Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 3,585
- 8,106
#Repost @wasafifm
——
Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Happyness Khalfan amekatwa mkono na mume wake Charles Peter kwa kosa la kukataa asisome ujumbe mfupi (SMS) kwenye simu yake mara baada ya kuchelewa kurudi nyumbani.
Tukio hilo limetokea mnamo tarehe Desemba 15, 2024 katika kata ya Mwendakulima halmashauri ya manispaa ya Kahama Mkoani Shinyanga.
Akizungumza na vyombo vya habari Kamanda wa Polisi Mkoani Shinyanga SACP. Janeth Magomi ametoa ufafanuzi juu ya tukio hilo na kusema kuwa jeshi la polisi linaendela na ufuatiliaji wa kitendo hicho cha kikatili huku wivu wa mapenzi ukitajwa kuwa chanzo cha mwanamke huyo kufanyiwa kitendo hicho.
Akisimulia kwa njia ya simu mhanga wa tukio la kukatwa mkono Bi. Happyness Khalfan amesema kabla ya kufanyiwa kitendo hicho hakukuwa na ugomvi wowote kati yake na mumewe isipokuwa mara tu alipochelewa kurudi nyumbani ndipo alichukuwa panga na kumkata sehemu ya mkono wa kushoto.
Aidha kamanda Magomi ametoa rai kwa watu kutoa taarifa kwenye Jeshi la Polisi kupitia madawati ya jinsia pindi wanapofanyiwa vitendo vya ukatili na si kuyafumbia macho.
Cc: @officialkimoco
#WasafiDigital
——
Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Happyness Khalfan amekatwa mkono na mume wake Charles Peter kwa kosa la kukataa asisome ujumbe mfupi (SMS) kwenye simu yake mara baada ya kuchelewa kurudi nyumbani.
Tukio hilo limetokea mnamo tarehe Desemba 15, 2024 katika kata ya Mwendakulima halmashauri ya manispaa ya Kahama Mkoani Shinyanga.
Akizungumza na vyombo vya habari Kamanda wa Polisi Mkoani Shinyanga SACP. Janeth Magomi ametoa ufafanuzi juu ya tukio hilo na kusema kuwa jeshi la polisi linaendela na ufuatiliaji wa kitendo hicho cha kikatili huku wivu wa mapenzi ukitajwa kuwa chanzo cha mwanamke huyo kufanyiwa kitendo hicho.
Akisimulia kwa njia ya simu mhanga wa tukio la kukatwa mkono Bi. Happyness Khalfan amesema kabla ya kufanyiwa kitendo hicho hakukuwa na ugomvi wowote kati yake na mumewe isipokuwa mara tu alipochelewa kurudi nyumbani ndipo alichukuwa panga na kumkata sehemu ya mkono wa kushoto.
Aidha kamanda Magomi ametoa rai kwa watu kutoa taarifa kwenye Jeshi la Polisi kupitia madawati ya jinsia pindi wanapofanyiwa vitendo vya ukatili na si kuyafumbia macho.
Cc: @officialkimoco
#WasafiDigital