Mwanamke mjamzito kupata kichefuchefu na kutapika: Chanzo na tiba yake


Ubarikiwe kaka yangu asante
 
Tena wanaokushauri utowe mimba achana nao? hivi wenyewe mama zao wangetoa mimba wenyewe wangekuwepo? watu kila siku wanalilia watoto lakini hawapati lakini wewe Mungu aliyejujalia unaona ni kero kwako. Vumilia hiyo ni hali ya muda tu.

Asante dada
 

Ginger ndo nini mkuu?
 
Pole sana, hio kwa wengine kawaida. Vumilia kiasi cha miezi mitatu mpk minne itatulia. Na hata kama unatapika jitahidi na kula, tafuna ubani mkali wa mint kila mara itakusaidia. Na epukana na harufu ya vyakula au perfumes unochukia kwa sasa mana zinazidisha. Lkn si mbaya pia kama utaenda hospital kupata ushauri wa Dr au hata tiba
 

Kuna nyengine shoga hata ufanyeje hazikai sawa, utatapika hata mate yako unayoyameza. Mie ya mwanzo nliona kama roho inatoka kila mbinu nlimaliza. Hadi ikakaa sawa wenyewe. Ajabu wengine wala habari hawana
 

Amekwambia HATAKI KUITOA!
 
Kazi na mtoto vyote muhimu ila mtoto ni muhimu zaidi kuliko kazi, jikaze mtoto wakike mimba sio ugonjwa ikishakomaa hayo yote yataisha
 

Si wote walipata mimba kwa kukata kiuno bana!

Backto the topic:
Halafu kuna mmoja yupo mtaa wa Samora ofisi fulani hivi, naye ana tatizo kama la mleta thread.
Naye ni mimba ya kwanza. Nafikiri atulie tu litakwisha taratibu.
 
pole dada ndio ukubwa huo, vumilia tu hiyo hali itakwisha baada ya muda.
 
Habari zenu

Wapendwa naujauzito wa mwezi na nusu,inanisumbua natapika sana yaani kula cwezi na nikila natapika.watu wananishauri nitoe kwani naweza poteza kazi kwa hali hiyo.jamani kuna tiba kwa hili tatizo.nisaidieni sipend kuitoa.

hawa watu ni wabaya sana tena kaa nao mbali hata wewe wanaweza kukwambia ujiue siku moja hawana mana hata kidogo.

kwanza watu wa umri gani hao wanawake wanaume? nimewaogopa sana.
 
Habari zenu

Wapendwa naujauzito wa mwezi na nusu,inanisumbua natapika sana yaani kula cwezi na nikila natapika.watu wananishauri nitoe kwani naweza poteza kazi kwa hali hiyo.jamani kuna tiba kwa hili tatizo.nisaidieni sipend kuitoa.

Usitoe hiyo ni kawaida ya mimba na wataalam wanasema mtu ambae anapata morning sickness basi ana low risk of miscarriage huanzia 8week na humaliza at 12-13 weeks of pregnancy at the second trimester utajiskia better my dear
 

Duh ameongea points muhimu sana i hope atazinduka mana kama ana lepe la usingizi vile
 
Salaam wakuu,mke wangu ana ujauzito wa mwezi 1,lakini ana matatizo mawili yanayomsumbua sana,kichefuchefu muda wote hujisikia kutapika,mdomo kujaa mate muda wote,je kuna dawa yeyote kuzuia hali hii isiendelee?naomba msaada wa mawazo tafadhali.

 
Pole sana Mkuu.


Japo kutapika kwa hali hiyo ni kawaida
kuna wengine huwa hivyo kwa muda tu.

Ila ngoja wenye uzoefu na aina ya dawa
ingawa hali hiyo itapita japo anakuwa
kila anachokula ni kutapita huleta hofu.
 
hiyo .ni hali ya kupita mkuu, ila ikizidi aende akamuone mganga ...
 
Salaam wakuu,mke wangu ana ujauzito wa mwezi 1,lakini ana matatizo mawili yanayomsumbua sana,kichefuchefu muda wote hujisikia kutapika,mdomo kujaa mate muda wote,je kuna dawa yeyote kuzuia hali hii isiendelee?naomba msaada wa mawazo tafadhali.

Mkuu hiyo hali ni kawaida kwa baadhi ya wanawake hasa kwenye first trimester ( kipindi cha miezi 3 ya kwanza ya mimba ) itakwisha au kwa wengine inaendelea kwa kipindi chote cha ujauzito ila anaweza kutumia vidonge vya Nosic kutwa mara 2 kwa siku 5 au vidonge vya Vomidoxin.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…