Mwanafunzi wa Upadri (Frateri) wa Kanisa Katoliki Shirika la Roho Mtakatifu Tanga anadaiwa kujinyonga hadi kufa

Mwanafunzi wa Upadri (Frateri) wa Kanisa Katoliki Shirika la Roho Mtakatifu Tanga anadaiwa kujinyonga hadi kufa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
GOGkQqgXkAA-pCN.jpg


Mwanafunzi wa Upadri (Frateri) wa Kanisa Katoliki Shirika la Roho Mtakatifu Jimbo la Tanga Rogassion Hugho anadaiwa kujinyonga hadi kufa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Mchunguzi amezungumza na JamiiForums na kusema “Ni kweli huyo Mwanafunzi wa Upadri amekutwa amejinyonga kwenye mazingira ya eneo wanalosoma (Magamba alipokuwa akiishi).

“Uchunguzi wa awali unaonesha chanzo ni kwamba alifeli masomo yake, akiwa ndiye Mwanafunzi pekee kati ya wote waliofanya mitihani.

“Alikuwa na umri wa Miaka 25 na kinachofanyika kwa sasa ni uchunguzi wa Jeshi la Polisi kuendelea ili kubaini kama kulikuwa kitu kingine kilichosababisha afanye maamuzi hayo.”

Amesema chanzo cha kujinyonga kwake kinadaiwa ni kufeli mtihani wake uliokuwa unampeleka kwenye Daraja la Upadri ambapo wenzake wote wamefaulu kasoro yeye.

Hivyo, kutokana na msongo wa mawazo ndiyo akafikia uamuzi huo wa kujinyonga,” amedai Kamanda Mchunguzi.

Amesema Polisi wanaendelea na uchunguzi wa kifo hicho na ukikamilika, taarifa kwa umma itatolewa.
 
Frateri wa Kanisa Katoliki Shirika la Roho Mtakatifu Jimboni Tanga, Rogassion Hugho, anadaiwa kujinyonga hadi kufa.

Hili ni tukio la pili kwa viongozi wa dini kudaiwa kujinyonga. Mei 16, 2024 mkoani Dodoma, Askofu Mkuu wa Makanisa ya Methodist, Joseph Bundala naye alidaiwa kujinyonga ndani ya ofisi yake iliyopo katika kanisa hilo eneo la Meriwa jijini Dodoma.

Akizungumza na Mwananchi kwa simu jana Jumatatu Mei 20, 2024 usiku, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Mchunguzi kuhusiana na kujinyonga kwa Frateli Hugho, amesema amekutwa amejinyonga kwenye nyumba yao ya Malezi ya Magamba aliyokuwa akiishi.

Hata hivyo, kamanda huyo amesema chanzo cha kujinyonga kwake kinadaiwa ni kufeli mtihani wake uliokuwa unampeleka kwenye daraja la upadri.

“Taarifa za awali tulizozipata zinadai sababu ya kujinyonga kwa mwanafunzi (Frateri) huyo, walikuwa na mitihani ya kuvuka kutoka ngazi moja, kwenda mwaka mwingine, sasa katika wenzake wote yeye peke yake ndio amefeli.

Hivyo kutokana na msongo wa mawazo ndiyo akafikia uamuzi huo wa kujinyonga,” amedai Kamanda Mchunguzi.

Amesema Polisi wanaendelea na uchunguzi wa kifo hicho na ukikamilika, taarifa kwa umma itatolewa.

Chanzo: Mwananchi

MK254, Moisemusajiografii , Mzee Kigogo na wale waisilaeli wa Buza sasa; yale mambo yetu: "hiiiiiiiiii...iii!"

Apumzike kwa amani Frateri ndugu katika kristo.
 
Back
Top Bottom