Mwandishi wa Habari Gordon Kalulunga adaiwa kusakwa na Jeshi la Polisi, aishi mafichoni

Mwandishi wa Habari Gordon Kalulunga adaiwa kusakwa na Jeshi la Polisi, aishi mafichoni

KooZito

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2020
Posts
397
Reaction score
1,377
Mwandishi wa Habari mkongwe Gordon Kalulunga anadai kusakwa na Jeshi la Polisi kila Kona ya jiji la Mbeya.

Kwa maelezo yake Kalulunga anasema tarehe 6 mwezi huu saa sita mchana alipigiwa simu na Msaidizi wa OCCID wilaya ya kipolisi Mbalizi Christopher Makawia na kumwambia, "tukutane pale Benki ya NMB Mwakapangala jijini Mbeya kwa mazungumzo".

Kalulunga anadai alipofika alikuta gari la Polisi na maaskari wenye silaha za moto akapitiliza kuwapotezea.

Anadai, "aliendelea kunipigia lakini sikupokea kwa nini aniite maeneo yale na si kituoni".

Kalulunga anayemiliki blogu maarufu Mbeya ya Sauti ya Nyikani amekuwa mkosoaji wa matumizi ya Fedha za umma zinazoletwa mkoani humo.

"Nimepata taarifa kuwa ni DED ameagiza nikamatwe kueleza wapi ninatoa Siri za Serikali na kuandika mtandaoni".

Kalulunga ametoweka nyumbani kwake na ameeleza anaishi mafichoni kuhofia mazingira hayo.

My take: Haya mambo ya Polisi au Watumishi kutishia au kujenga uadui na wanahabari yaliachwa na kuondoka na awamu ya 5.
 
Mie sielewi jeshi la police KWa Sasa wakosa KAZI za kufanya, ebu achen Mambo aya jeshi la police ,jikiten KWa Mambo ya msingi ya nchi , KWa mjibu wa taratibu zenu na maelekezo ,na mwongozo wa KAZI zenu, ethics
 
Kwanza, tunakubaliana kimsingi kitisho dhidi ya waandishi wa Habari wanaofanya kazi kwa mujibu wa sheria, hakikubaliki kabisa. Pili, pia kuchukua siri za Serikali kinyume cha sheria pia haikubaliki.

Tatu na kinachokera zaidi, hivi DED kafanya yake wilayani huko, tunawezaje kutaja jina la Rais wetu na kumhusisha? Tunaingizaje CCM kama taasisi kwa jambo la DED? Tunaiingizaje Serikali kwa jambo la DED?

Kwa sababu inawezekana kabisa kama mimi nilivyosoma hapa ndivyo viongozi wa Chama na Serikali nao wameona hapa. Tusipende kuhukumu jumla jumla kwa kosa la mtu mmoja.
 
Kwanza, tunakubaliana kimsingi kitisho dhidi ya waandishi wa Habari wanaofanya kazi kwa mujibu wa sheria, hakikubaliki kabisa. Pili, pia kuchukua siri za Serikali kinyume cha sheria pia haikubaliki...
DED amechaguliwa na kiongozi wa CCM na CCM ndicho chama kinachounda serikali.

Hii tabia ya kutekana inajulikana wazi inafanywa kwa maslahi ya CCM, hivyo usipoteze muda wako kuitenga CCM, viongozi wake, na utekaji, utachekwa.
 
Back
Top Bottom