DOKEZO Mwanangu ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inazungushwa

DOKEZO Mwanangu ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inazungushwa

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Shida ya MADAKTARI MAKANJANJA, unaona kabisa mtoto ameshambiliwa mwili mpaka amedhurika, lakini unaandika CANCER kwenye ripoti! 🤓

Is cancer the cause or a co-existing condition? (which is not a causation).

Mtu akiwa na malaria mwilini, kisha akakakatwa panga akafa, utasema amekufa kwa malaria?

Hizi shule zinazofundisha hawa MAKANJANJA zimesajiliwa kweli kihalali au zinafundishaje?

Hawa ndio wanaotushindilia MACHANJO YENYE MERCURY kutoka Marekani.

Nakuagiza Dkt. Gwajima D ulifuatilie hili swala haraka sana na uwawajibishe wahusika kwa mujibu wa sheria, la sivyo nitakuja hapo ofisini kwako kwa namna ambayo hautaielewa.

Cc Lamomy & DR Mambo Jambo
Kabisa mkuu, huyu Dr anapaswa kuchunguzwa vyeti vyake na post mortem ifanyike upya.
 
Kama ripoti ya Daktari inaonesha mwanao alikuwa na Kansa ya Damu ( dalili zote unazoelezea zinaendana) kwanini unalazimisha ionekane Mwalimu ndio kamuua mwanao?

Kuchapwa viboko kungekuwa kunaua tungeshakufa wengi sana tuliosoma zamani. Mnataka kutengeneza kizazi gani cha watoto wasiochapwa?

Kwanini mnataka kuleta malezi ya Kizungu watoto wa Kitanzania wenye mazingira na tamaduni tofauti katika malezi na makuzi?

All in all may His Soul Rest in Eternal Peace. Amen. Kuendeleza hii kesi ni kumkosea Marehemu kwa kulazimisha kitu kisichokuwepo.
kupasuka bandama ni dalili ya cancer ya damu?
 
Hakuna mwalimu anayeweza kumpiga mtoto ngumi tena mtoto wa darasa la kwanza, huyo mtoto labda alipigana na wenzake au alipata ajali, uchunguzi wa kina ufanyike. Kuchelewa namba hakuwezi kumfanya mwalim ampigie mtoto ngumi ya tumboni.

Nimulize kitu hapa.

Siku hiyo adhabu ilipotekelezwa na huyo mwalimu kwa marehemu je ni wanafunzi wangapi walikuwa wamechelewa namba?

Hiyo ngumi alipigwa huyo marehem tu au walipigwa wanafunzi zaid ya huyo marehemu?

Hiyo adhabu ilitolewa katika mazingira gani? ili ushahidi uwe wa kina zaidi

Zaidi ya yote niseme kwamba, poleni sana wazaz, ndugu, jamaa na wote tulioguswa na msiba huu. Mungu amrehemu marehemu! Amina.
Katika michango yoote iliyotolewa katika thread hii, comment hii imetolewa na mtu mwenye akili tulivu, mwenye kutafakari mambo kwa kina na kifanisi sana.

Jamani hivi kweli mwalimu aweza kuadhibu mtoto kwa nguvu ya juu ya kadiri, eti mangumi?

Walimu watumie miongozo gani kulea watoto wetu mashuleni sasa?

Najiuliza nabakia njia panda.

Nadhani jambo hili lifanyiwe uchunguzi huru ili haki itendeke pasiwe na bias ya kumbeba yeyote.

Mkasa huu unaleta simanzi sana, lakini usichukuliwe kwa mihemko ama kiushabiki, hapana.

Natanguliza pole zangu za dhati kwa wafiwa pamoja na walimu pia.
 
Ndio haya aliyoyasema juzi Rais Samia yaani Kuna watu hawawajibiki kabisa mpaka wawajibishwe, huyo Wazir Gwajima mwenyewe Dada wa watu anasema amempigia simu mara mbili anamkazania arudi dawati la jinsia ambako wamempuuza sasa sijui wanataka mpaka Makonda apite ndio awasikilize watu wa namna hiyo?
Mm nahisi wakat mwingine huyu wazir Huwa anatafuta kiki tu aonekane ame respond kwa haraka mtandaoni ili Hali hatupati feedback kuhusu nini amemsaidia mlengwa
Kweli kabisa mkuu. Kwanza hii criminal offence lakini waziri anataka ipelekwe kwenye dawati la jinsia ili iweje? Kwani huu ni mgogoro wa ndoa? Hii moja kwa moja ni criminal case wala haina uhusiano wowote na masuala ya jinsia.

Nchi hii ina viongozi mbumbumbu sana. Mtu anaona kabisa mwananchi kakosea njia bado anasmsisitiza aende huko huko. Na inawezekana hata mkuu wa dawati alimshauri aende mahakamani lakini kwa kuwa waziri alimshauri amuone mtu wa dawati basi akawa amebaki njia panda.

Hili nitukio la ajabu sana kutendeka katika nchi inajidai kuzingatia haki za raia. Katika kesi kama hii haki iko wapi sasa?
 
Kama ripoti ya Daktari inaonesha mwanao alikuwa na Kansa ya Damu ( dalili zote unazoelezea zinaendana) kwanini unalazimisha ionekane Mwalimu ndio kamuua mwanao?

Kuchapwa viboko kungekuwa kunaua tungeshakufa wengi sana tuliosoma zamani. Mnataka kutengeneza kizazi gani cha watoto wasiochapwa?

Kwanini mnataka kuleta malezi ya Kizungu watoto wa Kitanzania wenye mazingira na tamaduni tofauti katika malezi na makuzi?

All in all may His Soul Rest in Eternal Peace. Amen. Kuendeleza hii kesi ni kumkosea Marehemu kwa kulazimisha kitu kisichokuwepo.
Ujinga ujinga tu. Wewe ulipigwa ngumi za bandama ulipokuwa drs la 1?
 
Nyie wenzetu mnaishi nchi Gani mwanamme mzima mwenye familia anabaka kitoto Cha miaka mi3 sembuse mwalimu kumpiga ngumi mtoto wa miaka 7?
Katika michango yoote iliyotolewa katika thread hii, comment hii imetolewa na mtu mwenye akili tulivu, mwenye kutafakari mambo kwa kina na kifanisi sana.

Jamani hivi kweli mwalimu aweza kuadhibu mtoto kwa nguvu ya juu ya kadiri, eti mangumi?

Walimu watumie miongozo gani kulea watoto wetu mashuleni sasa?

Najiuliza nabakia njia panda.

Nadhani jambo hili lifanyiwe uchunguzi huru ili haki itendeke pasiwe na bias ya kumbeba yeyote.

Mkasa huu unaleta simanzi sana, lakini usichukuliwe kwa mihemko ama kiushabiki, hapana.

Natanguliza pole zangu za dhati kwa wafiwa pamoja na walimu pia.
 
Tatizo sio limempata nani? Suala ni uhalisia wa jambo husika. Je, ungekuwa wewe ni huyo Mwalimu unapewa tuhuma zisizo na uhalisia na kuhukumiwa na jamii ungejisikiaje?
Umemchapa mtoto, kafa lazima ujieleze kilichotokea sio unafichwa fichwa kama mwali. Kama ulimchapa kwa weledi kwanini unafichwa fichwa? Unatetea ujinga ujinga tu.
 
Tafuta ndugu zako mkafanye fujo hapo shulen hakikisha iwe fujo mpka waandishi wa habari waje shule ifungwee kwa muda .. hapo tatizo lako litakuwa limesikika kikamilifu. Au chukua maiti ya mwanao beba mpka shule
 
Wewe Hakimu tuambie namna gani fimbo za Mwalimu zimemuua huyo mtoto na kumletea cancer ya damu?
Acha kutetea ujinga. Huyo mwalimu aliyemchapa anatakiwa aeleze ni nini kilitokea. Mtoto kafariki unatetea pasiwe na maelezo ya aliyemtandika?

Kansa ya damu hata kama alikuwa nayo inaua baada ya fimbo? Mtu mzima tu tena mzee wa miaka 90 mwenye magonjwa yote unayoyajua wewe ukimwingiza ndani kwako akafia huko na hukumgusa unawajibika kutoa maelezo, huyo mwalimu kwanini asijulikane akajieleza?
 

Naitwa Janeth Shayo, mkazi wa Uru, Moshi. Naomba unisaidie kupaza sauti mwanangu Jonathan Makanyaga (07) mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Mrupanga, ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inataka kupindishwa.

Tar.28/02/2024 mwanangu alienda shuleni akiwa mzima. Alipofika aliadhibiwa kwa kuchelewa "namba". Alipoingia darasani alianza kutokwa damu puani na mdomoni. Akarudishwa nyumbani. Nilipomkagua nikamkuta na majeraha yaliyovilia damu mgongoni, kwenye mbavu na mguuni.

Kesho yake nikaenda nae shuleni kutaka kuoneshwa mwalimu aliyemfanyia ukatili mwanangu. Lakini Mwalimu mkuu akaomba nibaki nje. Akaingia na mwanangu ofisi ya walimu na kumtaka amtambue Mwalimu aliyemuadhibu. Mwanangu akamtanbua. Mwalimu Mkuu akaniambia wameshamfahamu ni mwalimu wa "Field" hivyo atazungumza nae.

Wakanipa 20,000/= za matibabu. Nikampeleka mwanangu zahanati. Kesho yake akazidi kutoka damu, na kulalamikia maumivu sehemu za mbavu. Nikampeleka hospitali ya masista. Daktari akaniambia bandama imejeruhika ndio sababu ya kutoka damu mdomoni. Mtoto alidai pamoja na viboko alivyochapwa, Mwalimu pia alimpiga ngumi tumboni. Huenda ndiyo iliyopasua bandama.

Hali yake ilizidi kuwa mbaya tukapewa rufaa kwenda KCMC. Akatakiwa kufanyiwa upasuaji. Gharama 350,000/= lakini sikuwa nayo. Nikapiga simu shuleni wakasema tuombe afanyiwe halafu watalipa baadae. Hata hivyo kabla hajafanyiwa hali yake ikazidi kuzorota, akashindwa kupumua, akawekwa kwenye Oxygen. Akashindwa kula, akawekewa mpira wa chakula. Baada ya siku chache akafariki 😭.

Lakini ripoti ya hospitali inasema mwanangu amekufa kwa kansa ya damu. Kansa gani ya damu inayomuua mtoto kwa wiki mbili? Na kwanini hiyo kansa itokee baada ya kuadhibiwa shuleni? Kwanini Mwalimu aliyemuadhibu mwanangu anafichwa, na sipewi haki ya kumfahamu?

Nalazimishwa nichukue maiti nikazike lakini nimekataa. Nataka uchunguzi huru. Nimeenda dawati la jinsia kulalamika nikapuuzwa. Nimepiga simu kwa Waziri Dkt. Gwajima D akanipa namba ya mtu wa kunisaidia. Nilipopiga kumbe ni yuleyule Mkuu wa dawati la jinsia aliyenipuuza. Nikamrudia Gwajima akasema niwasiliane nae huyohuyo. Nimekosa pa kulilia haki ya mwanangu Jonathan
inauma sana asee Mungu akutie nguvu
 
Katika michango yoote iliyotolewa katika thread hii, comment hii imetolewa na mtu mwenye akili tulivu, mwenye kutafakari mambo kwa kina na kifanisi sana.

Jamani hivi kweli mwalimu aweza kuadhibu mtoto kwa nguvu ya juu ya kadiri, eti mangumi?

Walimu watumie miongozo gani kulea watoto wetu mashuleni sasa?

Najiuliza nabakia njia panda.

Nadhani jambo hili lifanyiwe uchunguzi huru ili haki itendeke pasiwe na bias ya kumbeba yeyote.

Mkasa huu unaleta simanzi sana, lakini usichukuliwe kwa mihemko ama kiushabiki, hapana.

Natanguliza pole zangu za dhati kwa wafiwa pamoja na walimu pia.
Mkuu inakuja akilini eti mtoto wa darasa la kwanza kachelewa namba then mwalim ampige ngumi? Hivi kweli? Hapa kuna vilivojificha watoto skuhz wanadanganya sana.

Ukute mtoto alipigana na wenzake au alipata kiajali flan kikampelekea kupata maumivu na majeraha yalompelekea kufa lakini aliogopa kusema ukweli kwa wazaz bas akamsukumizia mwalim aliyemuadhibu labda kwa ka kiboko kamoja au tuwili twa miguuni au mkononi
 

Naitwa Janeth Shayo, mkazi wa Uru, Moshi. Naomba unisaidie kupaza sauti mwanangu Jonathan Makanyaga (07) mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Mrupanga, ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inataka kupindishwa.

Tar.28/02/2024 mwanangu alienda shuleni akiwa mzima. Alipofika aliadhibiwa kwa kuchelewa "namba". Alipoingia darasani alianza kutokwa damu puani na mdomoni. Akarudishwa nyumbani. Nilipomkagua nikamkuta na majeraha yaliyovilia damu mgongoni, kwenye mbavu na mguuni.

Kesho yake nikaenda nae shuleni kutaka kuoneshwa mwalimu aliyemfanyia ukatili mwanangu. Lakini Mwalimu mkuu akaomba nibaki nje. Akaingia na mwanangu ofisi ya walimu na kumtaka amtambue Mwalimu aliyemuadhibu. Mwanangu akamtanbua. Mwalimu Mkuu akaniambia wameshamfahamu ni mwalimu wa "Field" hivyo atazungumza nae.

Wakanipa 20,000/= za matibabu. Nikampeleka mwanangu zahanati. Kesho yake akazidi kutoka damu, na kulalamikia maumivu sehemu za mbavu. Nikampeleka hospitali ya masista. Daktari akaniambia bandama imejeruhika ndio sababu ya kutoka damu mdomoni. Mtoto alidai pamoja na viboko alivyochapwa, Mwalimu pia alimpiga ngumi tumboni. Huenda ndiyo iliyopasua bandama.

Hali yake ilizidi kuwa mbaya tukapewa rufaa kwenda KCMC. Akatakiwa kufanyiwa upasuaji. Gharama 350,000/= lakini sikuwa nayo. Nikapiga simu shuleni wakasema tuombe afanyiwe halafu watalipa baadae. Hata hivyo kabla hajafanyiwa hali yake ikazidi kuzorota, akashindwa kupumua, akawekwa kwenye Oxygen. Akashindwa kula, akawekewa mpira wa chakula. Baada ya siku chache akafariki 😭.

Lakini ripoti ya hospitali inasema mwanangu amekufa kwa kansa ya damu. Kansa gani ya damu inayomuua mtoto kwa wiki mbili? Na kwanini hiyo kansa itokee baada ya kuadhibiwa shuleni? Kwanini Mwalimu aliyemuadhibu mwanangu anafichwa, na sipewi haki ya kumfahamu?

Nalazimishwa nichukue maiti nikazike lakini nimekataa. Nataka uchunguzi huru. Nimeenda dawati la jinsia kulalamika nikapuuzwa. Nimepiga simu kwa Waziri Dkt. Gwajima D akanipa namba ya mtu wa kunisaidia. Nilipopiga kumbe ni yuleyule Mkuu wa dawati la jinsia aliyenipuuza. Nikamrudia Gwajima akasema niwasiliane nae huyohuyo. Nimekosa pa kulilia haki ya mwanangu Jonathan
jaribu pia kwenda kufungua kesi kwenye vyombo vya usalama
 
Nyie wenzetu mnaishi nchi Gani mwanamme mzima mwenye familia anabaka kitoto Cha miaka mi3 sembuse mwalimu kumpiga ngumi mtoto wa miaka 7?
Swala la kubaka linasabbshwa na vitu tofaut kabsa na swala tunaloongelea hapa.

Obviously mwalim kumpiga ngum mtoto wa darasa ya kwanza ni swala fikirishi sana.

Lakini ukiambiwa mtu mzima kambaka mtoto wa miaka 10 utaenda Moja kwa moja kwenye maswala kama imani za kishirikina na matamanio ya mwili yaliyomshinda mtekelezaj wa kosa hilo.

Mwalim sawa kuna mambo ya hasira lakini sio kiasi cha kumpiga mtoto ngumi ya mbavu mpaka kumjeruhi bandana nakataa
 
Kama ripoti ya Daktari inaonesha mwanao alikuwa na Kansa ya Damu ( dalili zote unazoelezea zinaendana) kwanini unalazimisha ionekane Mwalimu ndio kamuua mwanao?

Kuchapwa viboko kungekuwa kunaua tungeshakufa wengi sana tuliosoma zamani. Mnataka kutengeneza kizazi gani cha watoto wasiochapwa?

Kwanini mnataka kuleta malezi ya Kizungu watoto wa Kitanzania wenye mazingira na tamaduni tofauti katika malezi na makuzi?

All in all may His Soul Rest in Eternal Peace. Amen. Kuendeleza hii kesi ni kumkosea Marehemu kwa kulazimisha kitu kisichokuwepo.
Ukweli
 
Back
Top Bottom