Mwanza: Mama mbaroni kwa kuwatelekeza watoto kwenye majaruba ya mpunga usiku

Mwanza: Mama mbaroni kwa kuwatelekeza watoto kwenye majaruba ya mpunga usiku

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
ac66100e0ebe95b6eb87815a71c99aa6

Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza limemtia mbaroni mama mmoja aitwaye Happyness Mafuru, kwa tuhuma ya kuwatelekeza watoto wake wawili katika majaluba ya mpunga, huko mtaa wa Mtakuja kata ya Nyamhongolo wilayani Ilemela Jijini Mwanza.

Watoto hao wameokotwa wakiwa hai na kisha kupelekwa katika hospitali ya rufaa ya kanda Bugando Jijini Mwanza, ambako wanaendelea kuchunguzwa afya zao wakati uchunguzi dhidi ya tukio ukiendelea.

Watoto hao wameokotwa majira ya saa tisa usiku, huku baridi ikiwa ni yao na usalama ukiwa ni tishio la maisha yao, kama anavyosimulia Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Mtakuja Adamu Magina.

============

Ni dhahiri kuwa wapo wanaohitaji watoto lakini hawajabahatika kuwapata, na waliobahatika wanashindwa kushukuru kwa kupata bahati hiyo ya mtende, lakini Je, ni hatua zipi zitafuata kwa Happynes na mumewe?

Kwa wenye kufahamu majaluba ya mpunga, katika kipindi hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha nchini majaluba mengi yamejaa maji, hivyo unaweza kupata picha, jinsi watoto hao walivyokuwa wakikabiliwa na wakati mgumu kunusuru uhai.
 
Kwaiyo mama alienda kupiga show time akanogewa na kusahau watoto ama,,
 
Afande wa mbele kashusha barakoa wakati afande wa nyuma kamechisha barakoa na nguo
 
Hii habari imenisikitisha sana asee,hasa hayo mazingira ambapo watoto waliachwa so sad... all in all wanaume tukumbuke majukumu kama tumeamua kuwa na familia na sio kukimbia na kusababisha mateso kwa viumbe wasio na hatia...
 
Hapo unakuta mtu kanywa miti yote ya duniani kala kila kitu isipokua sumu, nyumba ina mitishamba ka mganga wa kienyeji kazunguka hospitali zoote kapandikiza kaambulia patupu kila siku mto wake wa kulalia unalowana kwa machozi ya uchungu kuto pata mtoto! halafu mwingine anakwambia alilewa akafanya kimoja tu na mimba kapata au mwingine anapiga kabisa simu umsaidie wapi hospital nzuri akatoe mimba wengine wanatupa chooni "dunia kizungumkuti jamani"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumbe hii stori imeanzia mbali.Mi nilikuwa nashangaa mbona haijakamilika ila watu wana comment kama vile wanaijua sana!

Binafsi ningependa kujua aliwaacha saa ngapi?

Hiyo saa Tisa usiku nani aliwaokoa huko?Je ni watu wa ulinzi shirikishi?Maana sio kawaida saa tisa watu kuwa majarubani!

Kwani alikuwa ameolewa?Aliwaazaaje kwa mpishano huo wa umri?
Kwa mujibu wa twiter, watoto hao ni wachanga kabisa. Mmoja ana mwa na miezi 7 na mwengine miezi 4.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumbe hii stori imeanzia mbali.Mi nilikuwa nashangaa mbona haijakamilika ila watu wana comment kama vile wanaijua sana!

Binafsi ningependa kujua aliwaacha saa ngapi?

Hiyo saa Tisa usiku nani aliwaokoa huko?Je ni watu wa ulinzi shirikishi?Maana sio kawaida saa tisa watu kuwa majarubani!

Kwani alikuwa ameolewa?Aliwaazaaje kwa mpishano huo wa umri?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata huko twiter haikukamilika pia. Kilichoelezwa twitani ambacho hakikuandikwa kwenye hii habari ya hapa JF ni huo umri wa hao vichanga tu basi. Hata mimi najiuliza waliokolewaje? ilikuwaje au niseme walionekanaje? n.k
 
Hii habari imenugusa sana unaanzaje kutelejeza watoto wadogo kiasi hicho mh
 
Inasikitisha sana.

Mwanamke akiamua ni Mtu mwenye ujasiri mkubwa sana.

Hebu fikiria Mtu ameweza kubeba Ujauzito kwa muda wa miezi Tisa, kisha akaja kujifungua kwa usalama.

Baadae huyo huyo aliepitia tabu zote hizo, anaenda kutelekeza Watoto wake aliowapatia tabu.

Huyo Mama wamuangalie jamani.

Pengine amepatwa na matatizo ya kurukwa na Akili.

Maana kurukwa na Akili kunapishana, wengine wanaanza taratibu (pengine ndio yupo kwenye hatua za mwanzo).

Wasimuhukumu moja kwa moja, wamuangalie kwanza
 
Haya mambo yanawezekana.

Matukio mengi yanafanywa kwa sababu ya matatizo ya kiakili.

Bahati mbaya wengi kutokana na ubinafsi wa hali ya juu kabisa,wanaikataa situation halisi(self denial) na hivyo kushindwa kuchukua hatua stahiki.

Mfano hawa wanaoishi kwa kudanga mjini,kipindi cha kabla ya corona ukiwaambia wauze japo uji au mihogo kuliko kuishi kwa kudanga tu,wanaweza kukupa tusi hadi ujidharau.Ila sasa hivi hao madanga yao wana hali ngumu,wengine wamejifungia ndani,ukikuta mtu kama huyu,mfano wanaodanga kwa madereva wa malori,hali ilivyo sasa hivi,madereva wenyewe wanakutwa na corona,hali inakuwa tete sana.Kama ana watoto,ataenda kwa nani?Ndio hapo atajikuta anakuwa chizi maana hawezi kufanya chochote kazoea kudanga
Inasikitisha sana.

Mwanamke akiamua ni Mtu mwenye ujasiri mkubwa sana.

Hebu fikiria Mtu ameweza kubeba Ujauzito kwa muda wa miezi Tisa, kisha akaja kujifungua kwa usalama.

Baadae huyo huyo aliepitia tabu zote hizo, anaenda kutelekeza Watoto wake aliowapatia tabu.

Huyo Mama wamuangalie jamani.

Pengine amepatwa na matatizo ya kurukwa na Akili.

Maana kurukwa na Akili kunapishana, wengine wanaanza taratibu (pengine ndio yupo kwenye hatua za mwanzo).

Wasimuhukumu moja kwa moja, wamuangalie kwanza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya mambo yanawezekana.

Matukio mengi yanafanywa kwa sababu ya matatizo ya kiakili.

Bahati mbaya wengi kutokana na ubinafsi wa hali ya juu kabisa,wanaikataa situation halisi(self denial) na hivyo kushindwa kuchukua hatua stahiki.

Mfano hawa wanaoishi kwa kudanga mjini,kipindi cha kabla ya corona ukiwaambia wauze japo uji au mihogo kuliko kuishi kwa kudanga tu,wanaweza kukupa tusi hadi ujidharau.Ila sasa hivi hao madanga yao wana hali ngumu,wengine wamejifungia ndani,ukikuta mtu kama huyu,mfano wanaodanga kwa madereva wa malori,hali ilivyo sasa hivi,madereva wenyewe wanakutwa na corona,hali inakuwa tete sana.Kama ana watoto,ataenda kwa nani?Ndio hapo atajikuta anakuwa chizi maana hawezi kufanya chochote kazoea kudanga

Sent using Jamii Forums mobile app
Naam Kiongozi.

Hapo kwenye kudanga inasikitisha kwa kweli.

Na mtu mwingine anakuwa hana jinsi sababu kudanga ndio tegemezi lake
 
ac66100e0ebe95b6eb87815a71c99aa6

Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza limemtia mbaroni mama mmoja aitwaye Happyness Mafuru, kwa tuhuma ya kuwatelekeza watoto wake wawili katika majaluba ya mpunga, huko mtaa wa Mtakuja kata ya Nyamhongolo wilayani Ilemela Jijini Mwanza.

Watoto hao wameokotwa wakiwa hai na kisha kupelekwa katika hospitali ya rufaa ya kanda Bugando Jijini Mwanza, ambako wanaendelea kuchunguzwa afya zao wakati uchunguzi dhidi ya tukio ukiendelea.

Watoto hao wameokotwa majira ya saa tisa usiku, huku baridi ikiwa ni yao na usalama ukiwa ni tishio la maisha yao, kama anavyosimulia Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Mtakuja Adamu Magina.

============

Ni dhahiri kuwa wapo wanaohitaji watoto lakini hawajabahatika kuwapata, na waliobahatika wanashindwa kushukuru kwa kupata bahati hiyo ya mtende, lakini Je, ni hatua zipi zitafuata kwa Happynes na mumewe?

Kwa wenye kufahamu majaluba ya mpunga, katika kipindi hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha nchini majaluba mengi yamejaa maji, hivyo unaweza kupata picha, jinsi watoto hao walivyokuwa wakikabiliwa na wakati mgumu kunusuru uhai.
Huko ziwani watu ni wakatili sana.
 
Back
Top Bottom