Mwandishi Andrew Chale anusurika kutekwa na watu wasiojulikana

Mwandishi Andrew Chale anusurika kutekwa na watu wasiojulikana

Waandishi hawajaipa uzito habari ya kutekwa kibanda badala yake wanaona mtekaji lwaka ameonewa

Hakuna post ambayo nitaitembelea nikose shudu lako lolote hongera sanaaaaaa..... sijui unafanya kazi saa ngapi na unahudumia kwel mkeo vizuri...... @ utaifakwanza mmmh! mpaka 2015 tutasikia mengi sanaaaaaaa
 
Mungu anusuru hilo balaa, waandishi muache kushabikia wauwaji muwe neutral.muige kenya
Utaifakwanza...hivi utaifa utakuwepo ikiwa watu wanaounda taifa wanauwawa...na kuumizwa kwa 'makusudi'!?

Kwa kiasi fulani inaonyesha dhahiri una kerwa na msimamo wa waandishi...na maoni/ushauri wako kwao ni kama unawatukana...yaani unataka kuuaminisha umma kuwa waandishi hawana uwezo wa kutambua na kutafakari haya yanayotokea juu ya wenzao!?

Nikipata muda nijaribu kutafuta ukweli kama unamfahamu 'NNAPPE' wa ukweli.
 
Waandishi sasa badilisheni mbinu zamedani kama JF. kuweni invisible, no real names.
 
Hata kama wengine mnabwabwaja tu humu ndani kuwa Tanzania hakuna waandishi wa habari, lakini wengi wetu hata humu ndani tunatumia ID ambazo hazifahamiki (tunajificha) hao tunao wadharau kwangui naona wanajitahidi pamoja na mapungufu yao. Tusilaumu saana kama vile sisi tuko sahihi kihivo.
 
CDM wanataka kutengeneza move mpya ili tusahau ya Gaidi Lwakatare na Mtandao wake wa kigaidi wa chadema. Huyo mwandishi wa Free Media chini ya Mbowe amepewa maelekezo aigize.Hapa hapotezwi mtu. Huko analogia tulishahama tuko Digital kajipangeni upya.
 
Ndani ya hizo gari kulikua na Koleo la kung'olea kucha na meno,
Bisibisi ya kutobolea macho,
Marungu na nyundo,
Ila hakukua na Ganzi! !!!!
 
Hakuna namba ya gari.Watu wengine tunaweza kusema habari hii imepikwa ili kupoteza mwelekeo wa kufuatilia kesi ya msingi ya bwana Lwakatare.Kama umeliona gari la polisi, weka namba ya gari hapa, naamini uliiona plate number inayoanzia na "PT.....".malizia na namba zingine.kama hiyo gari ilisimama for dam 2 hours, ni hakika kwamba number yake inajulikana.na kwanini watembee na gazeti la Tanzania Daima, tena usiku?hao waliolisoma hilo gazeti, walilimulika na tochi?au waliwamulika hao polisi?au hapa kwetu hatuna "investigative journalism", tunaandika tu kuwatia hofu watu wengine.Kwa hiyo hata mwandishi akiwa barabarani akaona gari ya polisi ikiwa kwenye doria za kawaida anahisi anafuatiliwa?
Dar es Salaam

MWANDISHI wa Habari wa Gazeti la Tanzania Daima Andrew Chale ameanza kuishi maisha ya wasiwasi baada ya watu wasiojulikana kufanya jaribio la kumteka.

Chale alisema kwamba siku ya Jumamosi usiku watu wasiojulikana walikuwa wakifuatilia nyedo zake.

Alisema watu walikuwa kwenye magari mawili yenye rangi na namba za Jeshi la Polisi walikuwa wakimfuta nyuma kila alipokuwa akipita kuelekea nyumbani kwake maeneo ya Sinza jijini Dar es Salaam.

"Siku ya Jumamosi usiku nikiwa njiai kutoka Kazini, niliona magari mawili ya Polisi yakinifuata kwa karibu na baada ya kuingia uchochoro flani wakuingia nyumbani magari hayo yakapaki"alisema Chale na kuongeza"
"Watu waliokuwa eneo hilo walisema kwamba baada ya magari hayo kupaki wakakaa hapo kwa saa mbili na baadaye walishuka askari watu huku wawili wakivaa nguo za kiraia huku mmoja akiwa na Gazeti la Tanzania Daima mkononi".

Alisema kwamba baada ya watu hao kushuka na kuuliza mtu waliemwita kwa jina la ANDRESON,, ndipo wakaambiwa kwamba hakuna mtu mwenye jina hilo katika mtaa huo lakini , walipoelezea mwonekano wake, wakajibiwa kuwa kijana anayefahamika eneo hilo hupita tu lakini mahali anapoishi hapajulikani.

"Tunayemfahamu ni kijana mmoja ila huwa anapita hapa akiwa na hilo Gazeti majira ya usiku, na wakati mwingine huwa anapita hapa akiwa na mambo yake mengine, baaada ya hapo magari hayo yaliondoka"aliwanukuu mashuhuda wa tukio hilo.

"Watu hao walirudi tena hadi nyuma ya nyumba yangu na nikawasikia wakijitambulisha kuwa wao ni Polisi jamiii na kwamba walikuwa wakimtafuta kijana mmoja ambaye wamesahau anapoishi"alifafanua Chale.



source habarimpya.com
 
baba amegonga mtu na kuendelea na safari akiwa na msafara wa magari mengi akifika atakuja na majibu nitamwambia

Inasikitisha sana yule mama namfahamu anakaa maeneo ya Bunju Shule nishawahi kukaa naye seat moja wakati naenda Bagamoyo akashukia kituo cha Bunju Shule.
 
Ukitaka amani, kawe mwandishi wa uhuru na daily news! au hamia tbc
 
Dar es Salaam

MWANDISHI wa Habari wa Gazeti la Tanzania Daima Andrew Chale ameanza kuishi maisha ya wasiwasi baada ya watu wasiojulikana kufanya jaribio la kumteka.

Chale alisema kwamba siku ya Jumamosi usiku watu wasiojulikana walikuwa wakifuatilia nyedo zake.

Alisema watu walikuwa kwenye magari mawili yenye rangi na namba za Jeshi la Polisi walikuwa wakimfuta nyuma kila alipokuwa akipita kuelekea nyumbani kwake maeneo ya Sinza jijini Dar es Salaam.

"Siku ya Jumamosi usiku nikiwa njiai kutoka Kazini, niliona magari mawili ya Polisi yakinifuata kwa karibu na baada ya kuingia uchochoro flani wakuingia nyumbani magari hayo yakapaki"alisema Chale na kuongeza"
"Watu waliokuwa eneo hilo walisema kwamba baada ya magari hayo kupaki wakakaa hapo kwa saa mbili na baadaye walishuka askari watu huku wawili wakivaa nguo za kiraia huku mmoja akiwa na Gazeti la Tanzania Daima mkononi".

Alisema kwamba baada ya watu hao kushuka na kuuliza mtu waliemwita kwa jina la ANDRESON,, ndipo wakaambiwa kwamba hakuna mtu mwenye jina hilo katika mtaa huo lakini , walipoelezea mwonekano wake, wakajibiwa kuwa kijana anayefahamika eneo hilo hupita tu lakini mahali anapoishi hapajulikani.

"Tunayemfahamu ni kijana mmoja ila huwa anapita hapa akiwa na hilo Gazeti majira ya usiku, na wakati mwingine huwa anapita hapa akiwa na mambo yake mengine, baaada ya hapo magari hayo yaliondoka"aliwanukuu mashuhuda wa tukio hilo.

"Watu hao walirudi tena hadi nyuma ya nyumba yangu na nikawasikia wakijitambulisha kuwa wao ni Polisi jamiii na kwamba walikuwa wakimtafuta kijana mmoja ambaye wamesahau anapoishi"alifafanua Chale.



source habarimpya.com
tatizo la tanzania polis ni sehemu ya watuhumiwa kwenye matukio ya utekaji!
 
Waandishi wa habari wameundiwa hali ya kuamini kuwa mbaya wao ni Lwakatare na kwa vile sasa yuko ndani basi wako salama,
Kalagabao
 
Huu upumbavu wa nchi hii, halafu kova ndo atakuwa msemaji mkuu wa hilo, hawa polisi ndo watuhumiwa inakuwaje wao ndo wasemaji tene, jamani taifa linaangamia
 
Eeh! ameripoti kituo kipi cha Usalama?

nadhani hukuielewa habari. Wanaotaka kumteka ni wana usalama, kisha aende kujisalimisha au? Unamfundisha kesi ya nyani aipeleke kwa ngedere au?
 
Back
Top Bottom