Mwanamke peke yake hawezi kumkuza mtoto wa kiume kuwa mwanaume

Mwanamke peke yake hawezi kumkuza mtoto wa kiume kuwa mwanaume

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
PAKA JIKE HAWEZI KUKUZA SIMBA DUME

Mwanamke pekee hawezi kumkuza mtoto wake wa kiume kwenye kizazi hiki kipya, hii haijalishi mwanamke kaelimik kiasi gani, cheo, pesa, n.k. itakuwa ni ngumu sana, ponea ya mtoto labda awe na wajomba, ndugu wa kiume, n.k wenye muda nae, pia watoto wengine wanabahatika kuwa na watu wa mitaani sahihi ambao hugeuka kuwa kama baba kimtindo, lakini bado nafasi ya baba ni nzito.

Baba ni muhimu sana katika malezi ya mtoto wa kiume, uwepo wake pekee ndani ya nyumba hauna uzito, baba inabidi awe na jukumu la kukuza watoto wa kiume waje wanaume na sio watu wa kiume.

DISCIPLINE:

Mtoto wa kiume humuona mama yake kama rafiki yake tu ambae hata wakikosana anajua kuna madhara kidogo sana, atafinywa finya labda au atakaripiwa tu, binafsi mama yangu hata anichape nilikuwa namatania "hakijaingia", rafiki yangu flani akianza kuchapwa alikuwa anavunja vunja kiboko.

kwa baba ni tofauti kabisa, mtoto akikosea halafu aambiwe amsubiri baba yake wamalizane anajua tayari mziki wake, sio lazima kipigo kama wengi wanavyodhani lakini hata baba akikaa na mtoto wake kumpa darasa huwa kuna kitu kizito sana kinachomfanya mtoto ajihisi kweli kakosea na atajisikia vibaya, kiukweli huwa yanakuwa ni maumivu.

binafsi baba alikuwa ananipa dozi ya viboko mara chache sana na hapo ni kwamba nimekuwa mtukutu sana, lakini yale maneno aliyokuwa akinihusia kwenye makosa niliyofanya yalikuwa mazito sana, kuna muda niliwahi kulala saa tisa usiku nawaza tu darasa chungu alilonipa bila hata kuinua kiboko.... hii hali inamwingizia sana displini mtoto kujua kutii sheria hata za mama yake.

KUKABILIANA NA MAISHA YA WANAUME

Hapa utake usitake maisha ya wanaume utakutana na wanaume wenzako wakorofi ama waonezi, baba atamfundisha mtoto jinsi ya ku deal na hizi hali aidha kujua kupigana, kuwa na marafiki wa kum back up, n.k. mama yake atakuwa anaenda kulalamika mtoto kapigwa ila mzee wake anamuonesha mbinu.


ELIMU YA KUJITEGEMEA

Baba anaweza kuwa mfugaji, mkulima, seremala, fundi ujenzi, fundi mabommba, n.k hapa anaweza kumfundisha mtoto wake haya mambo ili hata akiondoka kuwe na mtu wa kuweka ugali mezani kihalali, mtoto akikosa hizi mbinu kuna uwezekano mkubwa akaanza kukaba watu.

MASULINITY (TABIA ZA KIUME)

Uwepo wa baba pia unamfanya mtoto wa kiume aweze kukopi tabia kibao za kiume, mzee anaweza kuwa mpenzi wa kutazama kwenye tv mieleka na muvi za ngumi, hapa mtoto nae anajijenga taia za ujasiri, kupenda mazoezi , n.k. hata pale mtoto anapoona mzee ana upinde ama rungu chumbani kwake hii inamfanya ajue mapema kwamba baba ndie mlinzi wa familia,

mtoto akikaa sana na mama yake si ajabu anaweza kuanza kupenda taarab, kujipiga make up, n.k,

INAENDELEA.............
 
PAKA JIKE HAWEZI KUKUZA SIMBA DUME

Mwanamke pekee hawezi kumkuza mtoto wake wa kiume, hii haijalishi mwanamke kaelimik kiasi gani, cheo, pesa, n.k. bado hataweza.

DISCIPLINE:

Mtoto wa kiume humuona mama yake kama rafiki yake tu ambae hata wakikosana anajua kuna madhara kidogo sana, atafinywa finya labda au atakaripiwa tu, binafsi mama yangu hata anichape nilikuwa namatanis "hakijaingia"

kwa baba ni tofauti kabisa, mtoto akikosea halafu aambiwe atamalizana na baba yake, anajua tayari mziki wake, sio lazima kipigo kama wengi wanavyodhani lakini hata baba akikaa na mtoto wake kumpa darasa huwa kuna kitu kizito sana kinachomfanya mtoto ajihisi kweli kakosea na anajisikia vibaya moyoni.

binafsi baba alikuwa ananipiga mara chache sana na hapo ni kwamba nimekuwa mtukutu sana lakini yale maneno aliyokuwa akinihusia kwenye makosa niliyofanya yalikuwa mazito sana, kuna muda niliwahi kulala saa tisa usiku nawaza tu darasa chungu alilonipa bila hata kuinua kiboko.... hii hali inamwingizia sana displini mtoto kujua kutii sheria hata za mama yake.

KUKABILIANA NA MAISHA YA WANAUME

Hapa utake usitake maisha ya wanaume utakutana na wanaume wenzako wakorofi ama waonezi, baba atamfundisha mtoto jinsi ya ku deal na hizi hali aidha kujua kupigana, kuwa na marafiki wa kum back up, n.k. mama yake atakuwa anaenda kulalamika mtoto kapigwa ila mzee wake anamuonesha mbinu.

ELIMU YA KUJITEGEMEA

Baba anaweza kuwa seremala, fundi ujenzi, fundi mabommba, n.k hapa anaweza kumfundisha mtoto wake haya mambo ili hata akiondoka kuwe na mtu wa kuweka ugai mezani kihalali, mtoto akikosa hizi mbinu kuna uwezekano mkubwa akaanza kukaba watu.

INAENDELEA.............
Duu mkuu wakati Niko o level pale songea boy's Kuna mtoto wa mwalimu wetu alikuja ANALIA amepigwa huko alikokuwa anacheza babake kamwambia mama mpe chakula ale halafu akapigane wamepiga sababu ya njaa
 
Duu mkuu wakati Niko o level pale songea boy's Kuna mtoto wa mwalimu wetu alikuja ANALIA amepigwa huko alikokuwa anacheza babake kamwambia mama mpe chakula ale halafu akapigane wamepiga sababu ya njaa
hapo kina mama wengi watamwambia awe anakimbia akimuona huyo mtu ama wanaweza kuhamisha shule kabisa.

Hii ni mwiko kabisa kwa vidume, mbinu zipo kibao tu utaelekezwa kufanya ambush, kumchangia adui, kujifunza kurusha mateke na ngumi, n.k.

Binafsi kaka yangu alnanisimulia aliwahi kurudi nyumbani kapigwa na mwenzake sasa karudi ili awambie baba, mzee alimcharaza bakora 2 kwa uzembe maana huyo mwenzake aliempiga alikuwa mfupi zaidi yake, kesho yake bro alienda kutembeza kipigo heshima ikarudi.

mama sijui angefenyeje hii hali??
 
Ndyo baba wa kikaz hichi sabab single mother n weng na wanazid kuongezeka msitegemee malezi bora
watoto wa kike wengi wamejawa tamaa sana, wakilishwa tu chipsi wanafungulia mapaja watu ambao wamejuana nao masaa tu.
 
PAKA JIKE HAWEZI KUKUZA SIMBA DUME

Mwanamke pekee hawezi kumkuza mtoto wake wa kiume kwenye kizazi hiki kipya, hii haijalishi mwanamke kaelimik kiasi gani, cheo, pesa, n.k. itakuwa ni ngumu sana, ponea ya mtoto labda awe na wajomba, ndugu wa kiume, n.k wenye muda nae, pia watoto wengine wanabahatika kuwa na watu wa mitaani sahihi ambao hugeuka kuwa kama baba kimtindo, lakini bado nafasi ya baba ni nzito.

Baba ni muhimu sana katika malezi ya mtoto wa kiume, uwepo wake pekee ndani ya nyumba hauna uzito, baba inabidi awe na jukumu la kukuza watoto wa kiume waje wanaume na sio watu wa kiume.

DISCIPLINE:

Mtoto wa kiume humuona mama yake kama rafiki yake tu ambae hata wakikosana anajua kuna madhara kidogo sana, atafinywa finya labda au atakaripiwa tu, binafsi mama yangu hata anichape nilikuwa namatania "hakijaingia", rafiki yangu flani akianza kuchapwa alikuwa anavunja vunja kuboko.

kwa baba ni tofauti kabisa, mtoto akikosea halafu aambiwe atamalizana na baba yake, anajua tayari mziki wake, sio lazima kipigo kama wengi wanavyodhani lakini hata baba akikaa na mtoto wake kumpa darasa huwa kuna kitu kizito sana kinachomfanya mtoto ajihisi kweli kakosea na anajisikia vibaya moyoni.

binafsi baba alikuwa ananipiga mara chache sana na hapo ni kwamba nimekuwa mtukutu sana lakini yale maneno aliyokuwa akinihusia kwenye makosa niliyofanya yalikuwa mazito sana, kuna muda niliwahi kulala saa tisa usiku nawaza tu darasa chungu alilonipa bila hata kuinua kiboko.... hii hali inamwingizia sana displini mtoto kujua kutii sheria hata za mama yake.

KUKABILIANA NA MAISHA YA WANAUME

Hapa utake usitake maisha ya wanaume utakutana na wanaume wenzako wakorofi ama waonezi, baba atamfundisha mtoto jinsi ya ku deal na hizi hali aidha kujua kupigana, kuwa na marafiki wa kum back up, n.k. mama yake atakuwa anaenda kulalamika mtoto kapigwa ila mzee wake anamuonesha mbinu.


ELIMU YA KUJITEGEMEA

Baba anaweza kuwa mfugaji, mkulima, seremala, fundi ujenzi, fundi mabommba, n.k hapa anaweza kumfundisha mtoto wake haya mambo ili hata akiondoka kuwe na mtu wa kuweka ugali mezani kihalali, mtoto akikosa hizi mbinu kuna uwezekano mkubwa akaanza kukaba watu.

MASULINITY (TABIA ZA KIUME)

Uwepo wa baba pia unamfanya mtoto wa kiume aweze kukopi tabia kibao za kiume, mzee anaweza kuwa mpenzi wa kutazama kwenye tv mieleka na muvi za ngumi, hapa mtoto nae anajijenga taia za ujasiri, kupenda mazoezi , n.k. hata pale mtoto anapoona mzee ana upinde ama rungu chumbani kwake hii inamfanya ajue mapema kwamba baba ndie mlinzi wa familia,

mtoto akikaa sana na mama yake si ajabu anaweza kuanza kupenda taarab, kujipiga make up, n.k,

INAENDELEA.............
Nakubaliana na wewe hakika
 
Weka sifa zako za mwanamme ili sisi tuliolelewa na mama pekee tujipime vinginevyo Mods wafute huu uzi. Kuna watu wamelelewa na mama pekee na sisi tunaona wako vizuri kila idara na wanaweza kukukuzidi uliyelelewa na baba na mama
 
wapo watu wengi wamelelewa na mama zao wako fresh tu wanaishi bila shida.. issue ni mama mwenyewe anaweza kuwa kimeo, wapo pia wamelelewa na baba na mama lakini shida tu pia....wapo wamelelewa na baba pekee shida tu..

Jamii nzima inahusika kwenye malezi ya mtoto au watoto, shida inaanza pale jamii inayokuzunguka ikiwa na watu waovu...watu waovu wanaweza kuwepo shule, wanaweza kuwepo mtaani, kanisani na msikitini....
 
Weka sifa zako za mwanamme ili sisi tuliolelewa na mama pekee tujipime vinginevyo Mods wafute huu uzi. Kuna watu wamelelewa na mama pekee na sisi tunaona wako vizuri kila idara na wanaweza kukukuzidi uliyelelewa na baba na mama
Mkuu hukuwa hata na wajomba, baba mdogo, wazee wa ukoo na mtaa waliosaidia kukusimamia katika makuzi yako?
 
Ndio maana naogopa sana nizae mtoto ambae akaishi na mama ake maisha yake yote.
 
I finally understand for a woman isn't easy tryna raise a man ~ 2 pac
 
Wanaume waliolelewa na single parent yaani mama peke yake huwa wanapwaya sana kwenye ndoa..wanashindwa kutenganisha space ya Mama yake na space ya mke wake . Mama anageuka mshauri mkuu huku mke akitupwa pembeni.

Hawajiqmini when comes to family decision making, mama yake anageuka mwamuzi ya mambo mengi ya kiuchumi hasa hasa.

Wanawake wengi huishia kuvunja ndoa hizi maana wanaishi kwa shida bila uthamani wa ndoa.
 
Back
Top Bottom