Mwanza City: The Photo Gallery

Hii nafikiri bajeti ijayo itafanyiwa kazi, pia inachagizwa na uwepo wa stendi ya Nyamhongolo bila shaka itakuwa soon
Hv kutoka nyamhongolo hadi buswelu ni km 9 ,,,mbona umbali kama sielewi kwa sababu kutoka national hadi buswelu ni km 5 wakati national huwa napaona ni mbali kuliko nyamhongolo
 
Meter chache kutoka keep left ya Kiseke kama unaelekea aridhi kabla hujafika filling station ya upande wa kulia, kuna barabara inaingia kulia ndio Mboga mboga hapo
Oky ..hvi ile lami inayojengwa kutoka round about ya halmashauri kupita kahama inaishia maeneo gani.maana nataka ninunue kiwanja maeneo ya huko
 
Oky ..hvi ile lami inayojengwa kutoka round about ya halmashauri kupita kahama inaishia maeneo gani.maana nataka ninunue kiwanja maeneo ya huko
Navyosikia mpango ni kuunganisha Buswelu na Kayenze kupitia Kahama, Ilalila, Kabusungu (Hospital ya wilaya) mpaka Kayenze. Ni main Road hiyo ukipata maeneo ya jirani na hiyo corridor ni asset nzuri sana.
 
Lengo ni kufika mpaka Igombe
Lami ikikamilika litakuwa bonge la shortcut kuelekea Ukerewa kwa kivuko. Pale nasikia muda ni mfupi sana hata bei pia ni nafuu kuliko mtu akitokea Kirumba au Mwanza North port. Nilimsikia Angelina alikuwa anapiganisha kipatikane kivuko cha pili kisaidiane na MV. Ilemela kuvusha abiria na magari. Igombe -Bezi kisiwani - Nansio.
 
Nyamagana sijua wanafeli wapi ,au geographical feature inawaangusha milima milima...yaan sioni project za ujenzi wa barabara ukilinganisha na ilemela ,,,,,,hadi mkuu wa mkoa aliwasifu ilemela wako vizuri na hati yao ya CAG iko poa ...
Barabara ya kwenda kanyerere kutokea mkuyuni ina watu wengi sana na inaunganisha hadi Nyakato , Igoma.lakini kuna vumbi na magari ya kule yanajaza hadi kero kwa sababu ya uchache unaosababishwa na ubovu wa barabara .
Mahina ni eneo kubwa sasa mjini kuna watu wengi lakini pametengwa kama sio mwanza ,kule ni shida tupu kuanzia barabara,huduma za umeme na maji kidogo sa hv ..
Luchelele nako kumetengwa hadi watu wanasema ile ni kigamboni ya mwanza
 
Sina uhakika labda Mbunge wao sio msumbufu kwa wizara husika. Ilemela ni mpya lakini inakuja kasi sana kuliko Nyamagana.
Nyamagana wapo nyuma kwa kila kitu mpaka usimamizi wa miradi.
Wakati mkuu wa mkoa anakabidhiwa stendi ya Nyamhongolo aliwasifu watenndaji wa Ilemela na kuwaambia watu wa Jiji waje Ilemela wajifunze namna ya kusimamia miradi iishe kwa wakati.
 
Upigaji labda 😁 😁 😁 😁 kwa aridhi Ilemela bado ina maeneo makubwa sana yanayotoa nafasi kwa miradi mikubwa kufanyika kwa gharama nafuu na fidia ndogo. Naona Nyamagana ni kama imejaa. Kuweka miradi mikubwa mikubwa ya kitaasisi kama vyuo , mashule kupata aridhi kubwa kwa bei nafuu ni kitu kigumu sana tofauti na Ilemela.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…