KERO Mwanza: Hali ya Barabara Mtaa wa Chenga ni mbaya, Wananchi wakitaka kuiboresha wanazuiwa

KERO Mwanza: Hali ya Barabara Mtaa wa Chenga ni mbaya, Wananchi wakitaka kuiboresha wanazuiwa

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

KwetuKwanza

Member
Joined
Mar 13, 2023
Posts
82
Reaction score
150
1000081286.jpg
Huku kwetu Mtaa wa Chenga pamoja na maeneo ya jirani ya Kata Nyegezi tumekuwa tukilalamikia changamoto ya barabara ambayo imekuwepo kwa muda mrefu ambayo inasababisha usumbufu mkubwa kwetu ambao tunaitumia.

Barabara hiyo ni muhimu na inatumiwa na Wanafunzi kwa asilimia kubwa kwa kuwa ipo karibu na Shule za Msingi Nyabulogoya na Nyegezi pamoja na Shule ya Sekondari Nyabulogoya.

Mbali na barabara hiyo kuharibiwa na maji ya mvua ila Wananchi wakitaka kujitolea kufanya ukarabati wa barabara hiyo, viongozi wa mtaa wamekuwa wakiwakataza na kusema ipo bajeti ya ukarabati wa Barabara, wanatoa kauli hiyo tangu Julai 2024.

Hii sio sawa, inabidi suala hili lifanyiwe kazi kwa kuwa linatuumiza wengi na linaathiri hata shughuli zetu za kiuchumi.
========================

UFAFANUZI WA SERIKALI YA MTAA
JamiiForums imewasiliana na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Chenga, Kata Nyegezi, Venance Edward Msinga kuhusiana na suala hilo, anafafanua:

Changamoto hiyo tunaifahamu na tumeiwasilisha kwa Vyombo husika, TARURA, ambao walisema kuna mafungu ya bajeti ya hilo suala yanakuja Januari (2025) sijajua imefikia wapi.

Pia tunatarajia kuwa na kikao na Mkuu wa Wilaya, tutaitumia nafasi hiyo kuzungumza suala hilo pamoja na Diwani kwa kuwa ni suala la muda mrefu.

Kuhusu Serikali ya Mtaa kuzuia Wananchi kufukia au kushughulikia barabara hizo mbovu, hatujawazuia kufanya kitu kama hicho.
WhatsApp Image 2025-01-14 at 10.50.52_8972bd05.jpg

WhatsApp Image 2025-01-14 at 10.50.51_d1fcb560.jpg

WhatsApp Image 2025-01-14 at 10.50.39_4a0bde70.jpg

WhatsApp Image 2025-01-14 at 10.50.34_d94dc52f.jpg

WhatsApp Image 2025-01-14 at 10.50.30_5a51e2e5.jpg
 
Hatari sana, hapo kuna serikali kweli? Kodi zenu zinatumika kufanya nini kama hiki sio kipaumbele cha eneo lenu hilo?

Kuna serkali ya mtaa, Diwani, Mbunge, mkuu wa wilaya, Mkoa nk.

Maendeleo yatakujaje kama barabara hazipitiki? Kwenda kazini, shuleni, hospitali, kwenye biashara, popote shida?
 
Waiteni mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya mbunge achananeni na hao watu wa serikali ya mtaa
Watawachelewesha

Ova
 
Mtaa wenyewe jina chenga,,,basi hata na viongozi wake nao ni chenga
 
Huku kwetu Mtaa wa Chenga pamoja na maeneo ya jirani ya Kata Nyegezi tumekuwa tukilalamikia changamoto ya barabara ambayo imekuwepo kwa muda mrefu ambayo inasababisha usumbufu mkubwa kwetu ambao tunaitumia.

Barabara hiyo ni muhimu na inatumiwa na Wanafunzi kwa asilimia kubwa kwa kuwa ipo karibu na Shule za Msingi Nyabulogoya na Nyegezi pamoja na Shule ya Sekondari Nyabulogoya.

Mbali na barabara hiyo kuharibiwa na maji ya mvua ila Wananchi wakitaka kujitolea kufanya ukarabati wa barabara hiyo, viongozi wa mtaa wamekuwa wakiwakataza na kusema ipo bajeti ya ukarabati wa Barabara, wanatoa kauli hiyo tangu Julai 2024.

Hii sio sawa, inabidi suala hili lifanyiwe kazi kwa kuwa linatuumiza wengi na linaathiri hata shughuli zetu za kiuchumi.
========================

UFAFANUZI WA SERIKALI YA MTAA
JamiiForums imewasiliana na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Chenga, Kata Nyegezi, Venance Edward Msinga kuhusiana na suala hilo, anafafanua:

Changamoto hiyo tunaifahamu na tumeiwasilisha kwa Vyombo husika, TARURA, ambao walisema kuna mafungu ya bajeti ya hilo suala yanakuja Januari (2025) sijajua imefikia wapi.

Pia tunatarajia kuwa na kikao na Mkuu wa Wilaya, tutaitumia nafasi hiyo kuzungumza suala hilo pamoja na Diwani kwa kuwa ni suala la muda mrefu.

Kuhusu Serikali ya Mtaa kuzuia Wananchi kufukia au kushughulikia barabara hizo mbovu, hatujawazuia kufanya kitu kama hicho.
Jaman kwani ukitaka kutoa taarifa kama hii unafanyaje
 
Back
Top Bottom