Japo pia nina waswas kuwa yawezekana uliokota jini, fikiria vzur mazngira uliomkuta ucku wa saa tano, mtoto mzuri yupo tu, unamuuliza shda yake nn anabaki kukubetulia midomo tu. na ukaenda nae kwako kiurahic bila ht kubembeleza sn, je alitoka wap muda huo hadi kukaa hapo posta? we mwenyew hujui. Cha kushangaza mpk unazaa nae bado hujui lolote kuhusu yeye, yur not serious ure joking..
Habari za jioni wakuu,
Kuna vitu ambavyo unaweza kukutana navyo katika maisha yako ya kila siku na ukavihifadhi katika moyo wako na kufanya siri kubwa ambayo kamwe hutataka kumwambia mtu yoyote yule.
Katika maisha ambayo nimeishi hapo kabla ikiwa bado sijakutana na huyu mpenzi niliyenae sasa nilibahatika kuzaa na msichana mmoja aitwaye Sheila.
Alikuwa ni msichana ambaye nilikutana nae kibahati mbaya sana, nasema kibahati mbaya sana kwa kuwa mazingira tuliokutana yalikuwa ni mazingira ya msaada zaidi, baada ya kumkuta maeneo ya Posta Mpya saa tano za usiku akiwa amejiinamia.
Sikujua nikitu gani ambacho kilinisogeza pale lakini nilijikuta tayari nikiwa mbele yake huku nikionyesha roho ya ubinadamu ikiwa ni pamoja na kuuliza ni lipi tatizo ambalo linamsibu.
Binti yule hakutaka kunijibu wala kunisikiliza alichokuwa anakifanya ilikuwa ni kunitazama tu na kunibinulia mdomo kwa dharau kubwa. Kusema kweli binti alikuwa ni mrembo sana na alikuwa anavutia sana.
Kijana nikaona nitangaze msaada huku moyoni nikiwa na mipango yangu mingine. Kweli baada ya vuta nikuvute binti akakubali kuondoka na mimi kuelekea Kigamboni ninakoishi huku akiweka angalizo la kutokumsumbua tukifika huko.
Mdomoni nikakubali lakini moyoni nilikuwa mbali sana, kifupi siku hiyo hiyo ndio siku ambayo tulifungua ukurasa wa penzi letu na tukawa kama kumbikumbi kila wakati tuko wote huku nikiwa sijui chochote kuhusu alikotoka na kwa wazazi wa huyu mwenzangu.
Ndani ya kipindi cha uhusiano wote mwenzangu akapata ujauzito ambao kila mmoja aliufurahia sana huku mapenzi yetu yakiongezeka maradufu.
Sasa kilichonifanya kuja hapa kwenu wanajamvi wenzangu ni kwamba licha ya kumhudumia kwa kila kitu kama mwenza wangu lakini baada ya kujifungua binti akanambia alichokuwa anakitaka ameshakipata hivyo nisimjue na nisimfuatilie tena.
Mwanzo niliona ni kama utani lakini baada ya siku chache akatoroka na mtoto mimi nikiwa kazini na hata niliporudi na kuwauliza majirani hawakuwa na jibu la maana.
Na hata namba zake za simu kila nikipiga hazipatikani tena lakini kuna siku nilitumiwa sms kwa namba ngeni akinipa hongera ya kumpatia mtoto.Lakini nilipoipiga haikupatikana na mpaka leo haipatikani.
Ombi langu kwenu wanajamvi wenzangu nifanyeje niweze kuipata damu yangu? Imefikia kipindi nahitaji kumuona mwanangu lakini sijui wapi nitampata huyu mwanamke.
Msaada wanajamvi wenzangu
Ulikutana na jini bro
Hahaa...Labda kama mimi siyo Yegomasika!. But It's all good buddy...Kupanga ni kuchagua!.
Sasa kwanini u quote mwenye uelewa mwembamba umeleta Uzi ulitaka usipate comment nyingine za tofauti. Au ulishaji creatia comments zako kichwani. Kwani hii ni hadithi kama nyingine based on imagination.wenye Uelewa Mpana Wamenishauri Vizuri na Nimewaelewa, Lakini Wachache Waliochini Ya Hapo Ndiyo Wanafikiri Hii Asali.... Mungu Anasimama na Mimi Kwenye Andishi Hili Mkuu...
Kamata like Kubwa mkuu like like like like like like like like like... Unakutana na mtu hamjafahamiana unamtongoza ndani ya Massa 5 umempa mimba kusa eti we ni rijali!!!????no thank you, hili ni nini kama story yake ni kweli again kula like like like!!!
naona kama story ya kutunga vile.
Anyway mwanaume mwenye akili timamu hawez okota mwanamke njian halafu anakwenda kumugeuza mke wake. Akifanya upuuzi kama huo matokeo yake ni kama haya.
Unaweza Kuwa na Akili Timamu na Hali Kama Iliyonikuta Mimi Ikakukuta na Ukafanya The Same Kama Mimi... Usiwe Mbishi Kwa Kuwa Haijakutokea Mkuu
Pole sana kwa kufanya hilo tukio ukiwa na akili timamu.
lazima uwe na malengo na msimamo ktk maisha kuwa unataka kuishi na mke wa namna gani. Usipokuwa na malengo na msimamo ndio kama hivi ukiona demu popote unamwambia twende tukaanze maisha. Utajiona mjanja kumbe mwanamke anakutega na ana malengo yake binafsi. matokeo yake ndio kama haya. hata hivyo una bahati sana maana ulikuwa ktk hatari ya kuambukizwa magonjwa, kuuwawa, kushikwa na polisi, kuibiwa mali zako na mengine megi yanayoambatana na kulala nyumbani kwako na mwanamke usiyemjua. usirudie tena kosa kama hilo
sikushangai, maana wewe si mtu wa kwanza kukutwa na tatizo hili,
Kule Mwanza nilikutana na issue kama hii, kijana alikutana na msichana usiku barabarani na kumng'ang'ania waende nyumbani na kisha kuwa mpenzi kabisa.
Baadaye shida na matatizo mengi yaanza na yule binti hakuwa anataka kuondoka.
Lakini mwishowe ilibainika kuwa alikuwa amemwoa jini.
Usipende kukurupuka na kuwa na mahusiano kwa kwa mtu usiyemfahamu. na tena una bahati bora ameondoka, huenda yangekupata makubwa .