Mwanasheria Mkuu wa Serikali kaamua kujikalia kimya kuhusu suala la Bandari?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Nilitegemea Mwanasheria Mkuu wa Serikali ndio awe kinara wa kutetea Mkataba wa kumkabidhi Mwarabu bandari zetu, ila naona yuko kimya na hata Bungeni sidhani kama alisimama kutetea huu Mkataba.

Binafsi nahisi atakuwa yuko against, kilichomshinda ni kujiuzulu tu. Kama niko sahihi, basi wakati wowote anaweza kuondolewa kwenye hiyo nafasi.

Kwa mtazamo wangu, kumuondoa wakati huu, kutaibua maswali ukizingatia ukimya wake.

Tusubiri.
 
Huo mkataba kama unavyo semwa ndivyo ulivyo hata bush loya akisimama mahakamani na mwanasheria mkuu anashinda na mkataba unapigwa chini.

Niaibu sana kwa inchi yetu, sauti ya wengi ni sauti ya Mungu.
Watawala waisikie sauti ya Mungu.
 
Tulia aliamua kuwa mwana sheria mkuu wa serikali. Mteuliwa kawa bubu.
Wazenji walia amua kumuweka pembeni na kufanya kazi ya kuuza bandari wao wenyewe.
Ati mwana sheria wa viwanja vya ndege ndia kaandaa mikataba ya kuuza bandari za Tanganyika. Mambo ya kishenzi kabisa.
 
Majizi nyie kelele zenu hazitazuia chochote, watz wengi Samia tumemwamini tumempa baraka ashirikiane na mwarabu wa DP world kuongeza ufanisi wa bandari yetu iliyodumazwa na majizi.
 

Tukitoka TPA tunawapa TAA. Mtalia milio yote mwaka huu
 
Imekuwa ni show ya Mh. Tulia Ackson Mwansasu na Mh. Waziri Mbalawa hawa ndo mmoja ni Mwanasheria Mkuu na mwingine ni naibu Mwanasheria Mkuu wa serikali huyo mwingine ana kazi nyingi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…