Mwanangu Makonda, umeichoka na kuikinai nafasi yako chamani?

Mwanangu Makonda, umeichoka na kuikinai nafasi yako chamani?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Jana nilikusikia na kukusikitikia sana. Jinsi unavyojikaanga kwa mafuta yako mwenyewe. Jinsi unavyoonesha kuchoka na kukinai nafasi uliyonayo kwasasa chamani. Pale ulipozungumzia kuhusu mdahalo na viongozi wa CHADEMA.

Ngoja nikusaidie kwakuwa nilikuwa kiongozi mwandamizi chamani kabla yako. Naujua msimamo wa CCM juu ya midahalo. Ni kwamba, CCM si mfuasi na wala mpenda midahalo. Hata wagombea wetu wa Urais tangu kuanza kwa vyama vingi hukwepa midahalo, isipokuwa Hayati Benjamin Mkapa.

Mdahalo si lelemama. Mdahalo si mchezo. Ni rahisi kuchanganya msimamo wa chama na hisia binafsi mdahaloni na kuharibu bila ya kutibu. Hata kutubu huwa tabu. Mdahalo na CHADEMA, chama kikuu cha upinzani ni kuwatangaza na kuwapa umaarufu.

CHADEMA watakuwa huru kusema kwa kukosoa kila lifanywalo na Serikali inayoundwa na CCM. Jazba inaweza kutokea; makosa ya kitakwimu yanaweza kutokea; usahaulifu unaweza kutokea; kujichanganya kunaweza kutokea na hivyo CCM huepuka midahalo baada ya kuyatazama mambo hayo na mengine kwa kina.

Mwanangu Makonda, acha kutafuta kiki zisizo na mpango. Midahalo inayohusisha CCM kama taasisi ilishapigwa marufuku. Mfuate Komredi Anamringi Macha, Kaimu Katibu Mkuu akuoneshe kumbukumbu nyeti za kichama kuhusu hilo.

Halafu, Mwenezi napaswa kusemezana na Mwenezi. Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti au Katibu Mkuu wa chama chochote cha siasa nchini si 'level' yako. Hautasifiwa na yeyote ukimtaja na kumtaka Mbowe au Lissu kwenye mdahalo. Ni kiki tu. Kama umechoka tuambie tuchukue hatua za kichama.

Mabadiliko ya sheria za uchaguzi yatanguliwe na mabadiliko ya katiba!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Burigi, Chato)
 
Chama cha Mapinduzi kinakwenda na wakati na siyo kushikilia ukale katika usasa. Kusema hivyo ni kama kukifanya chama cha Mapinduzi kubaki katika ukale. CCM Ni chama ambacho kinakwenda na wakati na mahitaji ya wakati. Hii ndio sababu ya kuendelea kuungwa mkono na kukubalika na watanzania wa rika zote . CCM Ndio maana huja na watu au viongozi katika nafsi mbalimbali za uongozi watakaokwenda na kukidhi mahitaji ya wakati huo. Mheshimiwa Makonda amekuja kwa wakati sahihi na mahitaji ya wakati. Yupo tayari kwa mdahalo kwa sababu uwezo na hoja anazo na wala hana wasiwasi. na kila mtanzania anafahamu uwezo mkubwa alio nao Mh makonda.usimpe hofu wala uoga .wewe kama unaogopa basi usitake kuambukiza hofu yako na uoga wako kwa watu wengine.

Acha Mh akatuwakilishe kama chama. CCM siyo ya kuogopa midahalo bali vyama vya upinzani kama CHADEMA ndio vinapaswa kuihofia na kuiogopa CCM kutokana na kazi kubwa iliyofanywa katika kuwahudumia na kuwapelekea maendeleo watanzania. Acha hofu mzee wangu .jasiri na kiongozi shupavu huwa hawatii na kuwapa hofu anaowaongoza .huo ni udhaifu.na kama kweli ulikuwa kiongozi basi ulifaa kwa wakati wako lakini siyo kwa wakati huu wa sasa unaohitaji vijana jasiri na wenye uwezo wa kihoja kama alivyo Mheshimiwa Paul Makonda.
 
Jana nilikusikia na kukusikitikia sana. Jinsi unavyojikaanga kwa mafuta yako mwenyewe. Jinsi unavyoonesha kuchoka na kukinai nafasi uliyonayo kwasasa chamani. Pale ulipozungumzia kuhusu mdahalo na viongozi wa CHADEMA.

Ngoja nikusaidie kwakuwa nilikuwa kiongozi mwandamizi chamani kabla yako. Naujua msimamo wa CCM juu ya midahalo. Ni kwamba, CCM si mfuasi na wala mpenda midahalo. Hata wagombea wetu wa Urais tangu kuanza kwa vyama vingi hukwepa midahalo, isipokuwa Hayati Benjamin Mkapa.

Mdahalo si lelemama. Mdahalo si mchezo. Ni rahisi kuchanganya msimamo wa chama na hisia binafsi mdahaloni na kuharibu bila ya kutibu. Hata kutubu huwa tabu. Mdahalo na CHADEMA, chama kikuu cha upinzani ni kuwatangaza na kuwapa umaarufu.

CHADEMA watakuwa huru kusema kwa kukosoa kila lifanywalo na Serikali inayoundwa na CCM. Jazba inaweza kutokea; makosa ya kitakwimu yanaweza kutokea; usahaulifu unaweza kutokea; kujichanganya kunaweza kutokea na hivyo CCM huepuka midahalo baada ya kuyatazama mambo hayo na mengine kwa kina.

Mwanangu Makonda, acha kutafuta kiki zisizo na mpango. Midahalo inayohusisha CCM kama taasisi ilishapigwa marufuku. Mfuate Komredi Anamringi Macha, Kaimu Katibu Mkuu akuoneshe kumbukumbu nyeti za kichama kuhusu hilo.

Halafu, Mwenezi napaswa kusemezana na Mwenezi. Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti au Katibu Mkuu wa chama chochote cha siasa nchini si 'level' yako. Hautasifiwa na yeyote ukimtaja na kumtaka Mbowe au Lissu kwenye mdahalo. Ni kiki tu. Kama umechoka tuambie tuchukue hatua za kichama.

Mabadiliko ya sheria za uchaguzi yatanguliwe na mabadiliko ya katiba!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Burigi, Chato)
Sentence ya maana no Moja TU" mabadiliko ya Sheria za uchaguzi yatanguliwe na mabadiliko ya katiba"

Hayo mengine yanaeleweka!
Makonda yupo Kwa ajili ya waliomweka hapo,kukivuruga chama na kinaanza kuvurugka kweli kweli!
 
Chama cha Mapinduzi kinakwenda na wakati na siyo kushikilia ukale katika usasa. Kusema hivyo ni kama kukifanya chama cha Mapinduzi kubaki katika ukale. CCM Ni chama ambacho kinakwenda na wakati na mahitaji ya wakati. Hii ndio sababu ya kuendelea kuungwa mkono na kukubalika na watanzania wa rika zote . CCM Ndio maana huja na watu au viongozi katika nafsi mbalimbali za uongozi watakaokwenda na kukidhi mahitaji ya wakati huo. Mheshimiwa Makonda amekuja kwa wakati sahihi na mahitaji ya watati. Yupo tayari kwa mdahalo kwa sababu uwezo na hoja anazo na wala hana wasiwasi na kila mtanzania anafahamu uwezo mkubwa alio nao Mh makonda.usimpe hofu wala uoga .wewe kama unaogopa basi usitake kuambukiza hofu yako kwa watu wengine.

Acha Mh akatuwakilishe kama chama. CCM siyo ya kuogopa midahalo bali vyama vya upinzani kama CHADEMA ndio vinapaswa kuihofia na kuiogopa CCM kutokana na kazi kubwa iliyofanya katika kuwahudumia na kuwapelekea maendeleo watanzania. Acha hofu mzee wangu .jasiri na kiongozi shupavu huwa hawatii hofu anaowaongoza .huo ni udhaifu.na kama kweli ulikuwa kiongozi basi ulifaa kwa wakati wako lakini siyo kwa wakati huu wa sasa unaohitaji vijana jasiri na wenye uwezo wa kihoja kama alivyo Mheshimiwa Paul Makonda.
Wewe unaweza fanya mdahalo na chadema!!?hata kikwete hawezi wewe unaweza!!?

Ukiulizwa sababu za kuhamishwa wamasai ngorongoro utajibu nini!!?
 
Wewe unaweza fanya mdahalo na chadema!!?hata kikwete hawezi wewe unaweza!!?

Ukiulizwa sababu za kuhamishwa wamasai ngorongoro utajibu nini!!?
Mimi naweza kufanya mdahalo na kamati kuu nzima ya CHADEMA iliyojiandaa kwa mwezi mzima na nikaikalisha na kuipa darasa na Elimu ya kutosha juu ya masuala mbalimbali ya kisiasa ,kijamii ,kiuchumi n.k.
 
Jana nilikusikia na kukusikitikia sana. Jinsi unavyojikaanga kwa mafuta yako mwenyewe. Jinsi unavyoonesha kuchoka na kukinai nafasi uliyonayo kwasasa chamani. Pale ulipozungumzia kuhusu mdahalo na viongozi wa CHADEMA.

Ngoja nikusaidie kwakuwa nilikuwa kiongozi mwandamizi chamani kabla yako. Naujua msimamo wa CCM juu ya midahalo. Ni kwamba, CCM si mfuasi na wala mpenda midahalo. Hata wagombea wetu wa Urais tangu kuanza kwa vyama vingi hukwepa midahalo, isipokuwa Hayati Benjamin Mkapa.

Mdahalo si lelemama. Mdahalo si mchezo. Ni rahisi kuchanganya msimamo wa chama na hisia binafsi mdahaloni na kuharibu bila ya kutibu. Hata kutubu huwa tabu. Mdahalo na CHADEMA, chama kikuu cha upinzani ni kuwatangaza na kuwapa umaarufu.

CHADEMA watakuwa huru kusema kwa kukosoa kila lifanywalo na Serikali inayoundwa na CCM. Jazba inaweza kutokea; makosa ya kitakwimu yanaweza kutokea; usahaulifu unaweza kutokea; kujichanganya kunaweza kutokea na hivyo CCM huepuka midahalo baada ya kuyatazama mambo hayo na mengine kwa kina.

Mwanangu Makonda, acha kutafuta kiki zisizo na mpango. Midahalo inayohusisha CCM kama taasisi ilishapigwa marufuku. Mfuate Komredi Anamringi Macha, Kaimu Katibu Mkuu akuoneshe kumbukumbu nyeti za kichama kuhusu hilo.

Halafu, Mwenezi napaswa kusemezana na Mwenezi. Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti au Katibu Mkuu wa chama chochote cha siasa nchini si 'level' yako. Hautasifiwa na yeyote ukimtaja na kumtaka Mbowe au Lissu kwenye mdahalo. Ni kiki tu. Kama umechoka tuambie tuchukue hatua za kichama.

Mabadiliko ya sheria za uchaguzi yatanguliwe na mabadiliko ya katiba!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Burigi, Chato)
Wasalimie huko Burigi
 
Back
Top Bottom