Mwandishi Andrew Chale anusurika kutekwa na watu wasiojulikana

Mwandishi Andrew Chale anusurika kutekwa na watu wasiojulikana

nginda

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
744
Reaction score
82
Dar es Salaam

MWANDISHI wa Habari wa Gazeti la Tanzania Daima Andrew Chale ameanza kuishi maisha ya wasiwasi baada ya watu wasiojulikana kufanya jaribio la kumteka.

Chale alisema kwamba siku ya Jumamosi usiku watu wasiojulikana walikuwa wakifuatilia nyedo zake.

Alisema watu walikuwa kwenye magari mawili yenye rangi na namba za Jeshi la Polisi walikuwa wakimfuta nyuma kila alipokuwa akipita kuelekea nyumbani kwake maeneo ya Sinza jijini Dar es Salaam.

"Siku ya Jumamosi usiku nikiwa njiai kutoka Kazini, niliona magari mawili ya Polisi yakinifuata kwa karibu na baada ya kuingia uchochoro flani wakuingia nyumbani magari hayo yakapaki"alisema Chale na kuongeza"

"Watu waliokuwa eneo hilo walisema kwamba baada ya magari hayo kupaki wakakaa hapo kwa saa mbili na baadaye walishuka askari watu huku wawili wakivaa nguo za kiraia huku mmoja akiwa na Gazeti la Tanzania Daima mkononi".

Alisema kwamba baada ya watu hao kushuka na kuuliza mtu waliemwita kwa jina la ANDRESON,, ndipo wakaambiwa kwamba hakuna mtu mwenye jina hilo katika mtaa huo lakini , walipoelezea mwonekano wake, wakajibiwa kuwa kijana anayefahamika eneo hilo hupita tu lakini mahali anapoishi hapajulikani.

"Tunayemfahamu ni kijana mmoja ila huwa anapita hapa akiwa na hilo Gazeti majira ya usiku, na wakati mwingine huwa anapita hapa akiwa na mambo yake mengine, baaada ya hapo magari hayo yaliondoka"aliwanukuu mashuhuda wa tukio hilo.

"Watu hao walirudi tena hadi nyuma ya nyumba yangu na nikawasikia wakijitambulisha kuwa wao ni Polisi jamiii na kwamba walikuwa wakimtafuta kijana mmoja ambaye wamesahau anapoishi"alifafanua Chale.

Source habarimpya.com

PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
Waandishi hawajaipa uzito habari ya kutekwa kibanda badala yake wanaona mtekaji lwaka ameonewa
 
baba amegonga mtu na kuendelea na safari akiwa na msafara wa magari mengi akifika atakuja na majibu nitamwambia
 
IKUlu inavyokazana kunyamazisha wakati ukifika watanyamazishwa vivyo
 
Mungu anusuru hilo balaa, waandishi muache kushabikia wauwaji muwe neutral.muige kenya
 
Tanzania ndio taifa lenye waandishi dhaifu na wasio na umoja na ambao hata hawaelewi nguvu walizonazo kama waandishi wa habari!

Hivi waandishi wa habari kwa umoja wao wakiamua kuungana na kutumia kalamu zao hii serikali itafua dafu?!

Hawana haja ya kuilamba serikali miguu bali serikali ndio inapaswa kuheshimu muhimili huu.Ila kwa kuwa waandishi wenyewe hawajitambui na kuendekeza "njaa njaa" zao wasubiri kuangamia mmoja baada ya mwingine.

Hivi waandishi wa habari mnapoambiwa kuwa taaluma yenu ni mhimili wa nne wa dola mnaelewa kweli maana yake?

Mimi nafikiri mnafaa kupokonywa hadhi hiyo kwani hamjitambui!

Au mpaka wamiliki wa vyombo vya habari nao wakianza kuong'olewa meno na kucha ndio muonyeshe makucha yenu?

Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.
 
Kwa nini hakuchukua namba za gari husika?
 
bora serikali ya mkoloni watu wahawakuishi kwa wasiwasi kama sasa.

kazi ya uandishi kwa sasa ukiwa mwoga lazima uweke kalamu chini nyenyua jembe begani moja kwa moja mwane-romamgo kulima mihogo. inatisha.
 
Tanzania ndio taifa lenye waandishi dhaifu na wasio na umoja na ambao hata hawaelewi nguvu walizonazo kama waandishi wa habari!

Hivi waandishi wa habari kwa umoja wao wakiamua kuungana na kutumia kalamu zao hii serikali itafua dafu?!

Hawana haja ya kuilamba serikali miguu bali serikali ndio inapaswa kuheshimu muhimili huu.Ila kwa kuwa waandishi wenyewe hawajitambui na kuendekeza njaa njaa zao wasubiri kuangamia mmoja baada ya mwingine.

Hivi waandishi wa habari mnapoambiwa kuwa taaluma yenu ni mhimili wa nne wa dola mnaelewa kweli maana yake?

Mimi nafikiri mnafaa kupokonywa hadhi hiyo kwani hamjitambui!

Au mpaka wamiliki wa vyombo vya habari nao wakianza kuong'olewa meno na kucha ndio muonyeshe makucha yenu?

Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.

Tanzania haina Waandishi wa Habari bali ina VIBARAKA Vya Habari.
 
Tanzania ndio taifa lenye waandishi dhaifu na wasio na umoja na ambao hata hawaelewi nguvu walizonazo kama waandishi wa habari!

Hivi waandishi wa habari kwa umoja wao wakiamua kuungana na kutumia kalamu zao hii serikali itafua dafu?!

Hawana haja ya kuilamba serikali miguu bali serikali ndio inapaswa kuheshimu muhimili huu.Ila kwa kuwa waandishi wenyewe hawajitambui na kuendekeza njaa njaa zao wasubiri kuangamia mmoja baada ya mwingine.

Hivi waandishi wa habari mnapoambiwa kuwa taaluma yenu ni mhimili wa nne wa dola mnaelewa kweli maana yake?

Mimi nafikiri mnafaa kupokonywa hadhi hiyo kwani hamjitambui!

Au mpaka wamiliki wa vyombo vya habari nao wakianza kuong'olewa meno na kucha ndio muonyeshe makucha yenu?

Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.

Haa haa haaa ... nacheka sio kama nakupuuza, ila nashindwa kuelewa waandishi wenye akili timamu wanaposhindwa kuona uliyoyaona wewe. Mkuu tamaa na kuweka njaa mbele ndio adui mkubwa wa waandishi wa Tanzania. Wameshaazima akili za nyumbu wa serengeti hivyo kuwavua hhizo fikra sio rahisi.
 
Ni kweli kabisa. Kwanza wengi ni ma- reporter tu skills za uandishi hawana! Magazet mengi yanaandikwa kwa kutumia udaku style na haya stimulate critical thinking wala kuongeza knowledge yoyote kwa msomaji!

Tanzania haina Waandishi wa Habari bali ina VIBARAKA Vya Habari.
 
Back
Top Bottom