Mwanza: Watu 6 wafariki kwa kugongwa na gari wakifanya mazoezi

Mwanza: Watu 6 wafariki kwa kugongwa na gari wakifanya mazoezi

Nina ndugu yangu anafanya mazoezi na rafiki zake nilimshaurigi zaidi ya mara mbili asiwe anakimbia (jogging) kwenye barabara au makazi ya watu angalau upate kiwanja mbona unafanya vizuri tu.

Sababu ya kumshauri kulishatokea tukio maeneo ya G5 mtu alikua anafanya tizi la mbio jioni katoka ufukweni zikapigwa kelele za mwizi mwamba hakupona.
Pili barabarani ndio kama hivyo mtu anaweza poteza uthibiti wa gari na mambo yakawa mengine.

Tujijali kila muda yuthamini kidogo haya maisha tuliopewa.
Siyo powa alooh nimeacha rasmi achakitambi kije
 
Ruuh mimi na masela tunapasha kila siku road ya malimbe kuanzia Jeshini mpaka Saut chuoni ipo siku yetu tu gari litapita na sisi kmk tuuliwe kwasababu ile road walevi ni wengi

Hasa mimi naekimbiaga kama kichaa ipo siku gari litanivunja miguu kama sio kuniua...kuacha ndo siwezi
 
Hiyo barabara ya 77 kwenda Buswelu ni mpya na imejengwa vizuri sana kiasi cha kumvutia dereva kwenda mwendo wa speed , changamoto ya hiyo barabara ni nyembamba na ina kingo pande zote hapana pa kuchepukia, mwenyewe nimewahi kukosakosa mtu hapo Kiseke na kibaiskeli chake
 
Ni wakati sasa serikali irusishe maeneo ya wazi miji iwe na city parks watu wawe wanaenda kufanya mazoezi huko pia barabara ziongezwe kuweka nafasi ya wakimbia kwa miguu na waendesha baiskeri.
Inarudisha kutoka wapi wakati wameruhusu wavamizi?
 
Leseni yake ifungiwe, huu ni uzembe wa hali ya juu sana.
... Uchunguzi wa kina ufanywe kujua chanzo cha ajali na sio blah blah zilizotolewa eti "mwendokasi" kana kwamba kuna mtu alikuwa anapima speed aliyokuwa akiendeshea. Hakuna mtu anayeamka asubuhi nyumbani kwake kwenda kuua watu barabarani; never!
 
Kuna MTU alishaandika humu kua ni harari kufanya mazoezi kando ya high way
... sio tu hatari kufanya mazoezi barabarani; bali pia barabarani sio sehemu ya kufanyia mazoezi! Mbele ya macho ya sheria wote hao wana makosa kwa kuhatarisha usalama wa vyombo vya moto na watumiaji wengine wa barabara kisheria. Mark my words; by saa nne asubuhi kesi itakuwa imetupiliwa mbali na mahakama.
 
Watu 6 wamefariki dunia na wengine 14 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari binafsi, ambalo limewagonga wananchi waliokuwa wakifanya mazoezi kandokando ya barabara eneo la Sabasaba Ilemela Mwanza leo Julai 22, 2023 majira ya asubuhi.


=====
Taarifa za awali ni kwamba Watu 6 wamefariki dunia na wengine 14 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari binafsi, ambalo limewagonga wananchi waliokuwa wakifanya mazoezi kandokando ya barabara eneo la Sabasaba Ilemela, Jijini Mwanza.

Chanzo cha ajali ni mwendokasi na Dereva kutozungatia Sheria na alama za barabarani.

Miili ya Waliofariki na Majeruhi wa ajali wamepelewa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou toure.

============

UPDATES...
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Gideon Msuya “Imetokea katika Wilaya ya Ilemela, gari aina ya Toyota Hilux lenye namba za usajili T476 DZL ikitoka Sabasaba kuelekea Buswelu ilipoteza mwelekeo kutokana na mwendokasi na kusababisha ajali iliyoua watu 6, kujeruhi 14 waliokuwa wakifanya mazoezi ya kukimbia ambapo jumla yao walikuwa 27.

"Majeruhi wanne wapo Hospitali ya Bugando, wengine 10 wapo Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Sekou Toure.

“Juhudi za kumtafuta Dereva zinaendelea kwa kuwa alikimbia mara baada ya tukio hilo.”
Pole Sana kwa wafiwa.
Haijapita hata mwezi mmoja tangu mwamba mmoja atuonye hapa jamii forum , kuhusu hatari za kufanya mazoezi barabarani.
Watanzania tuwe tunatii tunapoonywa, hatujui kuwa Mungu huzungumza na watu kupitia watu??
 
... Uchunguzi wa kina ufanywe kujua chanzo cha ajali na sio blah blah zilizotolewa eti "mwendokasi" kana kwamba kuna mtu alikuwa anapima speed aliyokuwa akiendeshea. Hakuna mtu anayeamka asubuhi nyumbani kwake kwenda kuua watu barabarani; never!
Usiseme NEVER. Kuna kitu kinaitwa
"Changamoto ya afya ya akili"
 
Watu 6 wamefariki dunia na wengine 14 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari binafsi, ambalo limewagonga wananchi waliokuwa wakifanya mazoezi kandokando ya barabara eneo la Sabasaba Ilemela Mwanza leo Julai 22, 2023 majira ya asubuhi.


=====
Taarifa za awali ni kwamba Watu 6 wamefariki dunia na wengine 14 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari binafsi, ambalo limewagonga wananchi waliokuwa wakifanya mazoezi kandokando ya barabara eneo la Sabasaba Ilemela, Jijini Mwanza.

Chanzo cha ajali ni mwendokasi na Dereva kutozungatia Sheria na alama za barabarani.

Miili ya Waliofariki na Majeruhi wa ajali wamepelewa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou toure.

============

UPDATES...
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Gideon Msuya “Imetokea katika Wilaya ya Ilemela, gari aina ya Toyota Hilux lenye namba za usajili T476 DZL ikitoka Sabasaba kuelekea Buswelu ilipoteza mwelekeo kutokana na mwendokasi na kusababisha ajali iliyoua watu 6, kujeruhi 14 waliokuwa wakifanya mazoezi ya kukimbia ambapo jumla yao walikuwa 27.

"Majeruhi wanne wapo Hospitali ya Bugando, wengine 10 wapo Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Sekou Toure.

“Juhudi za kumtafuta Dereva zinaendelea kwa kuwa alikimbia mara baada ya tukio hilo.”
Ajali haina kinga. R.I.P
 
Back
Top Bottom