Mwanaume unawezaje kukaa ukweni zaidi ya wiki mbili?

Mwanaume unawezaje kukaa ukweni zaidi ya wiki mbili?

Mie mwanaume. Sasa mkwe wangu tuna biashara pamoja, na tunafanya mambo mengi pamoja. NI mwaminifu sana, na mchap kazi kweli kweli kwenye miradi tunayofanya pamoja. Sasa ukimfanya mkwe ni mtu wa kukuzalia mke tu, na ukawa na aina ya uhusiano ambao wewe ndio msaada kwa mkwe, unaongea nao mara moja moja wakimpigia simu mkeo na kusema tunaomba tumsalimu, utakaa huko ukweni kufanya nini? Make your inlaws part of your family, and be genuinely happy when you see them.
Poa mkuu umeeleweka
 
Ukishaoa pale pia ni nyumbani. Mfano umeoa tabora na unaishi dar inakuwaje?
Jitahidi ujenge kabanda kama unautaratibu wa kukaa sana ila kukaa ukweni zaidi ya siku moja lazima kuna mazoea ya ajabu yataanza tu... kama kuna tatizo au ishu ya msingi ambayo inawakutanisha watu wengi hapo sawa nawe unaweza kushiriki nao hadi watu wakianza kutawanyika na wewe aga sepa.
 
SIjui mila desturi na taratibu za makabila mengine. Ila ukweli hata kama umeoa kwenye familia ya kitajiri kwenda kukaa ukweni zaidi ya wiki mbili aisee unajidhalilisha.

Mzee wangu aliniambia ukikaa ukweni siku mbili zinataosha sana ya tatu unaondoka hii ni kwamba usijue maisha yao na wao wasijue mipango yako. Ukikaa sana ukweni kuna siku utatumwa chumvi dukani uone wanakudharau kumbe mipango yako sio.

Chini ya hili jua kuna wanaume achilia mbali kwenda kusalimia ukweni, wapo ambao wanaishi ukweni. Na hapo mtu anahitaji haishimike. Aisee ukiona unaishi ukweni na mwanamke anakuheshimu wee jamaa hata mbingu ni yako. Nawasilisha.
Kwetu kawauda hiyo, wakwe zetu wanaishi kwetu.

Kwanza sisi hatukubali kukaa kwa mume bila ya yeye kukaa kwetu.

Tukanyanyaswe?
 
Mila za watu wa pwani....
Kuna mahala nilishuhudia mtu ameoa na anaishi na mke wake huko huko ukweni
Kwa sisi tuliooa WACHAGA,

Suala la kulala ukweni ni MARUFUKU! Yaani SAHAU!

Kwanza binti akishaolewa, YEYE mwenyewe haruhusiwi kulala kwao, sembuse wewe??

Mimi alifariki baba mkwe, nililala lodge wiki nzima. Kila siku naenda msibani asubuhi, usiku narudi lodge kulala.
 
Kwa sisi tuliooa WACHAGA,

Suala la kulala ukweni ni MARUFUKU! Yaani SAHAU!

Kwanza binti akishaolewa, YEYE mwenyewe haruhusiwi kulala kwao, sembuse wewe??

Mimi alifariki baba mkwe, nililala lodge wiki nzima. Kila siku naenda msibani asubuhi, usiku narudi lodge kulala.
Dah wachaga mbona nasikia ni wabaguzi kama huna hela unaweza lala hata kwenye migomba hawana habari na wewe ni kweli?
 
Dah wachaga mbona nasikia ni wabaguzi kama huna hela unaweza lala hata kwenye migomba hawana habari na wewe ni kweli?
Mimi sijui kama ni ubaguzi au ni nini lakini utaratibu wao ndio uko hivyo. Mwanamke akishaolewa haruhusiwi kurudi nyumbani na kulala. Ataenda kusalimia tu asubuhi na kuondoka jioni kurudi kwa mumewe.

Na hii haijalishi hata kama mwanamke ameolewa nyumba ya 3 kutoka kwao, hawezi kwenda nyumbani kulala.

Binafsi niliona kama ni utaratibu mzuri
 
Mimi sijui kama ni ubaguzi au ni nini lakini utaratibu wao ndio uko hivyo. Mwanamke akishaolewa haruhusiwi kurudi nyumbani na kulala. Ataenda kusalimia tu asubuhi na kuondoka jioni kurudi kwa mumewe.

Na hii haijalishi hata kama mwanamke ameolewa nyumba ya 3 kutoka kwao, hawezi kwenda nyumbani kulala.

Binafsi niliona kama ni utaratibu mzuri
Yap utaratibu mzuri sana.
 
Back
Top Bottom