TANZIA Mwanamuziki Mkongwe, Boniface Kikumbi Mwanza Mpango (King Kikii) amefariki dunia

Jabali la mziki limeanguka, pumzika kwa amani Mfalme Kikii
 
King Kikii aliishi uzeeni kwa kutegemea perfomance za jukwaani na siyo mirabaha ya kazi zake alizowahi kufanya ambazo zinachezwa sana.....

Ndugu, haya mashirika COSOTA, BASATA, TBC ni majinamizi kwa wasanii
Hayo mashirika si yameanzishwa juzi juzi tu. Wala hamna haja ya kulaumu
 
Mwanae wa kike ndiye mmiliki
Alihojiwa TBC akasema zile Bar hazimuhusu yeye na Familia yake hata kutumika Jina la Kitambaa Cheupe kwenye zile Bar yeye hanufaiki na chochote, mwisho wa kunukuu

Kwa hio sio za mtoto wake
 
Hawa watu walikuwa wanaimba nyimbo kuhusu maisha, ndio maana hata bongo fleva ilipokuja mwanzoni nayo ilikuwa na maudhui sana. Kulikuweko na party songs ila na story telling songs kuhusu maisha. Nyimbo za aina hii ni ngumu sana kuchuja.
 
Huenda 90% ya matibabu yake yaligharamiwa na mapato ya baa za kitambaa cheupe. Bintiye ndiye mkurugenzi wa zile Bar.
Mboni Mzee alikataa alipohojiwa na TBC au alikua anatuigizia? Alisema zile Bar hazimuhusu yeye na Familia yake yaan hawanufaiki kwa chochote kutokana na zile za Kitambaa Cheupe yaan haziwahusu, nyinyi haya mnayoyasema mmeyatoa wapi?
 
Alihojiwa TBC akasema zile Bar hazimuhusu yeye na Familia yake hata kutumika Jina la Kitambaa Cheupe kwenye zile Bar yeye hanufaiki na chochote, mwisho wa kunukuu

Kwa hio sio za mtoto wake
Yupo sahihi ila haliondoi ukweli kwamba biashara ni ya mtoto wake. Hakuna asiyejua kuwa mtoto wa kike ndiye humtunza baba yake uzeeni.
 
Yupo sahihi ila haliondoi ukweli kwamba biashara ni ya mtoto wake. Hakuna asiyejua kuwa mtoto wa kike ndiye humtunza baba yake uzeeni.
Sikia mkuu alihojiwa na TBC akiwa amelala kitandani walimfuata nyumbani kwake, wakamuuliza hilo swali zile Bar zinakuhusu wewe mboni zinatumia Jina la Wimbo wako? Mzee akasema zile Bar hazinihusu wala Familia yangu haihusiki na zile Bar na hakuna chochote tunachopata kutokana na kutumika Jina la Wimbo wangu wa Kitambaa Cheupe km Jina la Bar
 
Kwahio we unaamini hilo sababu yeye kasema? Halafu kila siku yule mwanae yupo site anasimamia ujenzi wa bar za kitambaa cheupe na juzi alifungua ya Mbagala? Ya Tabata iliungua akafungua upya na kisha kaongeza mbagala.
 
Kwahio we unaamini hilo sababu yeye kasema? Halafu kila siku yule mwanae yupo site anasimamia ujenzi wa bar za kitambaa cheupe na juzi alifungua ya Mbagala? Ya Tabata iliungua akafungua upya na kisha kaongeza mbagala.
Mimi najua Mzee Kingi mutu ya Mungu uongo dhambi km ingekua ni hivyo katuongepea atajua mwenyewe atakachojibu huko anakokwenda ila alijibu hivyo mbele ya camera za TBC 1

Ngoja niisake ile Video ogopa Mungu ogopa teknolojia nakuja kuiweka hapa uone anavyojibu
 
King Kiki binafsi anaweza akawa hanufaiki hilo sikatai ila kuniambia familia yake hainufaiki kabisa ni uongo mkubwa. Labda kama hio familia anayozungumzia haimuhusishi yule binti yake ambaye ndio anamiliki hio brand ya kitambaa cheupe.
 
King Kiki binafsi anaweza akawa hanufaiki hilo sikatai ila kuniambia familia yake hainufaiki kabisa ni uongo mkubwa. Labda kama hio familia anayozungumzia haimuhusishi yule binti yake ambaye ndio anamiliki hio brand ya kitambaa cheupe.
Sikiliza mkuu, nitasema kwa mara ya mwisho alisema yeye hausiki na Bar za Kitambaa Cheupe na Familia yake akiwemo yeye hawanufaiki na chochote ndio akaambiwa na mtangazaji aongee na watanzania akaanza kuomba msaada na kujielezea mbele ya camera kwa hio unataka kusema Mzee ametuongopea kabla hajafa?

Ngoja niifukue ile video huku nikuletee umsikie mwenyewe maana huamini ukiambiwa
 
Sawa mkuu
 
Wakati wa ujana wetu alitutumbuiza sana hasa alipohamia Safari Sound na kuanza kutoa ushindani mkubwa sana dhidi ya Marquiz chini ya mtindo wao wa Masantula. Enzi hizo kila jumapili Safari resort pale Kimara ilikuwa inajaa sana

Mungu alizae roho yake pema peponi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…