KWELI Mwanaume anaweza kuonesha dalili za Ujauzito badala ya Mkewe

KWELI Mwanaume anaweza kuonesha dalili za Ujauzito badala ya Mkewe

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
MADAI
Mdau wa JamiiForums ametoa mkasa mmoja unaomhusisha mume wa rafiki yake wa kike aliyeanza kuonesha dalili za ujauzito kwenye ujauzito mchanga wa mkewe.

E47BFDD1-5E84-4AA0-8B07-7889ECEC23CD.jpeg

Mdau anaeleza kwamba shemeji yake huyu ilikuwa kila asubuhi anatapika njano, na homa za hapa na pale na kila alipoenda hospital Ugonjwa haukuonekana, ilifikia wakati mwanamme akawa hawezi kufanya shughuli zake kwa sababu ya kutapika sana.

Baada ya kupima ilikuja kugundulika kuwa mkewe alikuwa na ujauzito. Ikasemekena kwamba kuna nyakati fulani ujauzito anabeba mwanamke Ila mabadiliko na dalili za ujauzito anakuwa nazo mwanaume.

Jambo hili ni kweli au uzushi?
 
Tunachokijua
Jambo hili lina ukweli. Huitwa Couvade Syndrome au Sympathetic Pregnancy.

Hali hii huwafanya wanaume wapate dalili za ujauzito kama vile kutapika, homa za asubuhi, kiungulia, kichefuchefu pamoja na kukosa usingizi.

Sababu za kutokea kwa hali hii huwa hazipo wazi sana lakini wasiwasi au furaha ya kuwa baba huhusishwa sana na kutokea kwake. Pia, ndoa au mahusiano yaliyopitia kwenye kipindi kirefu cha changamoto ya kupata mtoto hutoa nafasi kubwa ya kutokea kwa hali hii.

Mambo Muhimu Kuyafahamu
  1. Hutokea zaidi kwenye ujauzito wa kwanza
  2. Ni hali ya kawaida
  3. Dalili zake huwa kubwa kwenye miezi 3 ya mwanzo
  4. Hakuna dawa ya kutibu tatizo hili
Kwa mujibu wa tafiti, hali hii huendelea kupungua kadri ujauzito unavyozidi kukua na huisha kabisa muda mchache baada ya kujifungua kwa mwanamke.
Inaweza kuwa kutapika kula vitu vichungu au vichachu au maumivu pia,

Mimi binafsi hii kitu ilinitokea kipindi wife ana mimba ya mtoto wetu wa kwanza

Kiuno kilianza kuniuma hasa wakati nikiwa nimelala kuamka inakuwa mtihani kwani yalikuwa maumivu kweli kweli,

Nilihangaika mpaka kutumia dawa ya U.T.I lakini sikupona nilitumia mpaka dawa za kienyeji lakini wapi,

Lakini baada ya mke wangu kujifungua haikupita hata wiki moja nikapona kabisaa sikuamini kuwa nimepona kwani nilikuwa nalalamika mpaka kwa wazazi kila wakati ndo wakanipatia dawa za asili na zili shindwa,

Je, kuna ukweli wowote kuhusu hili?
 
Back
Top Bottom