Mwandishi wa habari wa Al Jazeera, Shireen Abu Akleh auawa akiwa katika majukumu yake ya kazi

Mwandishi wa habari wa Al Jazeera, Shireen Abu Akleh auawa akiwa katika majukumu yake ya kazi

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
Shireen-Abu-Akleh-FB-piv-696x435.jpg

Mwandishi wa habari Shireen Abu Akleh enzi za uhai wake

Mwandishi wa habari wa Al Jazeera Shireen Abu Akleh (51) ameuawa kwa kupigwa risasi ya kichwa akiwa katika majukumu yake ya kazi wakati akifuatilia uvamizi wa Jeshi la Israel kwenye kambi ya wakimbizi ya Jenin.

Wizara ya Afya ya Palestina imesema Bi. Akleh alipigwa risasi ya kichwa huko Jenin, na kufariki muda mfupi baadaye.

Al Jazeera imevishutumu vikosi vya usalama vya Israel kwa kumlenga na kumuua kwa makusudi Abu Akleh na kuitaka jumuiya ya kimataifa kulaani na kuiwajibisha Israel.

Jeshi la Ulinzi la Israel limesema vikosi vyake vya usalama vimekuwa vikifanya kazi katika eneo hilo "kuwakamata washukiwa wa shughuli za kigaidi," na washukiwa wa Kipalestina.

Mwandishi mwingine wa habari wa Al Jazeera, Al-Samudi, ambaye alikuwa na Abu Akleh wakati alipouawa, alisema hakukuwa na wapiganaji wa Kipalestina katika eneo hilo wakati huo. "Jeshi la Israel lilitupiga risasi," alisema Al-Samudi ambaye pia alipigwa risasi. "Hakukuwa na mpiga risasi wa Kipalestina mahali hapo."

Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel, Yair Lapid, alisema kupitia Twitter kwamba serikali yake imejitolea kufanya uchunguzi wa pamoja wa Israel na Palestina, na kuongeza kuwa: "Wanahabari lazima walindwe katika maeneo yenye migogoro na sote tuna jukumu la kupata ukweli."

Akleh aliwahi kufanya kazi na UNRWA, Voice of Palestine Radio, Amman Satellite Channel, Miftah Foundation na Monte Carlo Radio kabla ya kujiunga na Al Jazeera.
 
Wakulaumiwa ni Al Jazeera, unaenda kufanya ripoti mahali kuna oparesheni inaendelea. Hii kiherehere ya kutaka kuoneka unapeperusha live kutoka vitani itawaponza hawa wanahabari.
Haya ndio tunayosema kila siku, oooh Russia imevamia Ukraine watu wanakufa oooh sijui nini, ila wakifa Wapalestina basi ni sawa.

Usichokijua na huenda unakijua ila ndio basi hutaki kujali, Israel imejimegea karibu eneo lote la Palestina hata lile walilopewa kwenye mkata uliandaliwa na Umoja wa mataifa.

Wapalestina wanaishi kwenye makambi makambi nayo bado anayataka.
 
Hivi angepigwa mwandishi wa habari wa CNN na vikosi vya Russia kule Ukraine,nini kingetokea?

Hapa inalaumiwa Al-Jazeera Kwanini wamepeleka waandishi vitani lkn Kwa mahaba yetu endapo angekufa mwandishi mzungu,dunia mzima ingelaani Russia..

Dunia haina usawa kabisa
 
Alikuwa anatumika kuspy huyo pia, mossad walivyogundua mpango wa kumla shaba kwa bahati mbaya ukatekelezwa haraka.
Ili mradi ujustify tu.
Ikiwa Ukraine basi kelele. Some people are more humans than others.

Angalia hii ramani, tena hiyo mwaka 1947 Israel walisaini mkataba wa kukubali hiyo ramani lakini ona leo wamechekua eneo lote na hata hayo makambi wanayataka.

Lakini husikii mkipiga kelele

images (16).jpeg
 
Hivi angepigwa mwandishi wa habari wa CNN na vikosi vya Russia kule Ukraine,nini kingetokea?

Hapa inalaumiwa Al-Jazeera Kwann wamepeleka waandishi vitani lkn Kwa mahaba yetu endapo angekufa mwandishi mzungu,dunia mzima ingelaani Russia..

Dunia haina usawa kabisa
Double standards hawa wapiga vigelegele uwa wanajitoa ufahamu.

Na sheria za kuwalinda waandishi wa habari zipo. Hata eti fasta wanamwita spy.

Yani hii dunia hii we acha tu
 
Wakulaumiwa ni Al Jazeera, unaenda kufanya ripoti mahali kuna oparesheni inaendelea. Hii kiherehere ya kutaka kuoneka unapeperusha live kutoka vitani itawaponza hawa wanahabari.
hahahahaaa unapeperusha live ?
 
Ingekuwa jeshi la russia ndiyo limefanya hivyo tungesikia kelele kila kona
Kelele kila kona kivipi, hujaona hadi vyombo vyote vya magharibi mnavyosemaga ni vya propaganda vimetangaza hiyo habari
 
Haya ndio tunayosema kila siku, oooh Russia imevamia Ukraine watu wanakufa oooh sijui nini, ila wakifa Wapalestina basi ni sawa.
Hivi Palestina wasingekuwa waanzisha choko choko , lini wangepoteza hilo eneo?

Hivi ukivamiwa halafu akatumia kisu ukimdhibit unamuachia hicho kisu?
 
Double standards hawa wapiga vigelegele uwa wanajitoa ufahamu. Na sheria za kuwalinda waandishi wa habari zipo. Hata eti fasta wanamwita spy.
Yani hii dunia hii we acha tu
Binadamu akiamua kuchagua upande Fulani wa kusimamia,hata umwambie nini hawezi kukuelewa..hao jamaa kila kitu wanaona Sawa tu kwa sababu waliofanyiwa hiko kitendo ni Al-Jazeera
 
Hivi angepigwa mwandishi wa habari wa CNN na vikosi vya Russia kule Ukraine,nini kingetokea?

Hapa inalaumiwa Al-Jazeera Kwa Kwa nn wamepeleka waandishi vitani lkn Kwa mahaba yetu endapo angekufa mwandishi mzungu,dunia mzima ingelaani Russia..

Dunia haina usawa kabisa
Kwani hujasikia mwandishi aliuliwa huko Ukraine , umesikia mtu analialia?

Maana kajipeleka mwenyewe , kaona habari ni bora kuliko uhai wake
 
Back
Top Bottom