Panzi Mbishi
JF-Expert Member
- Mar 8, 2021
- 2,231
- 2,904
- Thread starter
- #61
Asante mkuu, karibu.Habari!
Pole kwa yanayokuzunguka. Binafsi nayaona mambo mengi ambayo yanakuletea mtanzuko:
1: Hali isiyo na majibu halisi
2: Hali yenye majibu halisi
A: HALI ISIYO NA MAJIBU HALISI
Umeeleza vyema kuwa mkeo karudi na taarifa husika na wewe binafsi haujashuhudia.
Binafsi ninaona ni vyema kwanza kufanya ufatiliaji wa majibu husika ili uonane na mtaalamu wa afya na kupewa uhakika wa maelezo.
Hali uliyonayo na kwenda mbele zaidi ya kuhukumu inaweza kuleta pengo ndani ya familia na maisha kwa ujumla kwani:
1: Inajenga mtizamo wako ulivyo kwa mkeo pale kuna tatizo au kuhisiwa tatizo.
2: Inajenga mtizamo wako kwa mwanao pale kuna tatizo au kuhisiwa tatizo.
Vyema ujiridhishe, kwani kama ulivyooa mkeo bila kujua ana tatizo hilo, vivo hivyo unaweza usijitambue wewe au ndugu zako kuwa na urithi wa tatizo husika.
Pia, kwa kutokufahamu namna majibu yalivyopatikana inaleta pengo la taarifa, kwani hatujui huyu mtoto:
1: Ni mgonjwa kamili wa sickle cell
2: Ana urithi tu wa sickle cell
Ni vyema kujua aina ya kipimo na aina ya sickle cell.
Vipimo vyetu pia vina hali ya kukata rufaa, kwenda kipimo cha juu ili kutanabaisha haya.
Mfano: Kama umefanya sickling test basi ni vyema kwrnda kwenye electrophoresis.
Nitarudi kwa B.
Sent using Jamii Forums mobile app