Mwanaume jenga utamaduni wa kurudi nyumbani na mfuko wa sokoni

Mwanaume jenga utamaduni wa kurudi nyumbani na mfuko wa sokoni

Unajitetea sana. Kama bado uko kwenye level za kuwaza kwenye friji kuna nini bado uko chini sana. Waza maendeleo sio hayo mambo madogo madogo. Kujaza friji mwachie mkeo
Sawa mkuu
Isijekuwa namuelewesha mtoto wa 2000 bure
Ila yote kwa yote haya ni maisha yangu na familia yangu
Nikiwa Baba wa familia ni muhimu kuhakikisha ndani chakula hakiishi

Muhimu familia hailali njaa basi

Kuhusu maendeleo mada haihusiani na maendeleo mada inahusiana na Baba kurudi nyumbani na mfuko wa sokoni
 
Naenda kazini na gari na gari la company halafu kwangu kutoka kituo ninachopandia ni mita zisizo zidi 300 halafu sokoni ni kama k1.5 kwahiyo nisiende nyumbani niende kunua chungwa km1.5 jumlisha mita 300=km1.8 nitakuwa na akili sawa sawa?

Mwanaume acha hela nyumbani atajua mwanamke atakcho nunua basi
 
Ukiwa umeoa / nyumbani una familia hakikisha kila unaporudi home unarudi na mfuko umejaa vitu vya sokoni.

Ukijenga huo utamaduni itakuongezea heshima kwenye nyumba yako hata kabla haujaingia ndani ya nyumba yako utaona mke au watoto wanakukimbilia kukupokea.
Kwa wale makapuku. Kama una gari na unanunua mahitaji kwa jumla hii ni aibu kwako.
 
Sawa mkuu
Isijekuwa namuelewesha mtoto wa 2000 bure
Ila yote kwa yote haya ni maisha yangu na familia yangu
Nikiwa Baba wa familia ni muhimu kuhakikisha ndani chakula hakiishi

Muhimu familia hailali njaa basi

Kuhusu maendeleo mada haihusiani na maendeleo mada inahusiana na Baba kurudi nyumbani na mfuko wa sokoni
Sio kazi ya baba kwenda sokoni.
 
sio kila siku unaweza kurudi na mfuko wa sokoni maana siku hazifanani katika utafutaji
 
sio kila siku unaweza kurudi na mfuko wa sokoni maana siku hazifanani katika utafutaji
Yeah huwezi kurudi na mfuko wa sokoni kila siku maana vitu vitakuwa vinajaa

Mimi huwa nikifika hom napita kwa mangi nachukua big G au pipi ya kijiti Big Bon nikiingia ndani nampa

Baadhi ya siku namchukulia ice cream ya jero hizi za ukwaju napeleka

Siku nyingine hata kama nipo fresh sibebi kitu
Namfanya asinikariri pia ijulikanae kuna kupata na kukosa, yaani sieleweki eleweki
 
Sina haja ya kujibu maswali ya kipumbavu. Cha muhimu jua kwenda sokoni ni kazi ya mwanamke.
Ukute wewe ni mwanamke umekosa bahati ya kuolewa sasa unaonea wivu wanawake wenzio
Mkuu haya ni maisha tu, na watu kama nyinyi ndo mnafanya maisha yaonekane magumu
Ishu ya mwanamke kwenda sokoni simzuii, akiamua anaenda kama sa hv nimeingia ndani nakuta kapika ndizi na aliniambia kabisa anaenda sokoni kununua ndizi,

Mimi nimechangia mada mkuu KURUDI NA MFUKO WA SOKONI

Kazi nafanya kariakoo, njia ya kurudi home ni lazima nipite kariakoo sokoni na hata nikiwa naenda ni lazima nipite kariakoo sokoni

Hivyo wewe unachopinga ni kusema, "Mwanaume utoke nyumbani uende sokoni kununua vitu". Wakati mimi nilichozungumzia ni kwamba mahitaji ya sokoni narudi nayo maana njia yangu ni kariakoo sokoni(hapa ndipo tunaposhindwa kuelewana)

Pia huwa naacha kodi ya meza kila siku japo kila kitu kipo ndani kwa hiyo mwanamke nimempa uhuru wa kuitumia pesa kwa mambo yake

Ndio mimi ni maskini lakini sijafika kukosa pesa ya kula, pia kula ndo kipaumbele changu, ninaposema kula sio kula ushibe hapana ni kula chakula bora

Maana umri wangu nahitaji kula vyakula vya kuimarisha Afya

Nakumbuka mwalimu wangu wa Biology aliwahi kuniambia, "Usipotumia pesa nyingi kwa chakula basi utatumia pesa nyingi kwa matibabu"

Nikutakie weekend njema mkuu
 
Back
Top Bottom