Mwanmke anaekimbilia kuvunja ndoa kisa mali furaha yake hudumu kwa muda mfupi kwenye nyumba isiyo na mume wa kumheshimisha kwenye jamii

Mwanmke anaekimbilia kuvunja ndoa kisa mali furaha yake hudumu kwa muda mfupi kwenye nyumba isiyo na mume wa kumheshimisha kwenye jamii

Mwa
Mkuu hakuna mwanamke timamu na anayejiheshimu anayezipenda hizo tabia labda awe mpumbavu na malaya tu, ila ni jamii ndio inalazimisha wanawake wakubaliane nazo, sababu wameambiwa hizo ndio tabia za wanaume wote hivyo hakuna namna wanatakiwa wavumilie tu
Mwanamke ndio mlezi wa watoto , angeweza kuwalea watoto vizuri ata hizo tabia zingetoweka .
 
Huwa najiuliza hivi wanaume ukitoa hizo pesa na mali huwa mnataka mpendewe nini kingine, maana kama ni mionekano wengi mna mionekano ya kawaida ambayo haiwashitui wanawake na kama ni tabia ndio kabisa wenyewe tabia zenu mnazijua, utasikia "oo nataka unipende kama nilivyo" mbona hata ninyi huwa hamuwapendi wanawake kama walivyo ni either mtapenda mionekano au tabia nk

Huwa mnasema pesa na mali vinaisha kwani uzuri na mvuto ndio haviishi, tena binafsi naona bora hata yule ambaye anampendea mtu pesa maana zinatafutwa kuliko yule anayempendea mtu uzuri maana uzuri hautafutwi na binadamu hajiumbi, si kila mtu anapenda hayo ma surgery na ma make up maana mengi yana madhara tu

Na kingine ninyi wenyewe mkishawaweka ndani hao wanawake huwa mnachepuka kama mnavyosema wenyewe, mwanaume hatosheki na mwanamke mmoja hivyo tunaassume hakuna mwanaume asiyechepuka na ukiacha kuchepuka pia wengi ni walevi au wanywaji, hivyo mkitoka kwenye shughuli za utafutaji huwa mnaamua kukaa baa na washikaji hadi kupelekea kuchelewa kurudi nyumbani

Mara nyingi mnajikuta mnakosa muda wa kukaa na familia zenu either wake tu au wake na watoto, na wake zenu wakihoji huwa mna kauli zenu eti ninyi ndio mmetoa mahari hivyo mna haki ya kurudi muda wowote mnaotaka bila kuulizwa, mara sijui mnataka turudi mapema ili tukae tuanze kupiga umbea na kuangalia tamthilia mara oo kwani wewe humu ndani unakosa nini si unavaa, unakula, unalala na mahitaji yako mengine unapata sasa unataka nini

Mwisho wa siku mke anaona kwahiyo kumbe hivyo unavyompa (ambavyo ni pesa na mali) unaona ndio vya muhimu zaidi kwake kuliko uwepo wako, ndipo hapo naye anapoanza kujenga interest na mali zako zaidi kuliko wewe, na akiona unaendelea na tabia zako za kuchepuka na kuchelewa kurudi nyumbani hana budi kuvunja hiyo ndoa ili mgawane hizo mali maana wewe humpi muda wako
Naomba utupie picha humu jf, mionekano ya wanaume inayowashtua wanawake Jadda
 
Mwa

Mwanamke ndio mlezi wa watoto , angeweza kuwalea watoto vizuri ata hizo tabia zingetoweka .
Mwanamke ni mlezi wa watoto kwenye suala la ukuaji wa mwili mkuu, ila tabia ni jukumu lenu wote baba na mama, wanaume msiwaachie wanawake tu

Halafu pia genetics nazo siyo kitu cha kudharau, zina nguvu na zinaplay part kubwa katika kuamua tabia na akili za mtoto, so watoto wanaweza kurithi tabia za hovyo za baba zao hata walelewe vipi

Na waswahili wana msemo wao unasema "vya kurithi vinazidi"
 
Mwanamke ni mlezi wa watoto kwenye suala la ukuaji wa mwili mkuu, ila tabia ni jukumu lenu wote baba na mama, wanaume msiwaachie wanawake tu

Halafu pia genetics nazo siyo kitu cha kudharau, zina nguvu na zinaplay part kubwa katika kuamua tabia na akili za mtoto, so watoto wanaweza kurithi tabia za hovyo za baba zao hata walelewe vipi

Na waswahili wana msemo wao unasema "vya kurithi vinazidi"
Kabsa mkuu
 
Asilimia 80 ya waliopeana talaka baada ya miaka kumi ujutia maamuzi Yao na kutamani siku zirudi nyuma waungane tena hasa kama walishazaa sema ndio hivyo tena.
Ule muunganiko wa kiroho ni muunganiko wa kiMungu
Hakuna mshindi kwenye talaka...both parties loose.
 
Back
Top Bottom