Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hapana yule hamli, wengi ndo wanajua hivyo,Najua na matibabu alimlipia...
Ila jamaa nae kala
Basi utachelewa sana, baba zako akina Cheni ndio wametoboa hivyo 😆😆Mi hawa mashangazi sijui kama nitawaweza yaani mi bila kuwa na hisia na mwanamke siwezi kufanya nae chochote na nikijilazimisha basi baada ya hapo ntaenda kuoga maji lita 300 au kama ni mashuka ya ghetto nitaamka niyafue hata kama ni usiku wa manane
Sasa lokolee aliyeshindwa kuendeleza biashara ya mazao, mtaji kutoka kwa mkuu wa mkoa mtumbuliwa lol.Huwa siaminiiiiii!
Kila nikiwaza picha haiji!
Ujue hadi Lokole naonaga kama anaonewa sometimes [emoji12] 🙄
Mimi niulize 80s kurudi nyumaAsante..
Naijua upanga nje ndani miaka ya late 80s to 90s.... from Tambaza village family, ..to upanga west
Gerezani, Kidongo chekundu, na enzi za wachizi wa Roller Boogie, Bibi Arafa Madras mtaa wa Lindi, Kibwiku family, lakini nilkuwa bado mdogo sana,.
Nyie wa zamani, haya mtupe archives.....
Jamaa kachokoza vita, hatoiweza asilani!Wewe Kiswahili umefundishwa kuandika kwa herufi za kilatino, ambazo hazijakamilika.
Mimi Kiswahili nimezaliwa nacho na nimeanza kukiandika kwa herufi zake za asili, za Kiarabu.
Jifunze kwangu kuandika Kiswahili.
Tobaaaaa! Kwahiyo sope kanyang'anywa tonge na kaka vishimo?Ucjekua wa kugombana na sope kisa boss, sope akaambiwa "sipo hapa kubishana nawee, utatoka ww mie utaniacha"
Watu na mashemu zao mjinii, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Ila pamoja na yote, lazima tuamini ule msemo wa wahenga!View attachment 2851623
Mafanikio ni mafanikio, haijalishi njia zilizotumika kuyafikia… mwisho yataitwa mafanikio bila kujali kama ni kwa njia halali au kupitia njia haramu.
Na daima mafanikio hutukuzwa, na waliofanikiwa hupewa heshima!
Muigizaji mkongwe, mfanyabiashara na mshereheshaji maarufu Mahsein Awadhi ‘Dr. Cheni’ yeye mafanikio yake yamepitia kwa mwanamke, ndio vijana huita mishangazi!
Si huwa wanasema mwanaume aliyefanikiwa nyuma yake kuna mwanamke? Ndivyo ilivyokuwa kwa Dr. Cheni… mwanamke aliyekuwa katika mafaniko yake sio mwanamke wa mchezo mchezo, ni mwanamke wa shoka kwelikweli!
Ukisikia mabalaa yake utabaki mdomo wazi, sio mwanamke, ni chuma!
NI SALMA MTAMBO!
View attachment 2851628
Bibie Salma Mtambo ni tapeli wa kupindukia. Akitapeli vijana kwa wazee, wanaume kwa wanawake.
Utapeli wa magari na kughushi nyaraka kwake ni jambo dogo na la kawaida kama kufumba na kufumbua macho!
Licha ya yote hayo, hakuna mkate mgumu mbele ya chai!
Bibie alikufa na kuoza kwa Dr. Cheni! Nini hakumpa Dr. Cheni? Mapenzi alimpa na mtaji wa biashara ya magari ambayo imemtajirisha sana Dr. Cheni alimpa yeye!
Kifedha na kwa kumpa baadhi ya magari yake mengi yaliyopatikana katika utapeli wake aanzie biashara hiyo.
Licha ya tofauti kubwa iliyokuwepo baina yao kiumri, haikuweza kuzuia mapenzi hayo mazito baina yao.
Kila mmoja akinufaika kwa namna yake, kimapenzi na kifedha!
Mapenzi yao yalikuwa mazito na yaliyojaa kufuru ya hela kutokana na utajiri wa kupindukia wa Salma!
ZA MWIZI AROBAINI…
Hakuna marefu yasiyo na ncha! Penzi la Dr. Cheni na ‘rich auntie’ Salma liliingia mdudu mara baada ya mfululizo wa kesi zilizomuandama Salma kutokana na ‘mission’ zake zilizomuweka mjini na kumpa heshima kubwa kutokana na ukwasi aliokuwa akiumiliki.
Ifahamike kwamba, utapeli wa Salma ulianzia miaka ya 90! Hivyo alikuwa na ‘Misala’ kibao!
Tamati ilifikia September 18 mwaka 2019 alipohukumiwa miaka 99 jela baada ya kupatikana na hatia katika mashtaka 17 ikiwemo kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu!
SALMA ALIA GEREZANI!
Baada ya Salma kupewa hukumu hiyo Dr. Cheni alipotelea kusikojulikana na Salma! Hakuwahi kuonekana kokote wala kumtembelea gerezani!
Salma anaumia zaidi kwa kuona kijana aliyempenda kwa moyo wote na kumpa kila kitu ikiwemo kushiriki katika ujenzi wa jumba la kifahari la Dr. Cheni akimtelekeza wakati alipokumbwa na matatizo!
Lakini, kesi za Salma ni mbaya na ni hatari zaidi kwa mtu maarufu na sasa mfanyabiashara mkubwa kujihusisha nae moja kwa moja.
Pengine ndio maana Dr. Cheni ameamua ‘kula kona’.
Lakini, kama ilivyo ada ya muosha huoshwa na mshahara wa dhambi ni mauti… ndiyo yanayomsibu Salma!
Ni yuleyule ripota kutokea JF mwenye chanzo chake nyeti…
Nawatakia sikukuu njema ya Krismasi,
Nifah
Nimeambatanisha baadhi ya nyaraka za kesi zilizokuwa zikimkabili Salma Mtambo.
La hawla wala quwatta.Basi Khadija Kopa alikukosha sana kwenye "Nalijua Jiji"
Haya wenye mji wenu Salma ndio huyo anatumikia kifungo kwa utapeli.
Huyu maza 2015 walikuja usukumani kwetu kule kampeni, TOT walifikia kwenye 'kigesti hausi' cha mzee. Alikuwa ana lala na vijamaa viwili, vijamaa vyenyewe ni viupinde kabisa.Basi Khadija Kopa alikukosha sana kwenye "Nalijua Jiji"
Haya wenye mji wenu Salma ndio huyo anatumikia kifungo kwa utapeli.
Hapana Nifah mi shabiki maandazi tu kuku mwenye kamba mguuni sijui A wala BE nyie ndo wakongwe buana maana mna ubuyu wa babu issa hauoni ndaniWewe nae mpanaaaaa! Watu kumbe umbea mnaujua kutuzidi sisi wambea?
Hapanaa, sope anahisi dimp anatoka na boss, kumbe wale ni mashemeji.Tobaaaaa! Kwahiyo sope kanyang'anywa tonge na kaka vishimo?
Ah nyie jamaniiiii!
Katika watu niliwashangaa ni waliokuwa wananunua mazao kwake, na kashfa zile unakulaje?Sasa lokolee aliyeshindwa kuendeleza biashara ya mazao, mtaji kutoka kwa mkuu wa mkoa mtumbuliwa lol.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
MwnawaneNi Mc gani huyo mbona mafumbo yamekuwa mengi jamani?