Mwanangu ana Sickle Cell, tiba yake nini?

Mwanangu ana Sickle Cell, tiba yake nini?

Habari!

Pole kwa yanayokuzunguka. Binafsi nayaona mambo mengi ambayo yanakuletea mtanzuko:

1: Hali isiyo na majibu halisi
2: Hali yenye majibu halisi

A: HALI ISIYO NA MAJIBU HALISI

Umeeleza vyema kuwa mkeo karudi na taarifa husika na wewe binafsi haujashuhudia.

Binafsi ninaona ni vyema kwanza kufanya ufatiliaji wa majibu husika ili uonane na mtaalamu wa afya na kupewa uhakika wa maelezo.

Hali uliyonayo na kwenda mbele zaidi ya kuhukumu inaweza kuleta pengo ndani ya familia na maisha kwa ujumla kwani:

1: Inajenga mtizamo wako ulivyo kwa mkeo pale kuna tatizo au kuhisiwa tatizo.
2: Inajenga mtizamo wako kwa mwanao pale kuna tatizo au kuhisiwa tatizo.

Vyema ujiridhishe, kwani kama ulivyooa mkeo bila kujua ana tatizo hilo, vivo hivyo unaweza usijitambue wewe au ndugu zako kuwa na urithi wa tatizo husika.

Pia, kwa kutokufahamu namna majibu yalivyopatikana inaleta pengo la taarifa, kwani hatujui huyu mtoto:

1: Ni mgonjwa kamili wa sickle cell
2: Ana urithi tu wa sickle cell

Ni vyema kujua aina ya kipimo na aina ya sickle cell.

Vipimo vyetu pia vina hali ya kukata rufaa, kwenda kipimo cha juu ili kutanabaisha haya.

Mfano: Kama umefanya sickling test basi ni vyema kwrnda kwenye electrophoresis.

Nitarudi kwa B.
Asante mkuu, karibu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu Salaam,

Niende moja kwa moja kwenye mada, nina binti yangu wa miaka minne. Hivi majuzi amebainika kuwa na sickle cell kusema kweli nimechanganyikiwa sababu nasikia ni ugonjwa usio na tiba.

Naomba kujua yafuatayo;
1. Ni kweli ugonjwa huu hauna tiba?
2. Kama si kweli, tiba yake ni ipi?
3. Kama hauna tiba nini hatima yake?

Nimenyongea kwa kweli[emoji27]

Sent using Jamii Forums mobile app
Bone marrow transplant, Benjamin Mkapa Hospital wanafanya kwa watoto wenye sickle cell.
 
Sickle Cell hauna Tiba maalumu ya kupona, na hii nikutokana na Maumbile mabaya ya cell nyekundu za Damu, kupelekea kugota kwenye mishipa ya Damu na nyinginezo uwa mwili uamua kuzivunja vunja hili kuondoa zilizo haribika... Sasa kitendo cha mwili wenyewe kuendelea kuzivunja vunja seli nyekundu ambazo ni mbovu, hivyo upelekea mtu kuishiwa Damu, kwa sababu asilimia kubwa ya chembe nyekundu za Damu zinakuwa ni mbovu basi mtu huyu upungukiwa Damu.

Mara nyingi kwa watu wa Sickle cell unatakiwa uwe unampima malaria mara kwa mara ukiona anaugua na kupata homa, kwa sababu shida yake ya malaria ukiongezea sickle cell inaweza kufanya ugonjwa kuwa mkubwa zaidi kwa sababu pia Malaria uenda nayo kushambulia sell nyekundu za Damu.

Mara nyingi hawa watoto, utibiwa maumivu ya mara kwa mara kwa kupewa dawa za kupunguza maumivu, kupewa vidonge vya folic acid kwa ajili ya kuongezea damu, upewa antibiotic kama Pen V kwa ajili kuzuia pneumonia na magonjwa mengine ya bacteria, pia kama kaishiwa Damu zaidi basi uwa wanaenda kuwekewa Damu, na kama kapata shida ya upumuaji basi oxygen uwa anaekewa ikiambatana na matibabu mengine madogo madogo. Nyumbani ajitahidi kunywa maji hili kupunguza msongamano wa seli nyekundu zilizogota kwenye mzunguko wa damu basi.

Mwisho, ni vyema kufuata ushauri wa Daktari zaidi kuliko humu mitandaoni kwa maana Daktari ndio atakuwa anaona hali ya mgonjwa, na matabibu ya wagonjwa wa Sickle cell uwa hayafanani, atatibiwa kulingana na Crisis (Hatua ya ugonjwa) aliyonayo. Hivyo ni vyema kumuona mtaalamu hili hajui mtoto yupo kwenye crisis gani na apewe matabibu yapi na dose hipi.
 
Ndio maana wanashauri kabla ya ndoa ni vyema kupima afya kwanza kuona kama kuna uwezekano wa kupata mtoto mwenye sickle cell au ugonjwa kama ule aliompata mtoto wa masood kipanya...DNA unaweza Pima lakini unaweza kuta still bado ni mwanao 100 percent ..make sure usiongeze mtoto wa pili bila kujua mwingiliano wako na mkeo kama ndio ulisababisha.
 
Kama biology naikumbuka vizuri ni kwamba siyo baba na mama mna ugonjwa ila mna hivyo vinasaba hivyo miongoni mwa watoto wenu kuna atakayepata vinasaba na kuna atakayepata ugonjwa kabisa.

Huyu mwenye vinasaba akikutana na mwenye vinasaba mwenzake basi na wenyewe watapata watoto wagonjwa au wenye vinasaba.

Kuhusu tiba sina cha kusema.
 
Wakuu Salaam,

Niende moja kwa moja kwenye mada, nina binti yangu wa miaka minne. Hivi majuzi amebainika kuwa na sickle cell kusema kweli nimechanganyikiwa sababu nasikia ni ugonjwa usio na tiba.

Naomba kujua yafuatayo;
1. Ni kweli ugonjwa huu hauna tiba?
2. Kama si kweli, tiba yake ni ipi?
3. Kama hauna tiba nini hatima yake?

Nimenyongea kwa kweli[emoji27]

Sent using Jamii Forums mobile app


Wanakuja wataalam, nilikuwa na rafiki yangu college na ugonjwa huu, zingatia sana maelekezo ya madaktari. Hakuwa mwangalifu alikuwa anateseka na kututesa sana, mbaya walokole hewa (Kuna walokole safi) wakawa wanafikiri ni mapepo.
 
Wakuu Salaam,

Niende moja kwa moja kwenye mada, nina binti yangu wa miaka minne. Hivi majuzi amebainika kuwa na sickle cell kusema kweli nimechanganyikiwa sababu nasikia ni ugonjwa usio na tiba.

Naomba kujua yafuatayo;
1. Ni kweli ugonjwa huu hauna tiba?
2. Kama si kweli, tiba yake ni ipi?
3. Kama hauna tiba nini hatima yake?

Nimenyongea kwa kweli[emoji27]

Sent using Jamii Forums mobile app
Inasikitisha sana kwa kweli.
 
Sickle Cell hauna Tiba maalumu ya kupona, na hii nikutokana na Maumbile mabaya ya cell nyekundu za Damu, kupelekea kugota kwenye mishipa ya Damu na nyinginezo uwa mwili uamua kuzivunja vunja hili kuondoa zilizo haribika... Sasa kitendo cha mwili wenyewe kuendelea kuzivunja vunja seli nyekundu ambazo ni mbovu, hivyo upelekea mtu kuishiwa Damu, kwa sababu asilimia kubwa ya chembe nyekundu za Damu zinakuwa ni mbovu basi mtu huyu upungukiwa Damu.

Mara nyingi kwa watu wa Sickle cell unatakiwa uwe unampima malaria mara kwa mara ukiona anaugua na kupata homa, kwa sababu shida yake ya malaria ukiongezea sickle cell inaweza kufanya ugonjwa kuwa mkubwa zaidi kwa sababu pia Malaria uenda nayo kushambulia sell nyekundu za Damu.

Mara nyingi hawa watoto, utibiwa maumivu ya mara kwa mara kwa kupewa dawa za kupunguza maumivu, kupewa vidonge vya folic acid kwa ajili ya kuongezea damu, upewa antibiotic kama Pen V kwa ajili kuzuia pneumonia na magonjwa mengine ya bacteria, pia kama kaishiwa Damu zaidi basi uwa wanaenda kuwekewa Damu, na kama kapata shida ya upumuaji basi oxygen uwa anaekewa ikiambatana na matibabu mengine madogo madogo. Nyumbani ajitahidi kunywa maji hili kupunguza msongamano wa seli nyekundu zilizogota kwenye mzunguko wa damu basi.

Mwisho, ni vyema kufuata ushauri wa Daktari zaidi kuliko humu mitandaoni kwa maana Daktari ndio atakuwa anaona hali ya mgonjwa, na matabibu ya wagonjwa wa Sickle cell uwa hayafanani, atatibiwa kulingana na Crisis (Hatua ya ugonjwa) aliyonayo. Hivyo ni vyema kumuona mtaalamu hili hajui mtoto yupo kwenye crisis gani na apewe matabibu yapi na dose hipi.
Maelezo yamejitosheleza bosi asante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio maana wanashauri kabla ya ndoa ni vyema kupima afya kwanza kuona kama kuna uwezekano wa kupata mtoto mwenye sickle cell au ugonjwa kama ule aliompata mtoto wa masood kipanya...DNA unaweza Pima lakini unaweza kuta still bado ni mwanao 100 percent ..make sure usiongeze mtoto wa pili bila kujua mwingiliano wako na mkeo kama ndio ulisababisha.
Asante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante mkuu, umetaja dalili zote vyema kinachonishangaza mama yake na mimi hatuna historia ya kiukoo kuwako kwa ugonjwa huu. Kwa sababu yeye ndiye aliyempeleka hospitali nikamuuliza mbona wote kwetu haupo akasema eti sisi ni carrier.

Mbaya zaidi sijaviona vipimo kwa macho, hata nikimdai document za majibu anadai hakupewa.

Mpaka napata mashaka. Ila dalili ni hizo

Sent using Jamii Forums mobile app
Mmh au ana baba mwingine isije kiwa si wako.


Nimewaza kwa sauti tu usije anza kuhukumu ila.
 
Relax

magonjwa mengi sana yaliyokuwa tishio miaka ya nyuma sasa hivi si tishio tena kwny Ulimwengu wetu kutokana na maendeleo kwny Technolojia na maendeleo ya tiba

Hata sisi wa zamani kidogo tuliopita shule shule na kupata ofisi za kuzugia miaka ya 1980s kendra 1990s tunepoteza marafiki na wafanyakazi wenzetu wengi kutokana na maradhi mengi ambayo leo yana ama Tiba au njia nyingine mfano Ukimwi

fuata maelekezo ya Wataalam na kujua namna ya kuishi na hilo tatizo,

Leonel Messi kama kumbukumbu zangu zipo sawa niliwahi kusikia alikuwa na tatizo hilo utotoni
Messi alikuwa na tatizo la ukuaji...(udumavu)
 
Nenda Benjamin Mkapa hospital-Dodoma nasikia wameanza kutoa huduma hiyo kwa watoto wadogo.
Usikate tamaa wala kuchanganyikiwa.
 
Wakuu Salaam,

Niende moja kwa moja kwenye mada, nina binti yangu wa miaka minne. Hivi majuzi amebainika kuwa na sickle cell kusema kweli nimechanganyikiwa sababu nasikia ni ugonjwa usio na tiba.

Naomba kujua yafuatayo;
1. Ni kweli ugonjwa huu hauna tiba?
2. Kama si kweli, tiba yake ni ipi?
3. Kama hauna tiba nini hatima yake?

Nimenyongea kwa kweli[emoji27]

Sent using Jamii Forums mobile app
Mungu ambaye ni muweza wa yote akutendee na kumtendea mwanao kwa kadiri ya mapenzi yako.Uwe na imani Mungu yupo.Amini kwamba hakuna jaribu lisilo na njia ya kupona
 
Asante mkuu, umetaja dalili zote vyema kinachonishangaza mama yake na mimi hatuna historia ya kiukoo kuwako kwa ugonjwa huu. Kwa sababu yeye ndiye aliyempeleka hospitali nikamuuliza mbona wote kwetu haupo akasema eti sisi ni carrier.

Mbaya zaidi sijaviona vipimo kwa macho, hata nikimdai document za majibu anadai hakupewa.

Mpaka napata mashaka. Ila dalili ni hizo

Sent using Jamii Forums mobile app
Mashaka Gani unapata jamaa angu
 
Ni ugonjwa wa kurithi/kuzaliwa nao, hakuna tiba; wapo jamaa zangu walizaliwa na hizo changamoto na kwa sasa wako kwenye miji yao na wameoa.
 
Back
Top Bottom