Mwanamke mjamzito kupata kichefuchefu na kutapika: Chanzo na tiba yake

Mwanamke mjamzito kupata kichefuchefu na kutapika: Chanzo na tiba yake

Pole dada yangu, mimi ni mume na mke wangu alikuwa na matatizo kama hayo kwenye ujauzito wa mtoto wetu wa kwanza mpaka mimi mwenyewe nilikonda jinsi nilivyokuwa namuonea huruma. So I can feel your pain.

Tiba: Kula ginger biscuit, ginger tea na tafuna ginger yenyewe huko kutapika na kichefuchefu kitaisha. Tena anza sasa hivi usisubiri muda upite, halafu baada ya nusu saa tupe feedback. Hii ni tiba tosha ya hili tatizo na kesho kazini utarudi. Nawakalisha

Ubarikiwe kaka yangu asante
 
Tena wanaokushauri utowe mimba achana nao? hivi wenyewe mama zao wangetoa mimba wenyewe wangekuwepo? watu kila siku wanalilia watoto lakini hawapati lakini wewe Mungu aliyejujalia unaona ni kero kwako. Vumilia hiyo ni hali ya muda tu.

Asante dada
 
Pole dada yangu, mimi ni mume na mke wangu alikuwa na matatizo kama hayo kwenye ujauzito wa mtoto wetu wa kwanza mpaka mimi mwenyewe nilikonda jinsi nilivyokuwa namuonea huruma. So I can feel your pain.

Tiba: Kula ginger biscuit, ginger tea na tafuna ginger yenyewe huko kutapika na kichefuchefu kitaisha. Tena anza sasa hivi usisubiri muda upite, halafu baada ya nusu saa tupe feedback. Hii ni tiba tosha ya hili tatizo na kesho kazini utarudi. Nawakalisha

Ginger ndo nini mkuu?
 
Pole sana, hio kwa wengine kawaida. Vumilia kiasi cha miezi mitatu mpk minne itatulia. Na hata kama unatapika jitahidi na kula, tafuna ubani mkali wa mint kila mara itakusaidia. Na epukana na harufu ya vyakula au perfumes unochukia kwa sasa mana zinazidisha. Lkn si mbaya pia kama utaenda hospital kupata ushauri wa Dr au hata tiba
 
Kinachosababisha kutapika, huwa kuna kitu kamaa makohozi yanakaa kooni au kwenye mfuko wa chakula juu juu. Pia huwa kuna nyongo inakaa maeneo hayo hayo.

Ili chakula kikae lazima hivyo vitu viwili vitoke. Ukiamka asubuhi kabla hujala kitu, piga mswaki na kuupitisha kooni. Utatapika sana, tena sana. Pitisha hadi usikie koo lote ni safi, baaada ya hapo unaweza kula chochote na hutakaa utapike.

Kama ni kuchoma sindano ama dawa utakunywa ngapi? Ukijua utamu wa kukata kiuno jua na kubeba masahibu yake, ushakua hivyo si mtoto tena.

Kuna nyengine shoga hata ufanyeje hazikai sawa, utatapika hata mate yako unayoyameza. Mie ya mwanzo nliona kama roho inatoka kila mbinu nlimaliza. Hadi ikakaa sawa wenyewe. Ajabu wengine wala habari hawana
 
Mh..jf we siku imeanza tulivu ya alhamic..umeolewa?ebu jiulize mama yako angetoa mimba yako ungekuwa hapa leo..watu wanalilia watoto kila siku wewe unataka kutoa..kaa utulie lea hiyo mimba ni miezi 3 tu ya misukosuko yote yatakwisha..ukiona shida kunywa vitu vichachu..

Amekwambia HATAKI KUITOA!
 
Kazi na mtoto vyote muhimu ila mtoto ni muhimu zaidi kuliko kazi, jikaze mtoto wakike mimba sio ugonjwa ikishakomaa hayo yote yataisha
 
Kinachosababisha kutapika, huwa kuna kitu kamaa makohozi yanakaa kooni au kwenye mfuko wa chakula juu juu. Pia huwa kuna nyongo inakaa maeneo hayo hayo.

Ili chakula kikae lazima hivyo vitu viwili vitoke. Ukiamka asubuhi kabla hujala kitu, piga mswaki na kuupitisha kooni. Utatapika sana, tena sana. Pitisha hadi usikie koo lote ni safi, baaada ya hapo unaweza kula chochote na hutakaa utapike.

Kama ni kuchoma sindano ama dawa utakunywa ngapi? Ukijua utamu wa kukata kiuno jua na kubeba masahibu yake, ushakua hivyo si mtoto tena.

Si wote walipata mimba kwa kukata kiuno bana!

Backto the topic:
Halafu kuna mmoja yupo mtaa wa Samora ofisi fulani hivi, naye ana tatizo kama la mleta thread.
Naye ni mimba ya kwanza. Nafikiri atulie tu litakwisha taratibu.
 
Ginger ndo nini mkuu?


Tangawizi

ginger.jpg
 
pole dada ndio ukubwa huo, vumilia tu hiyo hali itakwisha baada ya muda.
 
Habari zenu

Wapendwa naujauzito wa mwezi na nusu,inanisumbua natapika sana yaani kula cwezi na nikila natapika.watu wananishauri nitoe kwani naweza poteza kazi kwa hali hiyo.jamani kuna tiba kwa hili tatizo.nisaidieni sipend kuitoa.

hawa watu ni wabaya sana tena kaa nao mbali hata wewe wanaweza kukwambia ujiue siku moja hawana mana hata kidogo.

kwanza watu wa umri gani hao wanawake wanaume? nimewaogopa sana.
 
Habari zenu

Wapendwa naujauzito wa mwezi na nusu,inanisumbua natapika sana yaani kula cwezi na nikila natapika.watu wananishauri nitoe kwani naweza poteza kazi kwa hali hiyo.jamani kuna tiba kwa hili tatizo.nisaidieni sipend kuitoa.

Usitoe hiyo ni kawaida ya mimba na wataalam wanasema mtu ambae anapata morning sickness basi ana low risk of miscarriage huanzia 8week na humaliza at 12-13 weeks of pregnancy at the second trimester utajiskia better my dear
 
Dada samahani kwa lugha chafu nitakayoitumia....

Hivi una akili timamu???

Yaan unathamini kazi kuliko ndoa yako na uzazi wako?? Wanawake wengine hawalali usiku kucha, wanapoteza pesa na muda kutafuta ujauzito wewe unataka utoe kisa kutapika???? Je kama ndiye mtoto pekee uliyepangiwa kumzaa itakuwaje?? Ndio wale wale wanaishia kwa waganga wakitafuta mchawi kumbe wamejichawia wao wenyewe!!!

Huo ni upepo tu utapita... Hao wanaokushauri utoe ni wanafiki, toa uone cha moto utakiona. Unadhani mimba ni lelemama eeh.... Kama hukuwa tayari kuolewa bora usingekubali kuolewa na kumpotezea kijana wa watu muda.

Ulidhani unaolewa kwenda kuwa pambo la nyumba ya huyo mwanaume?? Unadhani ukitoa hiyo mimba, afu ukaja kubeba nyingine hutopatwa hayo maswahibu??????

Nimekuchukia aiseeeee........

Ungekuwa mdogo wangu wallah ningekukana!!!!!!!

Duh ameongea points muhimu sana i hope atazinduka mana kama ana lepe la usingizi vile
 
Salaam wakuu,mke wangu ana ujauzito wa mwezi 1,lakini ana matatizo mawili yanayomsumbua sana,kichefuchefu muda wote hujisikia kutapika,mdomo kujaa mate muda wote,je kuna dawa yeyote kuzuia hali hii isiendelee?naomba msaada wa mawazo tafadhali.

Habari wana JF,

Mpenzi wangu ana mimba ya miezi mitatu. Tatizo mara nyingi asubuhi huwa anatapika hata kama hajala chochote na jioni pia huwa anatapika akionja chakula tu. Hii kitu inaniumiza sana, maana siku nyingine analala bila kula. Mwenye ujuzi anifahamishe, nini tatizo?
 
Pole sana Mkuu.


Japo kutapika kwa hali hiyo ni kawaida
kuna wengine huwa hivyo kwa muda tu.

Ila ngoja wenye uzoefu na aina ya dawa
ingawa hali hiyo itapita japo anakuwa
kila anachokula ni kutapita huleta hofu.
 
hiyo .ni hali ya kupita mkuu, ila ikizidi aende akamuone mganga ...
 
Salaam wakuu,mke wangu ana ujauzito wa mwezi 1,lakini ana matatizo mawili yanayomsumbua sana,kichefuchefu muda wote hujisikia kutapika,mdomo kujaa mate muda wote,je kuna dawa yeyote kuzuia hali hii isiendelee?naomba msaada wa mawazo tafadhali.

Mkuu hiyo hali ni kawaida kwa baadhi ya wanawake hasa kwenye first trimester ( kipindi cha miezi 3 ya kwanza ya mimba ) itakwisha au kwa wengine inaendelea kwa kipindi chote cha ujauzito ila anaweza kutumia vidonge vya Nosic kutwa mara 2 kwa siku 5 au vidonge vya Vomidoxin.
 
Back
Top Bottom