Mwanasheria wa tiGO katika Organogram ya Kampuni ni mtu mdogo sana, hawezi kuwa na access na mifumo yote aliyoitaja

Mimi nataka kusema tu kuwa kama yule bwana ameajikita katika kumfunga mbowe bkashashindwa tayari ila Kama lengo Ni kuharibia kampuni ya tigo basi kaweza kwa asilimia sijui Ni ngapi ila kiukweli Ni nyingi mno!
 
Nadhani Kibatal ana2eza kufungua kesi dhidi ya Tigo kwa kutoa taarifa za mteja .Hata jamii forum ilikataa kutoa taarifa za watumiaji wake na kuibwaga seikali mahakamani
 
Hawa tigo hawafai Kuna kipindi walikua wanamtumia magufuli hadi SMS za kutongoana kwa viongozi siku moja magu akamwambia katibu mkuu, wewe unachati na mke wa mtu hadi saa nane usiku ujui Kama yupo na mumewe? Sasa nawaweka ofisi moja ili mkagombane vizuri.
 
Ujinga wake tu. Serikali haina pesa ya kuwapandikiza hao watu kila kona.
Hapana bwana, wapo radhi hela ya kuwalipa hao watu ipatikane hata kwa gharama ya kukosa madaktari wa kutosha nchini.
 
Huyo bwana kama hatafukuzwa kazi basi tutajua kabisa kwamba yuko hapo kimkakati kwa sababu kitendo alichokifanya kinahalalisha kabisa ufukuzwaji kazi.
 
Mwanasheria wa kampuni huwa ndiyo anakuwa katibu wa kampuni ( Company Secretary/ Corporate Counsel) au katibu wa bodi (Board Affairs Officer). Mwanasheria wa kampuni ni mkurugenzi pia, sasa hilo la wewe kusema mwanasheria wa kampuni ni mtu mdogo basi napata sana shida. Aidha TiGO ni kampuni la kizamani sana au wewe unachanganya mambo.
 
@Jerlamarel
 
Daaah nimeogopa Jana nilikuwa nachart na mke wa mtu, kupitia tigo chip huenda huyu Frank akamwambie mume wake , Jaman Fred aka Alfred usimwambie mumewe ntafungwa mie , la sivyo ntahamia Voda au Airtel au hallotel
Huwezi kufungwa kwa kuzini na mke wa mtu,kiongozi punguza pressure
 
Tigo wajanja. Waliamua kukaa pembeni ili baadae msala uwe wa mtu mmoja na sio watu wengi ambapo ni vigumu kampuni kujitoa. Huyo jamaaa wamemtoa kama sadaka baadae utasikia wamemfukuza ili jina la kampuni lisichafuke. Ni akili ndogo tu imetumika hapo.
Utawala wa JPM uliharibu sana nchi ila wenye akili walijua jinsi ya kudeal naye. Likija lolote kuhusu usiri wa taarifa za Mbowe hata kama jamhuri itashindwa kwenye kesi tigo bado wapo safe kwenye kusafisha jina kwa kitendo chao cha kuacha mtu mmoja kufanya kila kitu kuhusu hilo jambo. Tigo oyeeeee
 
Tigo kila mtu analake huko na wanatatua matatizo yote
 
Hatari tupu
 
Duuu, moja ya komenti zako chache sana zenye mashaka, iweje mwanasheria awe pia ni mkurugenzi, kwanza mkurugenzi maana yake nini? Mimi najua mwanasheria anahusika na mambo ya kisheria, tena ni mshauri wa mambo ya kisheria, ushauri wake unaweza ukapuuzwa na kampuni ikafanya contract.
 
Ruksa kunifikira chochote kile, lakini hoja yangu iko palepale. Mashirika makubwa au makampuni makubwa huwa yanakuwa na kurugenzi na idara (Directorates & Units) mbalimbali ndani yake. Hivyo huwa kunakuwa na mkurugenzi wa Fedha (Director of Finance), Mkurugenzi wa Rasilimali watu (Director of Human Resources), Kurugenzi ya Masoko (Director of Marketing) n.k. Inategemea shirika ni linahusika na kitu gani.

Hawa wakurugenzi wote hufanya kazi chini ya mkurugenzi-mtendaji-mkuu (Chief Executive Officer): Sasa taasisi kubwa na mashirika makubwa huweka kurugenzi ya sheria (Directorate of Legal Affairs/Corporate Counsel/ Office of Company Secretary). Mara nyingi mwanasheria wa kampuni huhesabiwa kama mkurugenzi wa sheria na katibu wa kampuni. Siku hizi hata kwenye mashirika makubwa ya kiserikali iko hivyo....

Ofisi yake huwa ni kurugenzi na ndiyo inashikilia muhuri wa kampuni, yeye ndiye mtunzi wa nyaraka zote za kampuni na yeye ndiyo mshauri mkuu wa mambo yote ya kisheria ya kampuni. Mwanasheria wa kampuni anaingia kwenye vikao vyote nyeti vya bodi ya wakurugenzi na yeye huwa ndiyo katibu. Nyaraka zote nyeti za kampuni au shirika ni lazima ziwe na saini yake.

Ninakwambia hivi kwasababu mimi nishashika nafasi za Corporate Counsel/Director of Corporate Affairs na Company Secretary, hivyo nafahamu fika kitu ninachokisema hapa. Japo una ruksa ya kuendelea kuamini unachokiamini mkuu.
 

Mkuu huwa naheshimu sana komenti zako...

Hilo neno mkurugenzi, kwa kampuni binafsi muda mwingine huwa linamaanisha mmiliki, badala ya kusema mkurugenzi wa idara, mimi naomba nitumie mkuu wa idara.

Ukishasema idara maana yake ni kitengo kinachohusisha watu zaidi ya mmoja, kama ni idara ya sheria, maana yake kuna wafanyakazi na wanasheria zaidi ya mmoja, kama alivyokiri Kapala maana ndicho tunachojadili, alisema kuna wanasheria watatu.. Maana yake ni kwamba sio kila mmoja ni mkuu wa idara.

Kwa hiyo mkuu ukisema mwanasheria wa kampuni ni mkurugenzi(mkuu wa idara), hiyo inaweza kuwa ni generalisation ya maksudi yenye lengo la ku mislead watu kwa malengo maalumu.

Kwa hii ishu tunayojadili, ni mashaka makubwa, kwamba jamaa yetu ndiye mwanasheria, ndiye mtu wa IT, ndiye katibu muhtasi(PS), Ndiye mkuu wa ya sheria, ndiye mtu wa miamala, barua inaletwa anaipokea yeye, ni mkuu wa idara ila hakuna mtu wa kupokea barua, anapokea yeye, anaifanyia kazi yeye, inasaini yeye na kila kitu yeye, na hadi anakuja mahakamani anaejua ni yeye tu, hana boss wa kumtaarifu wala menejimenti ya kutoa go ahead. Mambo yote ni yeye!

Anyway, unaweza ukawa sahihi mkuu ila mimi ndio sijaelewa!
Huwa naheshimu sana komenti zako.
 
Mkuu, hebu kila mtu abaki na anachokiamini.
 
Ukishakuwa chini ya Managing Director wewe tena siyo Director isipokuwa kwa sababu umbumbumbu umewajaa nyinyi watanzania wanaluita jina Director of corporate affairs.

Ni jina tu lakini wewe siyo director. The Compani Act imefafanua vizuri maana ya Director.

Wewe ni mnyapala wa wenzako.


 
Kwaheri tigo nawaacha kulinda usalama wangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…