Mwanza: Bomoabomoa yaacha Machinga na vilio

Kipindi mwendazake alivyokuwa akiwathamini wamachinga, wapinzani wa humu JF including ww mwenye hii thread(Erythrocyte ) walimponda sana "wanachafua jiji..."

Eti leo mnawaonea huruma hapo ndio utajua wanasiasa na wafuasi wao wote sigara kali.

Hili tena wale wale walilokuwa wakilipinga wakati wa mwendazake, leo wanalikubali na washaligeuza mtaji wao wakisiasa, huu unafiki..........
 
Kwani CCM ambao ndio waliwaambia wamachinga watembee kifua mbele wako wapi? Si kuna wabunge zaidi ya 360+ wanakula mishahara ya bure?Si mliaminishwa kwamba wapinzani wanatuchelewesha,leo mnawalilia?sasa acha watu wajifunze 'the hard way'
 
Huko kwenu Mnz si ndio mliompatia Mama Uchifu tena mkampa na jina Hangaya??? Leo kawageuka mnaanza kutafuta pa kutokea, pambaneni na Hali yenu.
 
Namimi nasema wapinzani waendelee na mambo yao waachache na hii operation ya wamachinga,hawa ndio walikuwa viherehere kutoa matamko sijui wamachinga nchi nzima tunamuunga mkono yule Bwana aliyetangulizwa kuzimu,acha wale matunda ya uchaguzi wao
 
Maendeleo huendana na maumivu ya muda mfupi,hilo ni jambo la kawaida,


Kwako Pingapinga FC.
 
Mabadiliko yoyote huwa ni machungu. Wavumilie, watazoea.
Mama simkubali mambo mengi, lakini kwenye hili nampa heko.
Lazima tuwe systematic sio kufanya biashara kiholela. Lakini bado lawama zangu kwa serikali inayoongozwa na CCM. Miaka yote waliacha umachinga ukue. Enzi hizo nakumbuka ilikua raha kutembea Kariakoo. Kipindi mambo haya yanaanza walikaa kimya hakuna jitihada.
Wameulea uozo.
Tatizo ni siasa nyepesi za viongozi wetu walafi na majuha.
 
Hii ishu siyo ya upinzani na hata wakikaa kimya haiwanyimi kura. Upinzani wametusaidia kwa muda mrefu sana lakini tulishindwa kuwashika. Tena walisema wapinzani wanatuchelewesha! Hapo mwanza kuanzia wenyeviti, madiwani na wabunge ni wa ccm, wakuu wa wilaya na mikoa ni wa ccm. Bado tu unaomba upinzani wazungumzie hili au unataka waonekane wachochezi? Mi nadhani upinzani waendelee kupambana na tume ya uchaguzi pamoja na katiba mpya.

Suala la wao kuondoka ni lazima waondoke ili kuweka mazingira salama kwa watu wote ila CCM wameshindwa kutumia njia nzuri na bora za kuwahamisha. Tatizo walilonalo ni kuamini mtu mmoja tu ndio anaweza kuamua kila kitu. Alikuwepo Raisi aliyepita alikuwa na mtazamo wake juu ya jambo hili, huyu nae anamtazamo wake na atakae kuja atakuwa na wake, hatuwezi kwenda hivyo.! Tunahitaji kuwa na mikakati mizuri ya kibiashara kwa wote hata kwa muda wa miaka 50 mbele.
 
Mpumbafu!!
Wapinzani ndo wamebomoa?
Kuna mpinzani yeyote bungeni?
Mpumbafu!
 

Aise umeongea kwa uchungu sana, sasa hivi Mbowe na Familia yake ndio wanahangaika wenyewe huko mahakamani wengine wanaendelea kupiga soga kwenye space na club house, all in all watanzania ni binadamu wa ajabu sana katika species zote za watu weusi unazozifahamu kwa ufupi tu hawajui wanataka nini? Wapo wapo tu kama misukule.
 
Upinzani wakishajaziwa kura zitawasaidiaje?
 
mama D ame like na kukenua meno yote 32
Leo ndio wanamlilia Mungu? Machinga walikuwa wanadharau kusali walikuwa hawaendi kanisani wala msikitini kutwa umachinga tu!!

Sasa tutarajie kuona makanisa na misikiti ikijaa machinga kusali kwa sana
 
Si mtasema wapinzani wanapinga kila kitu.

Wameamua kuiunga mkono serikali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…