Mwanafunzi Esther wa Panda Hill aliyepotea kwa siku 35 amepatikana, yadaiwa alitoroshwa na mchoma mkaa

Mwanafunzi Esther wa Panda Hill aliyepotea kwa siku 35 amepatikana, yadaiwa alitoroshwa na mchoma mkaa

Since day moko nilivyopata hii habari nikauliza umri wa bint nilivyoambiwa ni 19yrs halmashauri ya ubongo wangu ikaconclude huyu yupo mahali kafungiwa anafanya mchezo mbaya.
Nasisitiza wasisahau kumpima mimba.
Huyu hawezi pata mimba,coz ni konkodi,kutoroka si mara ya kwanza.
 
Mwamba aliyekua kamteka dogo aanze kusepa la sivyo miaka 30 kuna miaka 10 kusababisha taharuki na miaka 10 ya kumsumbua waziri mkuu !! Kiufupi huu ni Uhaini [emoji3][emoji3]
Hawezi kuwa mbeya hii tena , huyo asharuka viunzi vya Nakonde _ Tunduma anaitafuta kapirimposhi muda huu

Binti kupotea ? Shuleni ? Habari kwa bwana PM ? Subiri kwanza
 
Esther aliolewa KIMYA KIMYA WAZAZI WAKAMPIME MIMBA NA VVU NGOSWE ....PENZI KITOVU CHA UZEMBE WRITTEN BY EDWIN SEMZABA (R.I.P) PANDAHILL NISHULE YA KISHUA SANA KWA WALIO MBEYA WANAIJUA IYO SHULE NDIO
MAANA WANASEMA JUU NYAYA ZA UMEME BAIBIUI KALIPATA WAPI ?AIBU HII
 
Hatimaye Ester Noah Mwanyiru mwanafunzi wa sekondari ya Pandahill aliyetoweka 18 May 2023 amepatikana.

Taarifa iliyotolewa na mama yake mzazi inaeleza amepatikana wilayani Mbalizi kwa mama fundi cherehani. Alibadili jina kuwa Erica na amekua akivaa Hijab inayofunika uso, na kuacha macho tu na hivyo kuwa ngumu kutambulika.

Chanzo cha kupatikana ni baada ya binti mmoja wa Mbalizi kusimuliwa kisa cha Ester na kudai amemuona kwa mama mmoja fundi cherehani. Leo asubuhi polisi wamevamia nyumba ya mama huyo na kumkuta Ester. Wote wawili wapo kituo cha Polisi Mbalizi kutoa maelezo.

#MyTake:
Simulizi ya kupotea kwa Ester na kupatikana kwake inaacha maswali mengi kuliko majibu.

1. Ester alitoroka shuleni baada ya kukutwa akifanya udanganyifu kwenye mtihani. Akachapwa viboko vitatu, kisha akapewa mtihani mwingine afanye. Lakini polisi walipoenda shuleni hakukua na mtihani wowote Ester aliofanya. Je mitihani yake ilienda wapi?

2. Shule ya Pandahill ina ukuta (fence) ya urefu wamita 3 na juu kuna nyaya za umeme. Inawezekanaje mtoto wa kike kuruka ukuta wa mita 3 wenye umeme?

3. Matron wa shule anasema Ester alitoroka na mwenzie mmoja na walikimbizwa hawakupatikana. Hata hivyo "rall call" ilipofanyika wanafunzi wote walikuwepo isipokua Ester tu. Je huyo aliyekimbia na Ester akiwa kwenye sare za shule ni nani?

4. Barua aliyoacha Ester alidai kuonewa na Mwalimu Jimmy, japo hakutaja uonevu huo. Kwanini hakwenda nyumbani kuwaeleza wazazi badala ya kukimbilia Mbalizi?

5. Kwanini Headmaster alienda kwa wazazi wa Ester kutoa pole?

6. Huyo mama wa Mbalizi aliwezaje kumpokea binti asiyemfahamu na kukaa nae comfortably?

7. Aliishi kwa huyo mama kama nani? Housegirl au?

8. Inaelezwa alienda kwa huyo mama na Hijab. Aliipata wapi? Sare za shule alizototoka nazo aliziacha wapi?

9. Alibadili jina kuwa Erica lakini akavaa Hijab. Huyo mama hakujiuliza iweje mtoto wa Kikristo kuvaa Hijab?

10. Binti aliyetoa taarifa kuwa amemuona Ester Mbalizi alimtambuaje ikiwa alivaa Hijab ya kufunika uso na kubakiza macho tu?

NB: Tunamshukuru Mungu Ester amepatikana akiwa mzima, lakini kwa kuwa suala hili limepaziwa sauti na umma, basi ni vema umma ukapewa majibu ya kuridhisha.!
Maswali murua saana 🫱🏻‍🫲🏽🤜🏻💪🏻💪🏻💪🏻
 
😀😀 usikute dogo alienda kukalia, halafu amesumbua watu kinoma !! Mpaka hapo huyo dogo kuna vitu vingi anajua maana hii misheni sio ya mtoto mzembe mzembe !!
Waongee nae kwa upole ,
Halafu viongozi wetu bhana hizi mishe ndogo za hivi wapo makamanda mikoani huko wanatosha !!
Eti mpaka Waziri mkuu nae anatoa waraka 😀😀😀 halafu mtoto anakutwa kwa watu huko tena mkoa huo huo !!
Mambo makubwa makubwa ya upotevu wa Pesa wanainamisha vichwa ! Sema dogo nae kaweka historia " mimi niliwahi tafutwa hadi na waziri mkuu" mnajiaibisha
Makamanda ni hewa hadi wasukumwe.

Huyo dogo inaonyesha wamekulana sana na Jimmy.
Pili huyu sio dogo ni mtu mzima mwenzetu sio kwa hizi drama.

Mtoto mwema angeshtaki kwa wazazi
Screenshot_20230623-170719_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom