Mwanza: Waziri Mkuu azuia paspoti 7 za wakandarasi wa Meli ya MV Mwanza

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amefanya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa Meli ya MV. Mwanza ‘Hapa Kazi Tu’ na kubaini ukiukwaji wa makubaliano ya kimkataba ya ikiwa ni pamoja na Kampuni ya Korea ya Gas Entec Building Engineering iliyo na jukumu la kujenga meli hiyo kuuza sehemu ya jukumu la ujenzi kwa kampuni nyingine.

Hali hiyo imesababisha ujenzi kukomea katika kiwango cha 65% badala ya 95% kwa mujibu wa makubaliano ya muda wa kukamilisha ujenzi wa Meli.

Aidha, inadaiwa kampuni hiyo imepunguza Wafanyakazi kutoka 118 hadi kubakia 22 hali inayosababisha ujenzi wa Meli kutokamilika kwa wakati ambapo Serikali tayari imelipa fedha kwa asilimia 80 hadi sasa.

Waziri Mkuu baada ya kubaini mapungufu hayo ameagiza Uhamiaji Mkoa wa Mwanza kuzuia kwa muda hati za kusafiria za raia saba wa Korea Kusini wanaojenga Meli hiyo na kuagiza wasiondoke nchini hadi wakamilishe ujenzi wa Meli ya MV. Mwanza.

Ujenzi wa Meli ya MV. Mwanza ‘Hapa Kazi Tu’ utagharimu zaidi ya bilioni 97.5 za Kitanzania.
 
Yote hii ni sababu usimamizi wa serikali ya Samia kulegalega kwenye usimamizi wa miradi hii mikubwa ya kimkakati.
 
MTAKUJA KUJENGEWA MELI MUOGO MZAME NAYO KWA UTAHIRA WENU..!

MIAKA 6O YA UHURU HAMNA MAINGINIA WA KUJRLENGA MELI.
Akili yako inalingana na ulichokiandika!
 
Uyo jamaa akiongea jambo, Kaa nalo kwanza lifanyie utafiti. MWANZO ktk jitihada za kufuta legacy walikatisha malipo yote na hd vibarua walifukuzwa.
 
I
ID yako tu ,kaka yangu.Umenifurahisha.Nitajadili mada baadae
 
Kishasahau kuhusu bidhaa na mafuta kupanda bei?
 
Uyo jamaa akiongea jambo, Kaa nalo kwanza lifanyie utafiti. MWANZO ktk jitihada za kufuta legacy walikatisha malipo yote na hd vibarua walifukuzwa.
Haiingii akilini kabisa, kontracta afanye alivyofanya bila kuwepo na sababu ya kufanya alichofanya.

Naegemea zaidi kuamini ulichoandika hapa.

Hawa watu wanaweza kuwa wanafanya siasa kwenye mambo ya namna hii?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…