Mwanza: Mfalme Zumaridi, wenzake wafikishwa mahakamani, ajifunika uso kwa kitenge

Mwanza: Mfalme Zumaridi, wenzake wafikishwa mahakamani, ajifunika uso kwa kitenge

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Diana Bundala maarufu kama 'Mfalme Zumaridi' na wenzake 84 leo Alhamisi Machi 17, 2022 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza kusomewa maelezo ya awali katika mashtaka matatu ikiwamo usafirishaji haramu wa binadamu.

Makosa mengine ni pamoja na kusanyiko lisilo na kibali na kuzuia maofisa wa Serikali kutimiza wajibu wao.

Tofauti na alivyokuwa akifikishwa awali Mahakamani hapo alipokuwa akijiachia na kuwatania waandishi wa habari hasa wapigapicha, akijiita Mungu, safari hii ilikuwa tofauti ambapo akiwa ndani ya Mahakama alijifunika kwa kitenge wakati akipigwa picha na kuziba uso wake.

Washtakiwa hao wamefikishwa mahakamani hapo saa 6:00 mchana mbele ya ya Hakimu mkazi Mwandamizi wa Mahakama hiyo, Monica Ndyekubora.

Mchungaji huyo kutoka Mwanza amepata umaarufu mkubwa kwenye mitandao ya kijamii Instagram na YouTube akionekana anacheza huku baadhi ya video zikimuonesha ‘akisujudiwa’ na waumini wake.

Ni nadra sana kwa mwanamke kutumia jina ama cheo cha mfalme bali ni malkia, lakini kwa mchungaji huyu anaitwa kwa cheo hicho.


mfalmeepiic.jpg
Diana Bundala maarufu kama 'Mfalme Zumaridi' akiwa amejifunika kitenge ndani ya chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza kwa ajili ya kusomewa hoja za awali za mashtaka matatu yanayowakabili na wenzake. Picha na Mgongo Kaitira

Source: Mwananchi

Pia Soma>>>
 
Inawezekana sasa mashetani yaliyokuwa ndani yake yametimka, labda ameombewa na watumishi wa Mungu wa kweli na hatimaye muungu zumaridi ametoka sasa amebaki Diana.

Na kweli huyo ndiye Diana, hapo awali alikuwa amebeba mapepo ya kishetani yaliyo mbatiza jina mungu zumaridi.
 
Aibu kweli, pamoja na kujiita mfalme na majina kadhaa ya kiungu lakini ameshindwa kujifanyia muujiza hata wa kujigeuza upepo,magereza watakapofungua mlango wa selo waambulie inzi na mbu wakati mwenyewe ameshasepa zamani.
 
Diana Bundala maarufu kama 'Mfalme Zumaridi' na wenzake 84 leo Alhamisi Machi 17, 2022 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza kusomewa maelezo ya awali katika mashtaka matatu ikiwamo usafirishaji haramu wa binadamu...
Kuna mwanamama mwingine naye amepewa cheo cha uchifu. Wasemaje hapo?
 
Inawezekana sasa mashetani yaliyokuwa ndani yake yametimka, labda ameombewa na watumishi wa Mungu wa kweli na hatimaye muungu zumaridi amefika sasa amebaki Diana.


Na kweli huyo ndiye Diana, hapo awali alikuwa amebeba mapepo ya kishetani yaliyo mbatiza jina mungu zumaridi.
Hakuna cha maombi wala nini, ingekuwa ni maombi ya watumishi mapepo yangekuwa yamemtoka siku nyingi hata kukamatwa asingekamatwa.

Kilichotoa ufalme wake fake na wa kishetani ni virungu vya polisi na magereza.
 
Aibu kweli, pamoja na kujiita mfalme na majina kadhaa ya kiungu lakini ameshindwa kujifanyia muujiza hata wa kujigeuza upepo, magereza watakapofungua mlango wa selo waambulie inzi na mbu wakati mwenyewe ameshasepa zamani.
Walahi umenifanya nicheke kwa sauti. Eti ange perform Miracles & Wonders🤣🤣
 
Back
Top Bottom