Mwanaume halisi sharti asulubike: Mwanaume hujifunza na kuimarika kupitia magumu ila Wanawake ni kinyume chake

Mwanaume halisi sharti asulubike: Mwanaume hujifunza na kuimarika kupitia magumu ila Wanawake ni kinyume chake

Suffering is just like training don't hate it,
Just see it on other side of the continuum since everything is duality and the same.
But that so called training shouldn't be a reason to love suffering either especially if there is a simpler alternative.
Screenshot_20240827_004558_Instagram.jpg
 
Muanzisha uzi ukipata fursa ya kupata mamilioni kwa kukaa ofisini ama kuhustle juani na kupata kima hicho hicho cha pesa, je utachagua kuhaha mitaani ili kudhihirisha uanaume wako?
 
Muanzisha uzi akipata fursa ya kupata mamilioni kwa kukaa ofisini ama kuhustle juani na kupata kima hicho hicho cha pesa, je atachagua kuhaha mitaani ili kudhihirisha uanaume wake?
Kupitia ugumu siyo jambo la kuchagua ila ni njia tunayoipitia
 
Kupitia ugumu siyo jambo la kuchagua ila ni njia tunayoipitia
Kama hakuna njia mbadala ndio utasema ni mapitio ila ukiwa na options huwezi ukasema lazima upitie huo ugumu ili tu kudhihirisha kuwa wewe ni mwanaume.
 
Mwanaume halisi hatakiwi kuonewa huruma wala kujionea huruma Kwa sababu Mwanaume makini na mzuri ni yule aliyepitia magumu " the best men suffer". Haipo haja ya kumwambia mwanaume maneno laini kama una nia thabiti ya kumsaidia kuwa bora.

Ikumbukwe Mwanaume hujifunza zaidi kupitia ugumu na kukataliwa " Men always learn through negativity". Ipo Kila haja ya kulifanyia hii utafiti ila Sina mashaka na ukweli kuwa wanaume wengi wanaoonekana imara na bora leo nyuma ya pazia hawajapitia njia rahisi.

Wapo walioachwa yatima, waliotupwa magerezani na waliokataliwa kiasi ambacho hata leo wakikumbuka hawaamini. Wapo waliodhalilika na kudhalilishwa kuliko Mimi na wewe tunavyojiona leo lakini magumu hayo waliyoyapitia ni kama ngazi tu ya kupanda juu.

Vitabu vitukufu vinatuonesha mifano mingi sana ya wanaume waliokuwa imara sana na waliopitia madhila ya kutisha sana. Changamoto na matatizo ni darasa moja zuri na muhimu sana Kwa mwanaume.

Yupo msanii aliyewahi kuimba na katika wimbo wake alisema "wanaume tumeumbwa mateso". Hakika ni kama alifahamu njia ya kumnoa mwanaume ni mateso na kuhangaika haswaa.

Kujionea huruma ni kujichelewesha kufikia uimara na ubora unaotakiwa. Kanuni za ulimwengu zinamtambua mwanaume imara kuwa ni yule aliyejifinza kupitia magumu. Magumu yanapokuja ni Ili kujifunza na siyo kukata tamaa na kuacha kuendelea.

Ni ukweli tupo tunaopita katika hali tete sana lakini bado siyo sababu ya kujionea huruma na kuridhika na hali. Bado safari inaendelea licha ya uwepo wa vituo vingi njiani. Changamoto tunazopitia ni vituo vidogovidogo tu na siyo kituo kikuu ndiyo maana tunapaswa kuendelea mbele tu.
Takataka
 
Sio wote huzaliwa kuteseka mkuu, ulichoandika kinatokea sana kwa wenye maisha magumu.
 
Sijamalizia kusoma ila ni upuuzi mtupu ulioandika.

Hakuna faraja kwenye maumivu. Hii ni kwa wanaume wote, kama kuna njia mbadala ya kufanikiwa ambayo ni halali na haina mateso ichukue. Hakuna ugangwe kwenye kusurubika.
Yesu mwenywe na mitume wake walisulubika....mtoa maada yupo sahihi labda Kama wewe hunawaho kupitia hiyo situation
 
Mwanaume halisi hatakiwi kuonewa huruma wala kujionea huruma Kwa sababu Mwanaume makini na mzuri ni yule aliyepitia magumu " the best men suffer". Haipo haja ya kumwambia mwanaume maneno laini kama una nia thabiti ya kumsaidia kuwa bora.

Ikumbukwe Mwanaume hujifunza zaidi kupitia ugumu na kukataliwa " Men always learn through negativity". Ipo Kila haja ya kulifanyia hii utafiti ila Sina mashaka na ukweli kuwa wanaume wengi wanaoonekana imara na bora leo nyuma ya pazia hawajapitia njia rahisi.

Wapo walioachwa yatima, waliotupwa magerezani na waliokataliwa kiasi ambacho hata leo wakikumbuka hawaamini. Wapo waliodhalilika na kudhalilishwa kuliko Mimi na wewe tunavyojiona leo lakini magumu hayo waliyoyapitia ni kama ngazi tu ya kupanda juu.

Vitabu vitukufu vinatuonesha mifano mingi sana ya wanaume waliokuwa imara sana na waliopitia madhila ya kutisha sana. Changamoto na matatizo ni darasa moja zuri na muhimu sana Kwa mwanaume.

Yupo msanii aliyewahi kuimba na katika wimbo wake alisema "wanaume tumeumbwa mateso". Hakika ni kama alifahamu njia ya kumnoa mwanaume ni mateso na kuhangaika haswaa.

Kujionea huruma ni kujichelewesha kufikia uimara na ubora unaotakiwa. Kanuni za ulimwengu zinamtambua mwanaume imara kuwa ni yule aliyejifinza kupitia magumu. Magumu yanapokuja ni Ili kujifunza na siyo kukata tamaa na kuacha kuendelea.

Ni ukweli tupo tunaopita katika hali tete sana lakini bado siyo sababu ya kujionea huruma na kuridhika na hali. Bado safari inaendelea licha ya uwepo wa vituo vingi njiani. Changamoto tunazopitia ni vituo vidogovidogo tu na siyo kituo kikuu ndiyo maana tunapaswa kuendelea mbele tu.
sure
 
Akili za mijitu yenye rangi nyeusi sijui huwa ina kasoro gani??!! There is nothing noble about suffering.
Quite the contrary, .
What is happiñess without suffering?
Is there a north without a south?
Have you ever seen a coin with only head and no tail?
Is there an up without a down?
Is there good without evil?
 
Quite the contrary, .
What is happiñess without suffering?
Is there a north without a south?
Have you ever seen a coin with only head and no tail?
Is there an up without a down?
Is there good without evil?
All those you have mentioned are just the same thing in different polarities.
Mambo ni Yale Yale hakuna mambo mawili
 
Ukiona ina maslahi yasiyo na madhara kisheria wala kimaadili piga pesa ndugu. Yani ubebe zege kwa vile tu umeaminishwa mwanaume kaumbiwa mateso. Bullshit.
Hayo maslahi unayaonavmarahidi yana ugumu wake pia ni suala la mtazamo wa mtu tu ugumu anautafsiri vipi.
 
Suffering is just like training don't hate it,
Just see it on other side of the continuum since everything is duality and the same.
I beg to differ, suffering is not training, is a result of decision, could worng or right or whatever
Training is based series of event, could be good or could be bad
 
Humu watu mnachanganya kuteseka na kupitia magumu au changamoto…Mleta mada kwa upande wangu nimemuelewa kua kupitia changamoto ndo kunamkomaza mwanaume kua mrume ndago….so hata hao akina Mo na Gsm kuna magumu na wao wanayapitia ndo maana wako hapo…ila nyie mnahis magumu ni kuuza maji ya sh 100 juani….Magumu na kuteseka kuko kwa Aina nyiiingi sana.
 
Back
Top Bottom