Ni wakati wa JF kung'ara
ALIYETAZAMWA KAMA ADUI WA SERIKALI ATEULIWA KUWA MJUMBE WA BODI NYETI!
Baada ya miaka kadhaa ya kuandamwa na kesi akishtakiwa na Jamhuri, Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo Mubyazi sasa ameteuliwa kuwa Mjumbe wa Bodi katika moja ya Mamlaka za Serikali. Kwa muono wetu sisi, uteuzi wake si hisani bali Serikali imeona ujuzi na uelewa wake katika eneo husika kwani Melo amekuwa mstari wa mbele kupazia sauti juu ya haki ya taarifa binafsi za watu.
Je, nani ajuaye kama Yericko Nyerere na Dkt. Chris Cyrilo siku moja watalishauri Baraza la Usalama la Taifa? Kama mtu humjui Dkt. Chris Cyrilo, akatafute kitabu chake cha: 'Istilahi za Uhalifu na Usalama'! Je, huo ndio muelekeo mchapuko (paradigm shift) wa Rais Dkt. Samia katika kushirikisha watu walio nje ya Serikali Je, una neno gani kwa Max Melo Mubyazi? Je, ni nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Dar es Salaam, 18 Desemba 2023; 4:21 usiku
Sent using
Jamii Forums mobile app