwa akifanya udanganyifu kwenye mtihani. Akachapwa viboko vitatu, kisha akapewa mtihani mwingine afanye. Lakini polisi walipoenda shuleni hakukua na mtihani wowote Ester aliofanya. Je mitihani yake ilienda wapi?
2. Shule ya Pandahill ina ukuta (fence) ya urefu wamita 3 na juu kuna nyaya za umeme. Inawezekanaje mtoto wa kike kuruka ukuta wa mita 3 wenye umeme?
3. Matron wa shule anasema Ester alitoroka na mwenzie mmoja na walikimbizwa hawakupatikana. Hata hivyo "rall call" ilipofanyika wanafunzi wote walikuwepo isipokua Ester tu. Je huyo aliyekimbia na Ester akiwa kwenye sare za shule ni nani?
4. Barua aliyoacha Ester alidai kuonewa na Mwalimu Jimmy, japo hakutaja uonevu huo. Kwanini hakwenda nyumbani kuwaeleza wazazi badala ya kukimbilia Mbalizi?
5. Kwanini Headmaster alienda kwa wazazi wa Ester kutoa pole?
6. Huyo mama wa Mbalizi aliwezaje kumpokea binti asiyemfahamu na kukaa nae comfortably?
7. Aliishi kwa huyo mama kama nani? Housegirl au?
8. Inaelezwa alienda kwa huyo mama na Hijab. Aliipata wapi? Sare za shule alizototoka nazo aliziacha wapi?
9. Alibadili jina kuwa Erica lakini akavaa Hijab. Huyo mama hakujiuliza iweje mtoto wa Kikristo kuvaa Hijab?
10. Binti aliyetoa taarifa kuwa amemuona Ester Mbalizi alimtambuaje ikiwa alivaa Hijab ya kufunika uso na kubakiza macho tu?
NB: Tunamshukuru Mungu Ester amepatikana akiwa mzima, lakini kwa kuwa suala hili limepaziwa sauti na umma, basi ni vema umma ukapewa majibu ya kuridhisha.!
Msiongee sana , hawa hawachelewi kuzamisha meli au kudondosha treni wakafa watu bukunaona kila wakileta habari ya kuwatoa watz kwenye reli juu ya suala la waabaru wa dubai, wanadondokea pua.
Ndio lilikuwa donge?Huyo Binti aliyemgundua apewe milion 5 zake.
Umewaza mbali sana mkuunaona kila wakileta habari ya kuwatoa watz kwenye reli juu ya suala la waabaru wa dubai, wanadondokea pua.
Inatia hasira[emoji23]Eeeh ngumu kumezaaa ila kama chanzo ni dyudyuuuu alaaniwe huyu manzii...kutusumbua hivii mpaka wazirii mkuu alafu mwisho wa siku anaonekana kirahisii hivi
Usisubiri ipoe,hapahapa[emoji23]Mapema sana mkuu.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]naona kila wakileta habari ya kuwatoa watz kwenye reli juu ya suala la waabaru wa dubai, wanadondokea pua.
Ndiyo
NdiooooooHuyo Binti aliyemgundua apewe milion 5 zake.