Mwanangu ana Sickle Cell, tiba yake nini?

Mwanangu ana Sickle Cell, tiba yake nini?

Binafsi naona kama wewe siyo mzazi wa huyo mtoto aidha unataka majibu umsaidie mtu. Kwa nini nashindwa kukuamini? Issue serious ya ugonjwa huwezi kuiletea mzaha kama hivi, yaani mtoto wako ana dalili za sickle cell umezijuaje? Maana yake una elimu au uelewa wa huo ugonjwa.

Mkeo kaenda kumpima mtoto akaambiwa ana sickle cell na unadai amekunyima majibu je! Akikupatia hayo majibu ya daktari una elimu ya kutosha kusoma na kuyaelewa hayo majibu? Kama elimu hiyo unayo na mtoto ni wako. Kwa nini hamkwenda wote na mkeo kumpima mtoto?

Ok tufanye mkeo hakwenda kumpima mtoto sickle cell alienda kumpima ugonjwa mwingine ikatokea akapewa na hayo majibu. Mtoto ni wako unaishi naye, unadai anakupenda na unaogopa kumpoteza Kwa nini hujamchukua wewe na kumpeleka hospital uhakikishe kwanza kama ana ugonjwa huo?

Yaani unakuja jf kutafuta kujua Sickle cell Ina tiba au hapana wakati hujampima mtoto na kupata majibu na ushauri wa daktari? Naona kama unaleta mzaha kwenye mambo serious..
 
Ndugu Panzi Mbishi kwanza tambua kuwa jina lako linaashiria nguvu,fuata ushauri wa kitabibu,usikubali kupotezwa na wanaoamini njia zisizo za tiba ya kisayansi,wapo baadhi wanakuwa na hali hiyo katika umri mdogo,ila wanapovuka umri huo wanakuwa sawa,japo wakati mwingine kuna gharama za kupata huduma za tiba hadi kuvuka umri wa utoto.
Wewe ni nabii, hata jina langu halisi linamaanisha nguvu

Asante mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole kuna ndugu ana ugonjwa huo ni ugonjwa wa kurithi wazazi huwa ni carrier wa vinassba vya ugonjwa,cha kuzingatia hakikisheni anahudhuria clinik za wagonjwa wa sikocell,matibabu yameboresha atakua na atatimiza ndoto cha msingi muwe karibu naye muepusheni na baridi kali ama joto kali pia wanashauriwa wanywe maji mengi ili damu iwe nyepesi kuepusha maumivu yatokanayo na damu kukwama kwenye vishipa vidogo.

All the best.
Asante sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili ni jambo sahihi kwa wakati usio sahihi!! Mama na mtoto obviously watahisi uko na unyanyapaaa!! Tumia hekima na busara katika wakati huu!!
Mkuu hili halitanitikisa, tayari nina bond na huyu dogo awe wangu asiwe wangu...nakapenda sana na kenyewe kananipenda, so hekima itaongoza zaidi, ntafuatilia afya yake iwavyo vyote ni wangu tu.

Siku mtu mwingine akitokea kumdai ndio hekima itakaa pembeni tugawane majengo[emoji28]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwenu hakuna vinasaba vya selimundu.

Kwa mkeo hakuna vinasaba vya selimundu.

Mtoto ana selimundu.????

Sitaki kuwaza ninagyowaza hapa.

Pole sana mkuu.
Usiogope mkuu hata hili la DNA nitafuatilia na ikibainika sio wangu najimilikisha.

Nilishavuka level ya kuumizwa na baadhi ya mambo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi naona kama wewe siyo mzazi wa huyo mtoto aidha unataka majibu umsaidie mtu. Kwa nini nashindwa kukuamini? Issue serious ya ugonjwa huwezi kuiletea mzaha kama hivi, yaani mtoto wako ana dalili za sickle cell umezijuaje? Maana yake una elimu au uelewa wa huo ugonjwa.

Mkeo kaenda kumpima mtoto akaambiwa ana sickle cell na unadai amekunyima majibu je! Akikupatia hayo majibu ya daktari una elimu ya kutosha kusoma na kuyaelewa hayo majibu? Kama elimu hiyo unayo na mtoto ni wako. Kwa nini hamkwenda wote na mkeo kumpima mtoto?

Ok tufanye mkeo hakwenda kumpima mtoto sickle cell alienda kumpima ugonjwa mwingine ikatokea akapewa na hayo majibu. Mtoto ni wako unaishi naye, unadai anakupenda na unaogopa kumpoteza Kwa nini hujamchukua wewe na kumpeleka hospital uhakikishe kwanza kama ana ugonjwa huo?

Yaani unakuja jf kutafuta kujua Sickle cell Ina tiba au hapana wakati hujampima mtoto na kupata majibu na ushauri wa daktari? Naona kama unaleta mzaha kwenye mambo serious..
Tulianza tiba mkoani kwangu akapewa rufaa kwenda mkoa mwingine, mimi ni muajiriwa so nikabaki kulijenga taifa pamoja na kuangalia familia.

Kwahiyo majibu alipewa rufaa ya mkoa mwingine, unaweza kuona ugumu wa kuhakikisha.

Napokea ushauri kama natakiwa kufunga safari nitafanya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu Salaam,

Niende moja kwa moja kwenye mada, nina binti yangu wa miaka minne. Hivi majuzi amebainika kuwa na sickle cell kusema kweli nimechanganyikiwa sababu nasikia ni ugonjwa usio na tiba.

Naomba kujua yafuatayo;
1. Ni kweli ugonjwa huu hauna tiba?
2. Kama si kweli, tiba yake ni ipi?
3. Kama hauna tiba nini hatima yake?

Nimenyongea kwa kweli[emoji27]

Sent using Jamii Forums mobile app

Habari!

Pole kwa yanayokuzunguka. Binafsi nayaona mambo mengi ambayo yanakuletea mtanzuko:

1: Hali isiyo na majibu halisi
2: Hali yenye majibu halisi

A: HALI ISIYO NA MAJIBU HALISI

Umeeleza vyema kuwa mkeo karudi na taarifa husika na wewe binafsi haujashuhudia.

Binafsi ninaona ni vyema kwanza kufanya ufatiliaji wa majibu husika ili uonane na mtaalamu wa afya na kupewa uhakika wa maelezo.

Hali uliyonayo na kwenda mbele zaidi ya kuhukumu inaweza kuleta pengo ndani ya familia na maisha kwa ujumla kwani:

1: Inajenga mtizamo wako ulivyo kwa mkeo pale kuna tatizo au kuhisiwa tatizo.
2: Inajenga mtizamo wako kwa mwanao pale kuna tatizo au kuhisiwa tatizo.

Vyema ujiridhishe, kwani kama ulivyooa mkeo bila kujua ana tatizo hilo, vivo hivyo unaweza usijitambue wewe au ndugu zako kuwa na urithi wa tatizo husika.

Pia, kwa kutokufahamu namna majibu yalivyopatikana inaleta pengo la taarifa, kwani hatujui huyu mtoto:

1: Ni mgonjwa kamili wa sickle cell/sickle cell disorder
2: Ana urithi tu wa sickle cell/traits

Ni vyema kujua aina ya kipimo na aina ya sickle cell.

Vipimo vyetu pia vina hali ya kukata rufaa, kwenda kipimo cha juu ili kutanabaisha haya.

Mfano: Kama umefanya sickling test basi ni vyema kwrnda kwenye electrophoresis.

B: HALI YENYE MAJIBU HALISI

Kama utapata maji halisi.
Tatizo hili halina tiba ya moja kwa moja kwa dawa bali kwa mtu kuhamishiwa ute ulioko kwenye mifupa ambao huusika kwenye kuzalisha damu. Na hii huitaji ndugu wa karibu ili kuwiana kwa karibu sana.

Wagonjwa wa sickle cell wamegawanyika kwenye makundi mawili.

1: Wagonjwa halisia/sickle cell disorder
2: Wagonjwa wenye urithi/trait

I: Wagonjwa halisia

Hawa huweza kutambuliwa kwa muonekano kwa wataalamu wa afya hasa wanapokuwa na umri mkubwa. Si rahisi kuwafahamu wakiwa wachanga, labda tu wanapooanza kuonyesha dalili zinazoendana na tatizo.

Hawa ni wale ambao ambao wanakuwa wamerithi matatizo ya sickle cell toka kwa wazazi wote wawili.

Kwa sasa, watoto hawa wanaishi vyema kutokana na uwepo wa kliniki na dawa za kwasaidia hivyo kupunguza shida zinazowapata na kukua vyema.

Hii inahusisha:

1: Kutambua aina ya ugonjwa
2: Kutoa ushauri kwa wazazi au walezi juu ya jinsi ya kuwaelewa, kuwalea vs kuwasaidia watu husika kwa tiba halisi na kwa yupi hasa kulingana na sayansi na teknolojia iliyopo.
3: Kupewa viinirishe saidizi kwa wahusika.
4: Kutoa dawa za kuwakinga na maambukizi.
5: Kutoa dawa za kuwapunguzia attack.


Wagonjwa hawa hawatakiwi kupata stress yoyote ikadumu ndani yao hasa:

1: Maambukizi ya ugonjwa
2: Kutokunywa maji ya kutosha
3: Kuwa sehemu yenye oksijeni kidogo
4: Nk.

II: Wagonjwa wenye urithi/traits

Hawa huishi maisha ya kawaida na huwezi kuwatambua kwa macho hata kwa wataalamu.

Wahusika huweza kupata msukosuko kidogo mara wapatapo stress ndani ya miili yao kama ilivyotajwa hapo juu lakini si kwa kiwango cha wale wagonjwa halisi. Pia hawahitaji kuwa kwenye kliniki za mara kwa mara.

NB: Hivyo, yote kwa yote ni haki ya mtoto husika kuendelea na maisha kama kawaida na hasa ukichukua hatua kulingana na hali halisi utakayokutana nayo kwa misingi tajwa hapo juu.
 
Back
Top Bottom